Tamko la Maaskofu na Wachungaji wa Kipentekoste juu ya kuugua ghafla kwa Askofu Gwajima

TAMKO LA MAASKOFU NA WACHUNGAJI
KUTOKA MADHEHEBU MBALIMBALI JUU
YA TUKIO LA ASKOFU GWAJIMA.
Sisi maaskofu na wachungaji kutoka
makanisa mbalimbali tumeshtushwa na
kusikitishwa kwa taarifa ya ugonjwa wa
Askofu na mtumishi mwenzetu Josephat
Gwajima ambaye tarehe 27/03/2015
alifika kituo cha polisi cha kati kuitikia
wito wa polisi uliomtaka kwenda kujibu
shutuma za kutumia lugha ya matusi kwa
kardinali Pengo.
Tumepata fursa ya kutafakari na kujadili
kwa kina hali iliyompata Askofu
mwenzetu hasa baada ya kuzingatia kuea
Askofu Gwajima alifika polisi akiwa
mzima na mwenye afya njema lakini
wakati wa akihojiwa na polisi, hali yake
ilibadilika ghafla kiasi cha kupelekea yeye
kulazwa hospitali ya TMJ akiugua tena
kwenye wodi ya wagonjwa mahututi
yaani (ICU) katika chumba cha uangalizi
maalum.
Maswali yetu makuu ni kitu gani
kimempata mwenzetu? Tunajiuliza, je
vyombo vya usalama vimekua sio sehemu
salama kama zamani?
Tukiwa bado tunatafakari hill,
tumeshtushwa tena baada ya kupata
taarifa ya kuwa Wachungaji Wasaidizi wa
Askofu Gwajima pamoja na walinzi wake
waliokuwepo hospitalini hapo kwa ajili ya
kumuuguza nao pia wamekamatwa kwa
tuhuma za. kutaka kumtorosha Askofu
Gwajima.
Jambo hili linashangaza zaidi maana
wachungaji wale wale waliokuwa naye
akiwa mzima wa afya wakati anaelekea
polisi ndio wale wale wanatuhumiwa
kutaka kumtorosha akiwa mgonjwa.
Ni jambo la kushangaza na lisiloingia
akilini kuwa wasaidizi hao wa Gwajima
walitaka kumtorosha wakati Gwajima
kama angekua na nia hiyo angekwisha
fanya hivyo mana alikuwa na uwezo wa
kutoroka alipokua Arusha kwenye kikao
cha Maaskofu wakuu wa makanisa ya
Kipentekoste ambao alipata taarifa za
kuitwa Polisi.
Isitoshe Gwajima aliitija wito na kwenda
polisi mwenyewe kwa miguu yake bila
kushurutishwa, wala hakufikishwa polisi
kwa nguvu.
Swali: Kama alikua anaona ugumu wa
kutoroka wakati hakuna polisi
anayemlinda na huku akiwa mwenye afya
tele, itakuaje rahisi kutoroshwa leo akiwa
mahututi na akiwa kwenye ulinzi mkali
wa polisi?
Mbona hii inastaajabisha?
Jambo jingine linalotupa shida ni kuhusu
mlalamikaji wa kesi hii inayomkabili
Askofu Gwajima. Tumeelezwa na
wasaidizi wa Askofu Gwajima kuwa pale
polisi walielezwa kuwa aliyefungua kesi
hii sio Pengo ila mtu mmoja aitwaye
Aboubakar.
Kwa ufahamu wetu juu ya sheria
unatutuma kuamini kuwa Aboubakar sio
MTU sahihi wa kufungua kesi hiyo sababu
hawezi kutuonyesha ameumizwa kiasi
gani na matamshi ya Askofu Gwajima.
Isitoshe, Kardinali Pengo mwenyewe
ametamka katika Ibada yake ya Jumapili
hii ya tarehe 29/03/2015 kuwa
amemsamehe Gwajima, yupi tena mwenye
uchungu wa kumzidi Kardinali Pengo?
RAI YETU:
Rai yetu ni kwamba, ni vizuri serikali
pamoja na vyombo vyake vya usalama
vikatumia weledi katika kushughulikia
mambo ya kidini na viongozi wake kwani
yanaweza kusababisha chuki dhidi ya
serikali na pia kupelekea mpasuko
mkubwa wa kidini katika jamii yetu iliyo
na historia nzuri ya umoja na
mshikamano na ushirikiano katika
matukio yote ya kimaisha.
Tunaomba serikali isaidie kuondoa
mkanganyiko huu na busara kubwa
itumike ili kuepusha uvunjifu wa Amani
katika jamii.
MAAMUZI YETU:
Jambo hili linazungumzika, maana hata
hivyo tumeshaazimia kukutana na IGP ili
kupata suluhisho juu ya jambo hili.
Kwa niaba ya maaskofu na wachungaji:
Mwenyekiti: Askofu Dr. Mgullu Kilimba
Katibu: Askofu Dr. Dramas Mukassa


