'Ziara' zangu
ofisi za Serikali zinaelekea kubaya.Leo nilikuwa TAKUKURU ambapo mteja
wangu mmoja anahojiwa akidaiwa kula rushwa ya shilingi laki tatu ili
amwamishie mwanafunzi wake shuleni mwake.Nikawakuta maofisa wa TAKUKURU
wametingwa na shughuli zao.Uchokonozi wangu ukaiponza.Nikamtwanga swali
Afisa mmoja juu ya kuhojiwa na kupepelezwa kwa akina-MKULLO na TAKUKURU.
'Hao jamaa(Mkullo na wenzie) hawana tatizo lolote.Ni wasafi hadi
tutakapopokea maelekezo mengine toka kwa wakuu wetu.Hadi sasa hatujaanza
kuwapeleleza Waheshimiwa hao' alisema Afisa huyo. Wameanza taratibu za
kuripoti kwao kila siku? nikamuuliza. 'Waripoti ili iweje? Wakuu
hawajawapa amri hiyo.Mbona maswali yamekuwa mengi Wakili,unataka
kuwatetea nini?' alisema akiniuliza swali la kichefuchefu Afisa huyo.
Nikatamani niingie Ofisi ya Mwalimu wangu(wakati ule pale
UDSM),Dr.Edward Hossea,Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU hata nikapigane
naye.Kiukweli,nikaogopa kesi.Hadi sasa,sijui nichukue hatua gani baada
ya kukasirishwa na TAKUKURU...