Tamko la Tume ya Haki za Binadamu (THBUB) kuhusu matukio yanayohusiana na uvunjifu wa Haki za Binadamu yaliyotokea karibuni

Tamko la Tume ya Haki za Binadamu (THBUB) kuhusu matukio yanayohusiana na uvunjifu wa Haki za Binadamu yaliyotokea karibuni

Joined
Sep 17, 2024
Posts
26
Reaction score
28
Katika kipindi cha takriban mwezi mmoja na nusu, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imekuwa ikifuatilia kwa karibu matukio mbali mbali ambayo yamekuwa yakijitokeza nchini. THBUB baada ya kufanya tathmini kuhusu matukio hayo kwa mujibu wa Katiba na Sheria ya THBUB, imejiridhisha kuwa matukio hayo yanaashiria uvunjifu wa haki za binadamu, ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na uvunjifu wa amani na utulivu nchini.

Aidha, katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, kumekuwa na matukio mbali mbali yakiwemo matumizi ya lugha chafu zisizozingatia utu na heshima ya mtu na zinazoleta hamasa na kuchochea uvunjifu wa amani na utulivu, matukio yanayoashiria matumizi ya nguvu kupita kiasi wakati wa kushughulikia mikusanyiko ya kisiasa, kushambuliwa na kujeruhiwa kwa baadhi ya wananchi ikiwemo tukio lililotokea tarehe 30 Aprili, 2025 la kushambuliwa na kujeruhiwa Kiongozi wa Kidini Padre Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania na tukio la kutekwa kwa Faluka Saidi Nyagali kwa jina maarufu Mdude na matukio mengine.

THBUB inatambua kuwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi, sheria za nchi na mikataba mbalimbali ya kimataifa ya haki za binadamu ambayo Tanzania imeridhia, wananchi wote wa Tanzania wana haki ya kufurahia na kupata haki zao za binadamu. Aidha, kwa mujibu wa Katiba ya Nchi, kila mwananchi anayo haki ya kuishi, kuwa huru, kutoa maoni na kushiriki katika shughuli za umma moja kwa moja au kupitia wawakilishi kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa katika Katiba na sheria za nchi.

Pamoja na haki hizo, Katiba inaweka sharti la wajibu kwa kila mwananchi kutotumia misingi ambayo itasababisha kuingiliwa au kukatizwa kwa uhuru na haki ya watu wengine na kwamba pale mtu anapoamini kwamba haki yake imevunjwa anaweza kuwasilisha suala hilo Mahakamani au katika vyombo vyengine vyenye mamlaka kwa mujibu wa sheria.

Vile vile THBUB inatambua kuwa kwa mujibu wa sheria, Jeshi la Polisi limepewa dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao na hivyo kwa kuzingatia sheria na maadili, Jeshi hilo lina mamlaka ya kushughulikia viashiria vyote ambavyo vinaweza kuhatarisha amani na utulivu nchini.

THBUB inaona kuwa matendo yaliyojitokeza hayatoi taswira nzuri katika ustawi wa haki za binadamu, utawala bora na amani na utulivu nchini ambayo ni muhimu sana katika kipindi hichi kuelekea uchaguzi Mkuu. THBUB inalaani matukio hayo ambayo yamevunja haki za binadamu na kukiuka misingi ya utawala bora na yanayoashiria uvunjifu wa amani na utulivu.

Kutokana na matukio yaliyotokea THBUB inapendekeza yafuatayo:

a) Jeshi la Polisi ambalo ndiyo taasisi iliyopewa dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao kutekeleza wajibu wake kwa kufuata Katiba, Sheria na Kanuni;

b) Jeshi la Polisi liendelee kuwasaka na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika na kujeruhiwa kwa Dkt Charles Kitima, waliomteka Faluka Saidi Nyagali (Mdude) na waliohusika katika matukio mengine ya uvunjwaji wa haki za binadamu;

c) Msajili wa Vyama vya Siasa kuwataka viongozi wa vyama vya siasa kuzingatia matakwa ya Katiba na Sheria katika shughuli zao;

d) Serikali iendelee kukaa na wadau wa Demokrasia katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbali mbali zinazojitokeza;

e) Viongozi na wananchi waendelee kudumisha amani na utulivu ambao ndio msingi wa kufurahiya haki za binadamu; na

f) Wadau wote wa uchaguzi kuwa na ustahimilivu wakati wa mchakato wa uchaguzi kwa kuwa ushindani wa kisiasa nyakati za uchaguzi ndio chachu ya demokrasia.

