Mkulima wa Kuku
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 1,270
- 536
Tangu jana mchana wote haukuwa na umeme hadi muda huu niandikapo uzi huu. Sina taarifa ya kilichotokea ila ni kawaida sana Tanesco kufanya hichi walichokifanya. Aidha kuna maeneo kuna low voltage kiasi kwamba tumepata hasara nyingi ya mali sababu ya inconsistency ya umeme wao. Tumelalamika juu ya suala la low voltage hawajibu....Tunamuomba Mh. Magufuli aingilie kati kwani tumelipia ili tupate umeme mkamilifu si unaozidi au kupungua. Umeme kwa wengi wetu ni maisha, ni uchumi, ni kila kitu. Tunataka haki yetu ya kupata 220-240 V na si vinginevyo. Pengine kama haiwezekani tuamini kuwa kuna madaraja ya wanaostahili kupewa umeme toshelevu na wasistahili