Tanesco tuokoeni tunaumia sana

KIBURUDISHO

JF-Expert Member
Mar 28, 2011
1,002
274
Wakuu heshima iwe kwenu.
Waswahili husema ugumu wa maisha kipimo cha akili sidhani kama usemi huu ni sahihi sana.Mwenzenu baada ya purukushani na baba mwenye nyumba hatimae kwa sasa "nimehamia mtaa wa saba toka kule nilikokuwa nikiishi zamani........"!!
Niende moja kwa moja kwenye mada baada ya mwenzenu kufanikiwa kuhamia mtaa wa saba changamoto niliyokutana nayo ni hatari ya vyombo vyangu vitumiavyo umeme kugeuka mazalia ya viumbe hai kama vile wadudu na si binadamu.Nimekwenda kubisha hodi kwenye shirika letu hili la umma yaani Tanesco kwa ajili ya kuvinusuru vifaa vyangu vitumiavyo umeme visigeuke vichaka mtumishi wa tanesco kaja kanipimia zinahitajika nguzo nne ili niweze kupewa umeme mfukoni kiasi nilichonacho hakitoshi maana nguzo tatu tu zinagharimu sh 1,300,000/= ya nne sikujua itakuwa sh ngapi nikawacheki majirani zangu wawili kila mmoja ni chenga wanapiga wakiwa na taget kwamba nihangaike mimi ili wao waje wavute kiulaini nimefikiria sana nimeshindwa nifanye mbinu ipi ili niweze kuupata umeme.
Nilipofikia hapo nikapata wazo fulani japokuwa wazo hilo halitakuwa msaada kwa muda muafaka ila litakuwa limewapa mwanga fulani wahusika wa shirika letu.Kuna makampuni fulani ya solar kama vile Mobisol au Mpower nk yanayomkopesha mteja kwanini shirika letu lisiige huo mfumo kwasababu tulio wengi hatuna pesa ya kulipia kuunganishiwa umeme kwa mara moja.Ningewashauri Tanesco waweze kuwa na mkopo wa kuwakopesha wateja huduma ya kuunganishiwa umeme kwa mkopo wa muda fulani kadri watakavyokuwa wanaona inafaa endapo kama mteja atachelewa kulipia deni lake system yenyewe inamkatia mteja umeme hadi hapo atakapolipia deni ndio huduma inarudi.Natumai kwa utaratibu huu shirika litapata wateja wengi mbinu ambayo makampuni ya soral yamekuwa yakijizolea wateja wengi.
 
  • Thanks
Reactions: SIM
Mkuu hili shirika linakera kweli kweli. mfano hapa mkoani kilimanjaro kuna eneo lina wakazi zaidi ya elfu mbili lakini cha ajabu tanesco hawataki kuleta umeme ni zaidi ya miaka miwili sasa wenzao wa maji walishafikisha huduma siku nyingi. hivi kinawashinda nini kupitisha laini kubwa barabara kuu na sisi wateja tuingie gharama ya kuuvuta kuuingiza mtaani kwetu au mnataka na hii lain kuu tulipie sisi ndipo mfikishe huduma??? acheni hizo bana tuleteeni umeme wakazi wa Shabaha mabogini
 
Mkuu hiï mada inaniîhusu moja kwa moja.Kwangu alikuja surveyor kutoka Tanesco akapima tukapata ni nguzo tano.cha ajabu hesabu ikaja ni 3,332,500.Yaan nilishndwa kuelewa hizo hesabu zao wanapigaje kwa sababu ukiuliza bei ya nguzo moja watakwambia ni 260000 sasa ni kigezo gani kilitumika mpaka kufanya hesabu iwe kubwa kiasi hicho?
 
Mkuu hili shirika linakera kweli kweli. mfano hapa mkoani kilimanjaro kuna eneo lina wakazi zaidi ya elfu mbili lakini cha ajabu tanesco hawataki kuleta umeme ni zaidi ya miaka miwili sasa wenzao wa maji walishafikisha huduma siku nyingi. hivi kinawashinda nini kupitisha laini kubwa barabara kuu na sisi wateja tuingie gharama ya kuuvuta kuuingiza mtaani kwetu au mnataka na hii lain kuu tulipie sisi ndipo mfikishe huduma??? acheni hizo bana tuleteeni umeme wakazi wa Shabaha mabogini



sehemu gani hio arusha
 
Mkuu hiï mada inaniîhusu moja kwa moja.Kwangu alikuja surveyor kutoka Tanesco akapima tukapata ni nguzo tano.cha ajabu hesabu ikaja ni 3,332,500.Yaan nilishndwa kuelewa hizo hesabu zao wanapigaje kwa sababu ukiuliza bei ya nguzo moja watakwambia ni 260000 sasa ni kigezo gani kilitumika mpaka kufanya hesabu iwe kubwa kiasi hicho?



ilikuwa wapi mkuu hio gharama yote
 
Back
Top Bottom