Jukumu la Ulinzi na Utetezi wa Haki za Binadamu na uzingatiwaji wa misingi wa Utawala Bora ni letu sote.

WhatsApp Image 2025-05-05 at 14.23.19.jpeg
WhatsApp Image 2025-05-05 at 14.23.32.jpeg
WhatsApp Image 2025-05-05 at 14.23.46.jpeg

Pia, Soma
 
b) Jeshi la Polisi liendelee kuwasaka na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika na kujeruhiwa kwa Dkt Charles Kitima, waliomteka Faluka Saidi Nyagali (Mdude) na waliohusika katika matukio mengine ya uvunjwaji wa haki za binadamu;
Hapa ni tatizo na ndio maana mikono yote tunawanyooshea polisi, Suala la Ally Kibao kunyakuliwa na watu wenye mitutu hadharani kwenye basi mpaka leo kimya. Soka na wenzake kutekwa kituo cha polisi Chang'ombe mpaka leo hakuna uchunguzi wa kueleweka. Matukio ni mengi yanayolihusisha jeshi la Polisi hivyo nashauri tume huru iundwe kufuatilia haya yote. Polisi haiwezi kujichunguza.
 
Chadema wametoa taarifa Mdude katekwa na waowao ndo wametoa taarifa kuwa bado yuko hai, wapelelezwe haraka kipindi hiki wakiwa bado wanamfanyia makeup ya manundu na kumpaka tomato Mdude huko walipomficha
 
Duh hawa nao kumbe wapo makubwaaaaaa haya tuone maelekezo yao kama yana nguvu ama ndio wale wale mbuzi wa bwana heri shamba la bwana heri.
 
Chadema wametoa taarifa Mdude katekwa na waowao ndo wametoa taarifa kuwa bado yuko hai, wapelelezwe haraka kipindi hiki wakiwa bado wanamfanyia makeup ya manundu na kumpaka tomato Mdude huko walipomficha
Mkuu lucha kwa Nia njema kabisa najua pengine umeshakula umeshiba na ni pleasure Kwako kuandika chochote kinacho kuijia kichwani.

Tambua mdude angekua ni mtu wa familia yako ama mlikua na blood relationship nae na akavamiwa na watu wanao sadikika ni police wakamtoa DAMU Kama clip inayo/ iliyo sambaa na mpaka Sasa haijulikani alipo unadhani ungejisikiaje?

Ni bora ndugu yako awe jela ama mahabusu na apatiwe na mahakama stahiki yake kuliko kutekwa na kuuwawa kikatili ama kupotezwa/ kukatishwa uhai kama ambavyo MDUDE kafanyiwa ni Bora hata mwili wake upatikane ukapumzishwe na wapendwa wake.

Uhai wa mtu sio Kama kushabikia Simba na yanga au uhai kuuletea siasa zetu za uccm na uchadema hapa tunazungumzia uhai wa binadamu ie.mdude.

Binafsi kila nikivaa uhusika na viatu vya familia, ndugu, mke ,jamaa na marafiki wa MDUDE natokwa na MACHOZI
 
Mkuu lucha kwa Nia njema kabisa najua pengine umeshakula umeshiba na ni pleasure Kwako kuandika chochote kinacho kuijia kichwani.

Tambua mdude angekua ni mtu wa familia yako ama mlikua na blood relationship nae na akavamiwa na watu wanao sadikika ni police wakamtoa DAMU Kama clip inayo/ iliyo sambaa na mpaka Sasa haijulikani alipo unadhani ungejisikiaje?

Ni bora ndugu yako awe jela ama mahabusu na apatiwe na mahakama stahiki yake kuliko kutekwa na kuuwawa kikatili ama kupotezwa/ kukatishwa uhai kama ambavyo MDUDE kafanyiwa ni Bora hata mwili wake upatikane ukapumzishwe na wapendwa wake.

Uhai wa mtu sio Kama kushabikia Simba na yanga au uhai kuuletea siasa zetu za uccm na uchadema hapa tunazungumzia uhai wa binadamu ie.mdude.

Binafsi kila nikivaa uhusika na viatu vya familia, ndugu, mke ,jamaa na marafiki wa MDUDE natokwa na MACHOZI
Imefikia hatua siyo kila unaloambiwa ulibebe muda mwingine ujiongeze wewe mtu kavuja damu kiasi kile alafu kuna watu wameleta taarifa kuwa bado yupo hai wamejuaje kuwa bado yupo hai? Na watu haohao ndo walileta taarifa za kutekwa, kuna dalili za drama kwenye haya matukio ili watu wanunue huruma kwa raia.
 
