Kuhusu suala hili tunaomba Mbunge yoyote anayesoma hapa tunaomba jamani mtusaidie, yaani kazi ya serikali imekuwa kama kazi ya kwa Mhindi kweli, tunaomba kina Zitto , Bashe, kina Nape tunaomba tusaidieni sisi wafanyakazi tunaonewa ! tunaomba suala hili mtutetee bungeni. ukiangalira mfano hata sasa watu wanaotakiwa kupanda mwaka huu kimya, hatujui nini kinaendelea !
kitu kinachotushangaza ni kwamba ; watu wote walioteuliwa wamepewa mishahara mipya
1. mawaziri walioteuliwa akiwemo Kairuki mbona wamebadilishiwa mishahara
2. wakuu wa mikoa na wailaya walioteuliwa mbona wamebadilishiwa mishahara
3. ma RAS na maDAS wapya mbona wambebadilishiwa mishahara
ma
4. makatibu wakuu wa wizara mbona wamebadilishiwa mishahara n.k
kwanini watu waliotajwa hapo juu wasisubiri UHAKIKI ?
Kwanini ni watu wa chini tu ndo tunasubiri uhakiki wakati nyinyi wakubwa mnabadilishiana mishahara bila kusubiri uhakiki ?