mfianchi
Platinum Member
- Jul 1, 2009
- 11,842
- 8,231
Nimekerwa na Tanesco mkoa wa Kinondoni Kaskazini pale Mikocheni, niliomba kuunganishiwa umeme kwenye kahekalu kangu pale Wazo,nimelipia kila kitu nikaahidiwa kuwa nitapigiwa simu kunitaarifu kuwa wanakuja kuunganisha huo umeme, naam kwanza baada ya mkaguzi kukagua uwekaji wa nyaya na kuridhia kuwa ziko sawa nikaambiwa nikalipie,lakini siku niliyoambiwa nikalipie nilikuwa busy ,walipoona muda unaenda nami sijaenda kulipia nikapigiwa simu siku hiyo hiyo kuwa natakiwa nikalipie hiyo 455,000.00.
Sasa naona shida yao tanesco imeisha baada ya kupata hiyo hela kwani hakuna umeme wala hata kupiga simu kunitaarifu kuwa tuna uhaba wa hizo mita. Leo nikaamua nipige kwata hadi hapo tanesco kwenda kuulizia kulikoni mbona sasa wiki iya pili inakatika na hamji kuunganisha huo umeme, jibu nililo ambiwa limeniacha hoi nimeambiwa nisubiri hadi mwezi ujao kwani kwa sasa hawana mita [LUKU] sasa najiuliza wakati wananipigia simu kuwa nikalipa hawakujua kama hawana hizo mita,kwani hiyo hele si ningezalishia kwa kuwekeza kwenye shughuli nyingine,kama hawakuwa na LUKU kwanini waliniharakisha kwa kunipigia simu kuwa nikalipe?
Hakika Tanesco wanakera sana. Kwa mambo kama haya yakizidi kuendelea sijui huo ufanisi utatoka wapi,kwa uzembe huu mimi naathirika zaidi ingawa wao Tanesco hawaoni hasara kukosa mapato kwani wanajua nipende au nisipende nitawasubiri tu.
Sijui niende EWURA kuwashitaki hawa watu?
Sasa naona shida yao tanesco imeisha baada ya kupata hiyo hela kwani hakuna umeme wala hata kupiga simu kunitaarifu kuwa tuna uhaba wa hizo mita. Leo nikaamua nipige kwata hadi hapo tanesco kwenda kuulizia kulikoni mbona sasa wiki iya pili inakatika na hamji kuunganisha huo umeme, jibu nililo ambiwa limeniacha hoi nimeambiwa nisubiri hadi mwezi ujao kwani kwa sasa hawana mita [LUKU] sasa najiuliza wakati wananipigia simu kuwa nikalipa hawakujua kama hawana hizo mita,kwani hiyo hele si ningezalishia kwa kuwekeza kwenye shughuli nyingine,kama hawakuwa na LUKU kwanini waliniharakisha kwa kunipigia simu kuwa nikalipe?
Hakika Tanesco wanakera sana. Kwa mambo kama haya yakizidi kuendelea sijui huo ufanisi utatoka wapi,kwa uzembe huu mimi naathirika zaidi ingawa wao Tanesco hawaoni hasara kukosa mapato kwani wanajua nipende au nisipende nitawasubiri tu.
Sijui niende EWURA kuwashitaki hawa watu?