Katika kipindi cha takriban mwezi mmoja na nusu, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imekuwa ikifuatilia kwa karibu matukio mbali mbali ambayo yamekuwa yakijitokeza nchini. THBUB baada ya kufanya tathmini kuhusu matukio hayo kwa mujibu wa Katiba na Sheria ya THBUB, imejiridhisha kuwa matukio hayo yanaashiria uvunjifu wa haki za binadamu, ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na uvunjifu wa amani na utulivu nchini.

Aidha, katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, kumekuwa na matukio mbali mbali yakiwemo matumizi ya lugha chafu zisizozingatia utu na heshima ya mtu na zinazoleta hamasa na kuchochea uvunjifu wa amani na utulivu, matukio yanayoashiria matumizi ya nguvu kupita kiasi wakati wa kushughulikia mikusanyiko ya kisiasa, kushambuliwa na kujeruhiwa kwa baadhi ya wananchi ikiwemo tukio lililotokea tarehe 30 Aprili, 2025 la kushambuliwa na kujeruhiwa Kiongozi wa Kidini Padre Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania na tukio la kutekwa kwa Faluka Saidi Nyagali kwa jina maarufu Mdude na matukio mengine.

THBUB inatambua kuwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi, sheria za nchi na mikataba mbalimbali ya kimataifa ya haki za binadamu ambayo Tanzania imeridhia, wananchi wote wa Tanzania wana haki ya kufurahia na kupata haki zao za binadamu. Aidha, kwa mujibu wa Katiba ya Nchi, kila mwananchi anayo haki ya kuishi, kuwa huru, kutoa maoni na kushiriki katika shughuli za umma moja kwa moja au kupitia wawakilishi kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa katika Katiba na sheria za nchi.

Pamoja na haki hizo, Katiba inaweka sharti la wajibu kwa kila mwananchi kutotumia misingi ambayo itasababisha kuingiliwa au kukatizwa kwa uhuru na haki ya watu wengine na kwamba pale mtu anapoamini kwamba haki yake imevunjwa anaweza kuwasilisha suala hilo Mahakamani au katika vyombo vyengine vyenye mamlaka kwa mujibu wa sheria.

Vile vile THBUB inatambua kuwa kwa mujibu wa sheria, Jeshi la Polisi limepewa dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao na hivyo kwa kuzingatia sheria na maadili, Jeshi hilo lina mamlaka ya kushughulikia viashiria vyote ambavyo vinaweza kuhatarisha amani na utulivu nchini.

THBUB inaona kuwa matendo yaliyojitokeza hayatoi taswira nzuri katika ustawi wa haki za binadamu, utawala bora na amani na utulivu nchini ambayo ni muhimu sana katika kipindi hichi kuelekea uchaguzi Mkuu. THBUB inalaani matukio hayo ambayo yamevunja haki za binadamu na kukiuka misingi ya utawala bora na yanayoashiria uvunjifu wa amani na utulivu.

Kutokana na matukio yaliyotokea THBUB inapendekeza yafuatayo:

a) Jeshi la Polisi ambalo ndiyo taasisi iliyopewa dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao kutekeleza wajibu wake kwa kufuata Katiba, Sheria na Kanuni;

b) Jeshi la Polisi liendelee kuwasaka na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika na kujeruhiwa kwa Dkt Charles Kitima, waliomteka Faluka Saidi Nyagali (Mdude) na waliohusika katika matukio mengine ya uvunjwaji wa haki za binadamu;

c) Msajili wa Vyama vya Siasa kuwataka viongozi wa vyama vya siasa kuzingatia matakwa ya Katiba na Sheria katika shughuli zao;

d) Serikali iendelee kukaa na wadau wa Demokrasia katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbali mbali zinazojitokeza;

e) Viongozi na wananchi waendelee kudumisha amani na utulivu ambao ndio msingi wa kufurahiya haki za binadamu; na

f) Wadau wote wa uchaguzi kuwa na ustahimilivu wakati wa mchakato wa uchaguzi kwa kuwa ushindani wa kisiasa nyakati za uchaguzi ndio chachu ya demokrasia.

Jukumu la Ulinzi na Utetezi wa Haki za Binadamu na uzingatiwaji wa misingi wa Utawala Bora ni letu sote.

Pia, Soma
Haki na Amani vinaenda pamoja,hoja ya mwanasheria Mkuu Bungeni na Waziri wa mambo ya ndani kuendeleza na nyazifa zao,Kwa kusema kesi ya Tundu Lissu na Bado Wapo madarakani!Ni Haki,wakati jambo lipo mahakamani?!
 
