Mwan mpambanaji
JF-Expert Member
- Apr 3, 2008
- 482
- 131
BARAZA LA VIJANA CHADEMA MKOA WA ARUSHA(BAVICHA)
P.0.BOX 12525
ARUSHA
TEL.0754 834152
Email.arushabavicha@gmail.com
Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
TAMKO LA BAVICHA MKOA WA ARUSHA.KUIPONGEZA KAMATI KUU YA CHADEMA PAMOJA NA KUUNGA MKONO SIKU 21 ZA SERIKALI KUTATUA SWALA LA UMEYA WA ARUSHA
Ndugu wanahabari
Mtakumbuka kuwa kamati kuu ya Chadema iliketi tarehe 19.3.2011,pamoja na maazimio mengine,ilitoa siku 21 kwa serikali kutumia busara kutatua swala la umeya wa Arusha,ambao sote ni mashahidi ya jinsi ulivyokiuka sheria.Bavicha mkoa wa Arusha tunaipongeza kamati kuu,kwa jinsi ambavyo wamekuwa na busara na jitihada zote za viongozi wetu kuzuia umma wa Arusha.Ni busara za viongozi wetu ambazo zimefanya hadi sasa umma wa Arusha umekuwa na subira,tukiamini kuwa kama serikali itatumia busara basi swala la umeya litatatuliwa kidiplomasia,siku 21 zinatosha kabisa kwa serikali kama ina nia ya kweli na dhamira zao zinawatuma hivyo
Bavicha mkoa wa Arusha,tunapenda kuihakikishia kamati kuu na umma wa Tanzania kwa ujumla kuwa,tupo imara,na tupo tayari kupambana hadi ushindi upatikane,vijana na umma wa Arusha hatutakubali wala kuendelea kuvumilia ukiukwaji huu wa sheria katika uchaguzi wa meya,na kamwe hatumtambui wala hatutamtambua meya ambaye si chaguo la wanaarushaNi lazima uchaguzi urudiwe ili haki itendeke,maana msingi wa maendeleo ni HAKI,na bila haki hamna maendeleo wala Amani.Tunasisitiza kuwa baada ya siku 21 tutaingia mitaani kushinikiza uchaguzi wa meya,vijana tupo tayari kwa mapambano,hatutaogopa wala kutishwa na awaye yote,tutapambana hadi kieleweke.
Ikiwa hakuna jambo lolote muhimu ambalo mtu yupo tayari kufa kwalo,basi mtu huyo hastahili kuishi,Martin Luther King Jr
NANYARO E.J.
MWENYEKITI BAVICHA (M)
..
P.0.BOX 12525
ARUSHA
TEL.0754 834152
Email.arushabavicha@gmail.com
Tovuti ya Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA)
TAMKO LA BAVICHA MKOA WA ARUSHA.KUIPONGEZA KAMATI KUU YA CHADEMA PAMOJA NA KUUNGA MKONO SIKU 21 ZA SERIKALI KUTATUA SWALA LA UMEYA WA ARUSHA
Ndugu wanahabari
Mtakumbuka kuwa kamati kuu ya Chadema iliketi tarehe 19.3.2011,pamoja na maazimio mengine,ilitoa siku 21 kwa serikali kutumia busara kutatua swala la umeya wa Arusha,ambao sote ni mashahidi ya jinsi ulivyokiuka sheria.Bavicha mkoa wa Arusha tunaipongeza kamati kuu,kwa jinsi ambavyo wamekuwa na busara na jitihada zote za viongozi wetu kuzuia umma wa Arusha.Ni busara za viongozi wetu ambazo zimefanya hadi sasa umma wa Arusha umekuwa na subira,tukiamini kuwa kama serikali itatumia busara basi swala la umeya litatatuliwa kidiplomasia,siku 21 zinatosha kabisa kwa serikali kama ina nia ya kweli na dhamira zao zinawatuma hivyo
Bavicha mkoa wa Arusha,tunapenda kuihakikishia kamati kuu na umma wa Tanzania kwa ujumla kuwa,tupo imara,na tupo tayari kupambana hadi ushindi upatikane,vijana na umma wa Arusha hatutakubali wala kuendelea kuvumilia ukiukwaji huu wa sheria katika uchaguzi wa meya,na kamwe hatumtambui wala hatutamtambua meya ambaye si chaguo la wanaarushaNi lazima uchaguzi urudiwe ili haki itendeke,maana msingi wa maendeleo ni HAKI,na bila haki hamna maendeleo wala Amani.Tunasisitiza kuwa baada ya siku 21 tutaingia mitaani kushinikiza uchaguzi wa meya,vijana tupo tayari kwa mapambano,hatutaogopa wala kutishwa na awaye yote,tutapambana hadi kieleweke.
Ikiwa hakuna jambo lolote muhimu ambalo mtu yupo tayari kufa kwalo,basi mtu huyo hastahili kuishi,Martin Luther King Jr
NANYARO E.J.
MWENYEKITI BAVICHA (M)
..