Bondpost
JF-Expert Member
- Oct 16, 2011
- 6,594
- 9,338
Ndugu zangu TANESCO walisema LUKU itapandisha mapato ili waweze kutoa huduma bora, watanzania tukakubali wafanye hivyo lakini matokeo yake ni yaleyale.
Wakaja na maombi ya kupandisha bei kwa viwango mbalimbali, matatizo ndio yameongezeka.
Sasa umeme ndio umekuwa wimbo miongoni mwa watanzania, kukatika kusiko na ukomo, umeme bei juu, ukinunua umeme wa elfu kumi unapata units 36 tu hapo wakikata ile service charge yao ambayo service hatuioni ndio umeumia.
Hivi tunakoelekea wapi? Sasa hivi maeneo kadhaa ya huku mbezi juu hakuna umeme, na toka asubuhi walikata, samaki, nyama sasa zilizokuwa kwenye fridge imebidi kununua ice blocks kuweka kwa fridge. Nawaza wale wenye biashara za kutegemea umeme!
Hivi kweli hakuna strategy madhubuti za kuweza kudhibiti hali hii? Mbona nahisi kuna uzembe tu na ukiritimba?
Mungu atusaidie, ila TANESCO wanatuumiza wananchi, bei ya umeme wamepandisha na matatizo ni yaleyale, i guess wao hawaishiwi visingizio.
TANESCO hebu kuweni makini kibiashara.
Wakaja na maombi ya kupandisha bei kwa viwango mbalimbali, matatizo ndio yameongezeka.
Sasa umeme ndio umekuwa wimbo miongoni mwa watanzania, kukatika kusiko na ukomo, umeme bei juu, ukinunua umeme wa elfu kumi unapata units 36 tu hapo wakikata ile service charge yao ambayo service hatuioni ndio umeumia.
Hivi tunakoelekea wapi? Sasa hivi maeneo kadhaa ya huku mbezi juu hakuna umeme, na toka asubuhi walikata, samaki, nyama sasa zilizokuwa kwenye fridge imebidi kununua ice blocks kuweka kwa fridge. Nawaza wale wenye biashara za kutegemea umeme!
Hivi kweli hakuna strategy madhubuti za kuweza kudhibiti hali hii? Mbona nahisi kuna uzembe tu na ukiritimba?
Mungu atusaidie, ila TANESCO wanatuumiza wananchi, bei ya umeme wamepandisha na matatizo ni yaleyale, i guess wao hawaishiwi visingizio.
TANESCO hebu kuweni makini kibiashara.