Chadema wametoa taarifa Mdude katekwa na waowao ndo wametoa taarifa kuwa bado yuko hai, wapelelezwe haraka kipindi hiki wakiwa bado wanamfanyia makeup ya manundu na kumpaka tomato Mdude huko walipomficha
We acha kushabikia ujinga, angekuwa ni baba Yako yamemkuta haya,ungeficha Upumbavu wako!Ni haki Yako pia kuonyesha ulivyo mtupu kichwani!
 
Imefikia hatua siyo kila unaloambiwa ulibebe muda mwingine ujiongeze wewe mtu kavuja damu kiasi kile alafu kuna watu wameleta taarifa kuwa bado yupo hai wamejuaje kuwa bado yupo hai? Na watu haohao ndo walileta taarifa za kutekwa, kuna dalili za drama kwenye haya matukio ili watu wanunue huruma kwa raia.
Sawa,
Ngoja tusubili maana TIME IS THE BEST TEACHER. Ngoja tuwe na subra kwenye hili.
 
Mkuu lucha kwa Nia njema kabisa najua pengine umeshakula umeshiba na ni pleasure Kwako kuandika chochote kinacho kuijia kichwani.

Tambua mdude angekua ni mtu wa familia yako ama mlikua na blood relationship nae na akavamiwa na watu wanao sadikika ni police wakamtoa DAMU Kama clip inayo/ iliyo sambaa na mpaka Sasa haijulikani alipo unadhani ungejisikiaje?

Ni bora ndugu yako awe jela ama mahabusu na apatiwe na mahakama stahiki yake kuliko kutekwa na kuuwawa kikatili ama kupotezwa/ kukatishwa uhai kama ambavyo MDUDE kafanyiwa ni Bora hata mwili wake upatikane ukapumzishwe na wapendwa wake.

Uhai wa mtu sio Kama kushabikia Simba na yanga au uhai kuuletea siasa zetu za uccm na uchadema hapa tunazungumzia uhai wa binadamu ie.mdude.

Binafsi kila nikivaa uhusika na viatu vya familia, ndugu, mke ,jamaa na marafiki wa MDUDE natokwa na MACHOZI
Mkuu watu wengine nadhani utu kwao Si lolote,ila mara nyingi watu Hawa,hujifunza Kwa matukio yanayowasibu wao wenyewe!
 
Katika kipindi cha takriban mwezi mmoja na nusu, Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imekuwa ikifuatilia kwa karibu matukio mbali mbali ambayo yamekuwa yakijitokeza nchini. THBUB baada ya kufanya tathmini kuhusu matukio hayo kwa mujibu wa Katiba na Sheria ya THBUB, imejiridhisha kuwa matukio hayo yanaashiria uvunjifu wa haki za binadamu, ukiukwaji wa misingi ya utawala bora na uvunjifu wa amani na utulivu nchini.

Aidha, katika kipindi hiki kuelekea uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani, kumekuwa na matukio mbali mbali yakiwemo matumizi ya lugha chafu zisizozingatia utu na heshima ya mtu na zinazoleta hamasa na kuchochea uvunjifu wa amani na utulivu, matukio yanayoashiria matumizi ya nguvu kupita kiasi wakati wa kushughulikia mikusanyiko ya kisiasa, kushambuliwa na kujeruhiwa kwa baadhi ya wananchi ikiwemo tukio lililotokea tarehe 30 Aprili, 2025 la kushambuliwa na kujeruhiwa Kiongozi wa Kidini Padre Dkt. Charles Kitima, Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Tanzania na tukio la kutekwa kwa Faluka Saidi Nyagali kwa jina maarufu Mdude na matukio mengine.

THBUB inatambua kuwa kwa mujibu wa Katiba ya nchi, sheria za nchi na mikataba mbalimbali ya kimataifa ya haki za binadamu ambayo Tanzania imeridhia, wananchi wote wa Tanzania wana haki ya kufurahia na kupata haki zao za binadamu. Aidha, kwa mujibu wa Katiba ya Nchi, kila mwananchi anayo haki ya kuishi, kuwa huru, kutoa maoni na kushiriki katika shughuli za umma moja kwa moja au kupitia wawakilishi kwa kuzingatia masharti yaliyowekwa katika Katiba na sheria za nchi.

Pamoja na haki hizo, Katiba inaweka sharti la wajibu kwa kila mwananchi kutotumia misingi ambayo itasababisha kuingiliwa au kukatizwa kwa uhuru na haki ya watu wengine na kwamba pale mtu anapoamini kwamba haki yake imevunjwa anaweza kuwasilisha suala hilo Mahakamani au katika vyombo vyengine vyenye mamlaka kwa mujibu wa sheria.

