Mwiba
JF-Expert Member
- Oct 23, 2007
- 7,607
- 1,760
Baada ya kusikiliza mkutano wa Paje -Unguja niliiona wazi njia ya Zanzibar kujikwamua na ukoloni Tanganyika ni nyeupe ,na gea walioondokea na mkutano huu wa Paje kwa kweli wamekusudia kwa hali yeyote ile Mamlaka kamili ya Zanzibar yanarudi chini ya Uongozi wa CUF.
Hisia kali zinazotolewa na Katibu Mkuu wa CUF ni hisia ambazo kila Mzanzibari mzalendo ataungana nae na haswa aliposema CCM wajiandae kisaikolojia kwani ushindi mkubwa ambao utavuka kiwango utaiangamiza CCM.
Jingine ni pale alipotangaza waziwazi kuwa Serikali itakayoongozwa na CUF haitafuata wala kusikiliza firimbi zitakazopulizwa Tanganyika aka Serikali ya Muungano ,wao kama WaZanzibari watakuwa na maamuzi yao kiserikali na hawatamsikiliza yeyote yule kutoka nchi nyingine (Tanganyika).
Hotuba yake imejenga matumaini 100% kwa WaZanzibari na imetangaza kuwa miezi tisa ijayo ni kuiangamiza CCM Zanzibar' kama una nafasi sikiliza hiki kipande sehemu ya mwisho baada ya Mansori. Ameukandia utawala wa mafisadi na kudai hakuna kitakachozuia CUF isiongoze Zanzibar ,hakuna na atakae jaribu atajuta.
Hisia kali zinazotolewa na Katibu Mkuu wa CUF ni hisia ambazo kila Mzanzibari mzalendo ataungana nae na haswa aliposema CCM wajiandae kisaikolojia kwani ushindi mkubwa ambao utavuka kiwango utaiangamiza CCM.
Jingine ni pale alipotangaza waziwazi kuwa Serikali itakayoongozwa na CUF haitafuata wala kusikiliza firimbi zitakazopulizwa Tanganyika aka Serikali ya Muungano ,wao kama WaZanzibari watakuwa na maamuzi yao kiserikali na hawatamsikiliza yeyote yule kutoka nchi nyingine (Tanganyika).
Hotuba yake imejenga matumaini 100% kwa WaZanzibari na imetangaza kuwa miezi tisa ijayo ni kuiangamiza CCM Zanzibar' kama una nafasi sikiliza hiki kipande sehemu ya mwisho baada ya Mansori. Ameukandia utawala wa mafisadi na kudai hakuna kitakachozuia CUF isiongoze Zanzibar ,hakuna na atakae jaribu atajuta.
Last edited by a moderator: