TANESCO Mwanza, hamjui kuwa mnatuharibia biashara zetu?

MNFUMAKOLE

JF-Expert Member
Nov 14, 2014
1,400
1,706
TaANESCO Mwanza mmekuwa kero kubwa! Hususani maeneo ya Malimbe. Kila siku mnakata umeme. Hivi hamjui kuwa mnatuharibia biashara zetu? Kweli tutafika Tanzania ya viwanda kwa mwendo huu? Au mmetumwa na mabeberu kumhujumu Baba Jesca?

Medard Kalemani chunguza meneja Tanesco mkoa wa Mwanza. Hastahili kuwa meneja!

Mtafutie wilaya, hana uwezo wa kumenege mkoa! Anaharibu biashara zetu! Mpaka muda huu naandika hiii mada, huku Malimbe tuko gizani!! Umeme umekatika toka saa Saba usiku!

Waziri komesha hii kadhia! Tanesco wanatuharibia biashara zetu!
 
Usiku wamekata! kuanzia saa saba, wakarudisha saa kumi na mbili. Sasahivi yamekata tena!! Tanesco ni mawakala wa shetani!!
 
Lakini Raisi si alisema mgao kwisha habari yake, imekuaje tena?
 
Mkuu TANESCO ni shida karibu nchi nzima.Na kwa kipindi ambacho kulikuwa hamna waziri wa Nishati hali ilikuwa mbaya sana.Sasa waziri kateuliwa nadhani atasimamia shoo hadi kieleweke.
 
Wanakata umeme

Ukirudi unit zimetumika unajiuliza umeendaje wakati ilikuwa umekata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…