Vile vile THBUB inatambua kuwa kwa mujibu wa sheria, Jeshi la Polisi limepewa dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao na hivyo kwa kuzingatia sheria na maadili, Jeshi hilo lina mamlaka ya kushughulikia viashiria vyote ambavyo vinaweza kuhatarisha amani na utulivu nchini.

THBUB inaona kuwa matendo yaliyojitokeza hayatoi taswira nzuri katika ustawi wa haki za binadamu, utawala bora na amani na utulivu nchini ambayo ni muhimu sana katika kipindi hichi kuelekea uchaguzi Mkuu. THBUB inalaani matukio hayo ambayo yamevunja haki za binadamu na kukiuka misingi ya utawala bora na yanayoashiria uvunjifu wa amani na utulivu.

Kutokana na matukio yaliyotokea THBUB inapendekeza yafuatayo:

a) Jeshi la Polisi ambalo ndiyo taasisi iliyopewa dhamana ya kulinda usalama wa raia na mali zao kutekeleza wajibu wake kwa kufuata Katiba, Sheria na Kanuni;

b) Jeshi la Polisi liendelee kuwasaka na kuwachukulia hatua za kisheria waliohusika na kujeruhiwa kwa Dkt Charles Kitima, waliomteka Faluka Saidi Nyagali (Mdude) na waliohusika katika matukio mengine ya uvunjwaji wa haki za binadamu;

c) Msajili wa Vyama vya Siasa kuwataka viongozi wa vyama vya siasa kuzingatia matakwa ya Katiba na Sheria katika shughuli zao;

d) Serikali iendelee kukaa na wadau wa Demokrasia katika kuzitafutia ufumbuzi changamoto mbali mbali zinazojitokeza;

e) Viongozi na wananchi waendelee kudumisha amani na utulivu ambao ndio msingi wa kufurahiya haki za binadamu; na

f) Wadau wote wa uchaguzi kuwa na ustahimilivu wakati wa mchakato wa uchaguzi kwa kuwa ushindani wa kisiasa nyakati za uchaguzi ndio chachu ya demokrasia.

Jukumu la Ulinzi na Utetezi wa Haki za Binadamu na uzingatiwaji wa misingi wa Utawala Bora ni letu sote.

Pia, Soma

Tume hii ni Mojawapo ya Taasisi za Umma ambazo ni hopeless katika nchi hii ya Tanzania. Uwepo wake ni muendeleZo wa Ufujaji wa Fedha za Kodi za Wananchi.
THBUB is a Toothless Dog, sioni faida yoyote ile ya kuwepo kwa Taasisi hii.

Tume ya Haki za binadamu ya nchi ya Afrika Kusini iko very powerful, inaaminika na inaheshimika Sana na Wananchi wa nchi hiyo kutokana na Utendaji kazi wake uliotukuka katika nchi hiyo. Hata Watawala wa nchi hiyo wanaiheshimu Time hiyo, Hali ambayo ni kinyume kabisa na uhalisia wa THBUB.
 
Mkuu watu wengine nadhani utu kwao Si lolote,ila mara nyingi watu Hawa,hujifunza Kwa matukio yanayowasibu wao wenyewe!
Ni kweli mkuu yakimkuta ya kumkuta ndipo anakuja kujua aaahaa kumbe mwenzako akinyolewa zako tia maji.

Haya matukuo yanauma Sana yaani Kama Kuna ulozi au MGANGA wale wa makafara ni Bora lifanyike ili haki ya damu ya mdude ISIENDE BUREEE.
 
Ni kweli mkuu yakimkuta ya kumkuta ndipo anakuja kujua aaahaa kumbe mwenzako akinyolewa zako tia maji.

Haya matukuo yanauma Sana yaani Kama Kuna ulozi au MGANGA wale wa makafara ni Bora lifanyike ili haki ya damu ya mdude ISIENDE BUREEE.
Inaumiza sana, nadhani watawala hawajakubali Kwa dhati mfumo wa vyama vingi!Yaani wenye nafasi tayari hawataki kutoka, Labda kifo tuu kiwakute!
 
Siku nyingine reply kwenye comment za watoto wenzako
Acha upumbavu kama upumbavu, Maisha ya binadamu si ya kuyafanyia mzaha hata kidogo,acha dharau,acha kujiona Bora kuliko wenzako,jishushe utainuliwe!
 
Back
Top Bottom