Askofu wa makanisa gani hao in red

 
Siamini katika fujo. Nakubali kwamba Gwajima ametumia lugha kali mno kufikisha ujumbe kwa Pengo, hapo anaweza akaomba radhi kwa lugha iliyotumika. Ila kuhusu ujumbe aliotoa Gwajima itabidi ubaki pale pale. Watu kama Gwajima kuna muda wanahitajika ili kuwasemea wale ambao wanabaki kulalamika chinichini tu.
 
Pamoja na mambo mengine kuna sababu ya kupitia upya huu uhuru wa kuabudu uliopitiliza....Gwajima aje mbele ya jamii aombe radhi kwa kutoa matamshi yasiyokuwa ya kiungwana ilihali akijua yeye ni mtumishi na kwamba ana wafuasi wengi na kwamba aliyetolewa matamshi hayo ni kiongozi pia ambaye angeweza kuwasiliana naye kwa njia ya kistaarabu!

Amekana kwamba HAJATUKANA bali ametoa ONYO KALI......vipi tena aje kuomba radhi??
 
Siamini katika fujo. Nakubali kwamba Gwajima ametumia lugha kali mno kufikisha ujumbe kwa Pengo, hapo anaweza akaomba radhi kwa lugha iliyotumika. Ila kuhusu ujumbe aliotoa Gwajima itabidi ubaki pale pale. Watu kama Gwajima kuna muda wanahitajika ili kuwasemea wale ambao wanabaki kulalamika chinichini tu.

nakubaliana nawe juu ya umuhimu wa ujumbe. But pia kuna wakati Yesu aliwaita mbweha viongozi wa siasa wa wakati wake, mh. kadinari Pengo alikemewa na ameridhika kwa kusamehe. Mungu hutumia watu kwa tabia zao.
 
Ni vema wakajua yaliyojiri huko kwenye majadiliano. Isije ikawa alifunguliwa ukarasa wa mambo yake ndiyo akajiona ya kwamba kumbe watu wanajua kila jambo lake ndo akapata pressure akaanza kuumwa. Inawezekana aliona sasa hapa ameshajulikana kila kitu na haenda hakuamini ya kwamba watu wana data zake. Aulizwe vizuri Gwajima mwenyewe tusimsemee, na kwa vile sasa anaongea aseme ukweli akiwa kama mtumishi wa mungu
 
nakubaliana nawe juu ya umuhimu wa ujumbe. But pia kuna wakati Yesu aliwaita mbweha viongozi wa siasa wa wakati wake, mh. kadinari Pengo alikemewa na ameridhika kwa kusamehe. Mungu hutumia watu kwa tabia zao.
Hah hah, pia YESU alishawahi kumwambia Petro, 'nyamaza shetani' pale alipokuwa anapinga kusubiwa. Nimekuelewa ndugu
 
Hisia kitu kibaya sn,gwajima kutukana kote Kule zilikua ni hisia,ila alishindwa namna ya kuziwasilisha kwa muhusika.lakini wanajuana hao.
 
Kwa Ninivyowajua ccm na serikali yao, huyu gwajima ni marehemu. Washainyofoa roho yake, hapo alipo ni msukule ni swala la mda tu hiyo roho itatengana na mwili
 
TAMKO LA MAASKOFU NA WACHUNGAJI KUTOKA MADHEHEBU MBALIMBALI JUU YA TUKIO LA KUUGUA GHAFLA ASKOFU GWAJIMA.


unnamed%252520%2525281%252529.jpg


Sisi maaskofu na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali tumeshtushwa na kusikitishwa kwa taarifa ya ugonjwa wa Askofu na mtumishi mwenzetu Josephat Gwajima ambaye tarehe 27/03/2015 alifika kituo cha polisi cha kati kuitikia wito wa polisi uliomtaka kwenda kujibu shutuma za kutumia lugha ya matusi kwa kardinali Pengo.

