The mountain lion
JF-Expert Member
- Oct 6, 2014
- 1,153
- 418
Ila kusema kweli hii nchi imeoza sana.Halafu bado kuna mambumbumbu humu JF wanatetea upuuzi wa serikali ya Chama cha Mamburula kisa tu wanapewa buku saba.
Umeme unakwenda sana mm natumia kwa siku unit 8 na nyumba yakawaida tu taa na tv hata feni situmii nipo karibu na beach sasa sijui nini tatizo
Sio kosa lao mkuu, wanapaswa kulipa sh. mil 200 daily watumie umeme au wasitumie, na mkataba wa IPTL umeongezwa muda.. sasa hizo hela watazipata wapi??? kwa hiyo ndo tunasaidiana kulipa deni.. tuvumilie tu labda maumivu haya kuna siku yatatupa akili ya kujua kura ni kitu gani..
Umeme ni moja ya huduma muhimu katika maisha ya kila siku. Kwa Tanzania huduma hii inatolewa na kusimamiwa na TANESCO. Tunashukuru kwa huduma zinazotolewa na shirika hili. LAKINI kwa upande wa gharama ya matumizi ya nishati hii ndo kilio kwa Watanzania tulio wengi! Gharama ya Umeme ni KUBWA MNO, MNATUUMIZA!
Tunaomba muweke wazi tarrifs (makato) zenu! Mnadai mmetenganisha tarrifs za mtumiaji mdogo na mtumiaji mkubwa ambapo: Mtumiaji mdogo mmesema ni yule anayetumia umeme chini ya unit 75 kwa mwezi na anapaswa kulipia Tsh 100 kwa unit; Na mtumiaji mkubwa mmesema ni yule anayetumia umeme zaidi ya unit 75 kwa mwezi na anapaswa kulipia Tsh 350 kwa unit.
Nasema mnatuibia kwasababu; mbona mnatutoza gharama ya mtumiaji mkubwa ilihali baadhi yetu ni watumiaji wadogo? Kwa mfano MIMI mwenyewe toka nimeingiza umeme matumiz yangu kwa mwezi hayazidi unit 70 kwa mwezi na mnatoza gharama ya mtumiaji mkubwa! Na kibaya zaidi hamtozi Tsh350 kwa unit badala yake mnatoza 375 na point kadhaa! Acheni kutuibia bwana!
Nawasilisha wadau
Bado ishu ya Service charge.
Ni kweli tanesco ni wezi hapo walitutega walipobadilisha tarrifs zao walibadilisha pasipo kufanya utafiti ili kujua mita gani itozwe viwango vya mtumiaji mdogo,wa kati,au mkubwa hivyo kama wewe unatumia chini ya unit 75 kwa mwezi inabidi uende ofisi za tanesco za mkoa au wilaya uendea na mita namba na uwaeleze kuwa unatumia units chini ya 75 kwa mwezi kisha watakupa fomu ujajeze na watahakikisha kwenye system zao kama kweli unatumia units hizo ni kisha wanakubadilishia,sema tatizo je ni wangapi wanajua hilo na kulifuatilia?je huo muda wakufuatilia nani anakulipa?
Kama unatumia UMEME chini ya Unit 70 kwa mwezi na umetumia zaidi ya miezi 3 andika barua kwa Tanesco na upeleke kwenye office zao za mkoa uliopo watakubadilishia Tariff.
mkuu emu nielekeze hii service charge gharama yake kwa mwezi huwa ni kiasi gani
Hivi capacity charges si ilikuwa ni ya miaka 20 au nakosea? Maana yangu ni kwamba sio ya kudumu hata ikinunuliwa na mtu mwingine, sana sana huyo mwingine anapata investment relief? Au ndio kizungumkuti chenyewe?
mkuu emu nielekeze hii service charge gharama yake kwa mwezi huwa ni kiasi gani
Let's kokotoa matumizi kwa siku:
Kifaa Power(kw) Muda(hrs) unit
Fridge 0.3 10* 3
Taa 5 0.2 5 1
TV. 0.15. 5 0.75
Pasi. 2. 0.2. 0.4
Jumla ya units kwa siku. 5.1
*Fridge kwa wastani lina nguruma chini ya dakika 30 kwa saa 1(on off operation) Hivo kwa masaa 24 litakuwa on kama masaa 10.
Usiwasahau na EWURA.Bado ishu ya Service charge.
Kwa sasa wanatoza Tsh 6734 na point kadhaa
Ukiwa na fridge kubwa ndani ya nyumba fahamu kuwa matumizi yako kwa mwezi yatazidi units 75. Ila mtu km mimi ambaye cna fridge ndan ya nyumba nilishafanya calculation nikaona matumizi yangu kwa siku hayazidi units 2.3