Tangazo hili la Equality For Growth linadhalilisha wanawake

Tangazo hili la Equality For Growth linadhalilisha wanawake

dafity

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2008
Posts
1,881
Reaction score
2,091
Nimekutana nayo hii habari Facebook na kwa kweli hili tangazo linadhalilisha wanawake. Silipendi kweli. Mwenye "Audio" yake iweke hapa please.

Linatangazwa sana kwa sasa na limeandaliwa na wanaojiita "EQUALITY FOR GROWTH" likidhaminiwa na "UN Trust Fund".

Lengo lao ni kukataa kuwatukana na kuwadhalilisha wanawake lakini kwa bahati mbaya wao ndio wanawatukana waziwazi kwenye tangazo hilo.

Kwenye tangazo anasikika mwanaume akienda kunywa supu kwenye kibanda cha mwanamke lakini yule mwanaume alivyodaiwa pesa akaanza kuporomosha matusi ya kikwelikweli ambayo hapa siwezi kuyaandika. Matusi ambayo watoto huyasikia na kujifunza kitu kibaya kutoka redioni.

Nashauri TCRA walifungie hili tangazo haraka kama walivyofungia baadhi ya nyimbo zisizo na maadili.

HAWAKUPASWA KUTUKANA KIKWELIKWELI ILI KUNOGESHA TANGAZO. TUSI NI TUSI TU. WAWE NA ADABU!
 
Binafsi hilo tangazo linanikera sana, at least lingeisha kwa vidume wengine kumshushia kipigo huyo mropokaji.
 
Ngoja mtukufu wetu atalishughulikia
 
Mi ndo hapo mnaponifurahisha wanawake kusema mnadhalilishwa,huko mitaani hamuoni wenzenu wengine wakiwadhalilisha mkiona kawaida nenda kwenye vigodoro hamuoni mnayoyafanya? Angalia mavazi mnayoyavaa kawaida tu eeeenh!,kwenye instagram ndo usiseme ukifungua tu utakutana na video inayowaoyesha mkicheza huku mkitingisha makalio kawaida tu eeeenh! Huku mwaona ndo fasion, na ukifanya hivyo upo sambamba na mabadiliko ya dunia,n.k ,hayo yote hamyaoni? Mjitambue kwanza na uufaham utu wako na hapo ndio utakapotoa nafasi ya jamii ya wengine kukuheshimu,angalieni wenzenu nchi zinazoishi kwa misingi ya huoni wakijidhalilisha lkn nyie huku mkiona wenzenu huko kama wananyanyasika na huku mkipaza sauti wao wawe kama nyie mlioshindikana ktk familia/jamii zenu(baadhi yenu)
 
mfano kiduchu wa "tusi"

'Pumbavu'
Sidhani kama ni kubwa namna hiyo mpaka mwandishi ashindwe kuliweka maana nakumbuka kuna kiongoz mmoja mkubwa kabisa wa nchi alishalitumia hili na wala haikuleta shida yoyote.
Tungeshadadia kipindi kile hata mimi ningekubaliana na wewe kuwa ni tusi ila si kwa sasa.
 
supu yenyewe maji pwa ya kizipompa pompa kimpompile pampapa!
 
'Pumbavu'
Sidhani kama ni kubwa namna hiyo mpaka mwandishi ashindwe kuliweka maana nakumbuka kuna kiongoz mmoja mkubwa kabisa wa nchi alishalitumia hili na wala haikuleta shida yoyote.
Tungeshadadia kipindi kile hata mimi ningekubaliana na wewe kuwa ni tusi ila si kwa sasa.

hilo tu ndio mleta uzi anasema matusi! hahahahahaahah!
 
Mi ndo hapo map on I fur Aisha wanawake kusema mnadhalilishwa,huko mitaani hamuoni wenzenu wengine wako was halo maisha mkiona kawaida nenda kwenye vigodoro hamuoni mnayoyafanya? Angalia mavazi mnayoyavaa kawaida tu eeeenh!,kwenye instagram ndo usiseme ukifungua tu utakutana na video inayowaoyesha mkicheza huku mkitingisha makalio kawaida tu eeeenh! Huku mwaona ndo fasion, na ukifanya hivyo upo sambamba na mabadiliko ya dunia,n.k ,hayo yote hamyaoni? Mjitambue kwanza na uufaham utu wako na halo ndio utakapotoa nafasi ya wengine kukuheshimu.

Aisee, nitakutafuta unywe soda! Huo ndio Ukweli kabisa uliosema! Sijui huwa hawaoni wanawake wenzao mtaani huku walivyo, wanatembea nusu uchi au saa nyingine ni uchi kabisa, wamekuwa bidhaa nyepesi nyepesi tu, wanafanya mambo ya kujidhalilisha zaidi ya hata tangazo hilo, nimeliona hilo tangazo halina tatizo lolote!
 
Aisee, nitakutafuta unywe soda! Huo ndio Ukweli kabisa uliosema! Sijui huwa hawaoni wanawake wenzao mtaani huku walivyo, wanatembea nusu uchi au saa nyingine ni uchi kabisa, wamekuwa bidhaa nyepesi nyepesi tu, wanafanya mambo ya kujidhalilisha zaidi ya hata tangazo hilo, nimeliona hilo tangazo halina tatizo lolote!
Wanajidhalilisha wenyewe halafu wanataka kuheshimiwa
 
7eabb568ed55d455bd8433f926efe870.jpg
nani apoteze muda wa kukuheshimu kwa aina hii
 
Ebu nendeni mka mueleze mkurugenzi wa Equality for Growth, anapatikana pale buguruni sheli, kwenye jengo la wasomali, pale chini Kuna duka la dawa na pia wanaoka mikate.
Panda ghorofa ya kwanzaa kisha ulizia Jane
 
Tangazo liko sahihi kulingana na kile kinachozungumziwa.Watz huwa hatupendi kuambiwa ukweli na hayo ni maisha ya kina mamantilie wengi wananyanyaswa sana na wateja wao!..KUBALINI UKWELI ILI MJIREKEBISHE.
 
298ca42ce549fa8b391b026a990355b6.jpg
aina hii ndo tunawakuza watoto zetu tutegemee Mani aje aone thamani ya mtoto huyu ukubwani kwake tena mzazi unaona ukimvalisha nguo za star a unaona utaonekana mshamba,mabadiliko yaanzie kwako na jamii nayo itafuata,nimechunguza hili huwezi kukuta jamii kama za kiislam zinazofuata misingi ya dini zao kwa mavazi yao ya kawaida tu mabaibui yao unawafurahia kabisa au kwa pande zetu wengine masister kanisani maisha yao safi kabisa na hawapungukiwi kitu kwao wala ktk jamii inatowahusu zaidi ya kuthaminika kwa utu wao,sasa wale walioshindikina kwenye kutamani hata pasiwepo nguo kama Gigi money nae aje kulalamika mnadhalilishwa?,Mbadilike.
 
Back
Top Bottom