Tumepata fursa ya kutafakari na kujadili kwa kina hali iliyompata Askofu mwenzetu hasa baada ya kuzingatia kuea Askofu Gwajima alifika polisi akiwa mzima na mwenye afya njema lakini wakati wa akihojiwa na polisi, hali yake ilibadilika ghafla kiasi cha kupelekea yeye kulazwa hospitali ya TMJ akiugua tena kwenye wodi ya wagonjwa mahututi yaani (ICU) katika chumba cha uangalizi maalum.

Maswali yetu makuu ni kitu gani kimempata mwenzetu? Tunajiuliza, je vyombo vya usalama vimekua sio sehemu salama kama zamani?

Tukiwa bado tunatafakari hill, tumeshtushwa tena baada ya kupata taarifa ya kuwa Wachungaji Wasaidizi wa Askofu Gwajima pamoja na walinzi wake waliokuwepo hospitalini hapo kwa ajili ya kumuuguza nao pia wamekamatwa kwa tuhuma za. kutaka kumtorosha Askofu Gwajima.

Jambo hili linashangaza zaidi maana wachungaji wale wale waliokuwa naye akiwa mzima wa afya wakati anaelekea polisi ndio wale wale wanatuhumiwa kutaka kumtorosha akiwa mgonjwa.

Ni jambo la kushangaza na lisiloingia akilini kuwa wasaidizi hao wa Gwajima walitaka kumtorosha wakati Gwajima kama angekua na nia hiyo angekwisha fanya hivyo mana alikuwa na uwezo wa kutoroka alipokua Arusha kwenye kikao cha Maaskofu wakuu wa makanisa ya Kipentekoste ambao alipata taarifa za kuitwa Polisi.

Isitoshe Gwajima aliitija wito na kwenda polisi mwenyewe kwa miguu yake bila kushurutishwa, wala hakufikishwa polisi kwa nguvu.

Swali: Kama alikua anaona ugumu wa kutoroka wakati hakuna polisi anayemlinda na huku akiwa mwenye afya tele, itakuaje rahisi kutoroshwa leo akiwa mahututi na akiwa kwenye ulinzi mkali wa polisi?

Mbona hii inastaajabisha?

Jambo jingine linalotupa shida ni kuhusu mlalamikaji wa kesi hii inayomkabili Askofu Gwajima.

Tumeelezwa na wasaidizi wa Askofu Gwajima kuwa pale polisi walielezwa kuwa aliyefungua kesi hii sio Pengo ila mtu mmoja aitwaye Aboubakar.

Kwa ufahamu wetu juu ya sheria unatutuma kuamini kuwa Aboubakar sio MTU sahihi wa kufungua kesi hiyo sababu hawezi kutuonyesha ameumizwa kiasi gani na matamshi ya Askofu Gwajima.

Isitoshe, Kardinali Pengo mwenyewe ametamka katika Ibada yake ya Jumapili hii ya tarehe 29/03/2015 kuwa amemsamehe Gwajima, yupi tena mwenye uchungu wa kumzidi Kardinali Pengo?

RAI YETU:
Rai yetu ni kwamba, ni vizuri serikali pamoja na vyombo vyake vya usalama vikatumia weledi katika kushughulikia mambo ya kidini na viongozi wake kwani yanaweza kusababisha chuki dhidi ya serikali na pia kupelekea mpasuko mkubwa wa kidini katika jamii yetu iliyo na historia nzuri ya umoja na mshikamano na ushirikiano katika matukio yote ya kimaisha.

Tunaomba serikali isaidie kuondoa mkanganyiko huu na busara kubwa itumike ili kuepusha uvunjifu wa Amani katika jamii.

MAAMUZI YETU:

Jambo hili linazungumzika, maana hata hivyo tumeshaazimia kukutana na IGP ili kupata suluhisho juu ya jambo hili.

Kwa niaba ya maaskofu na wachungaji:
Mwenyekiti: Askofu Dr. Mgullu Kilimba
Katibu: Askofu Dr. Dramas Mukassa

Na mwandishi
F.A.K
30/03/2015

 
Si wangeenda tu kumuona IGP mpaka watoe tamko? Tujaribu kuwa wenye hekima, busara na maarifa Wakati wote na kuepuka kutumia vyombo vya habari pasipo sababu za kufanya hivyo. Ni rai yangu kwa viongozi wote wawe dini au siasa au jamii.
 
Wamshauri kwanza Gwajima aombe radhi kwa Kardinali Pengo na wakristo kwa ujumla. Kwa kufanya hivyo atakuwa ameonesha uungwana. Huwezi kuwa askofu ukanena alivyonena kuhusu kiongozi Mwenzio!
 
Back
Top Bottom