MK254
JF-Expert Member
- May 11, 2013
- 33,570
- 53,584
Taiwan inaonekana kuwa nchi ya kwanza kuunga mkono uamuzi wa Israel kuitambua Somaliland.
Ijumaa Israel ilitangaza kuitambua rasmi Somaliland kama taifa huru, na kuwa nchi ya kwanza duniani kufanya hivyo, hatua ambayo imekosolewa vikali na mataifa yanayoiunga mkono serikali ya Mogadishu.
Katika taarifa yake, wizara ya mambo ya nje ya Taiwan imesema Israel, Somaliland na Taiwan ni washirika wenye mtazamo unaofanana katika kuenzi misingi ya demokrasia, uhuru na utawala wa sheria, kwa mujibu wa tovuti ya Focus Taiwan.
Israel ina uhusiano mzuri wa kirafiki na Taiwan pamoja na ushirikiano wa kibiashara, ingawa uhusiano wao wa kidiplomasia si rasmi sana kutokana na Israel kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Jamhuri ya Watu wa China.
Kwa mujibu wa Focus Taiwan, Taiwan na Somaliland zimekuwa zikijenga uhusiano wa pande mbili kwa miaka kadhaa, na mwaka 2020 zilifungua ofisi za uwakilishi katika miji mikuu ya kila upande.
-------------
Taiwan has seemingly become the first country to welcome Israel’s recognition of Somaliland.
Israel on Friday became the first country in the world to recognize the breakaway Somalian region as an independent state, drawing widespread condemnation from countries backing Mogadishu.
In a statement, the foreign ministry in Taipei says Israel, Somaliland and Taiwan are “like-minded democratic partners sharing the values of democracy, freedom, and rule of law,” according to the Focus Taiwan news site
Source: Times Of Israel
Ijumaa Israel ilitangaza kuitambua rasmi Somaliland kama taifa huru, na kuwa nchi ya kwanza duniani kufanya hivyo, hatua ambayo imekosolewa vikali na mataifa yanayoiunga mkono serikali ya Mogadishu.
Katika taarifa yake, wizara ya mambo ya nje ya Taiwan imesema Israel, Somaliland na Taiwan ni washirika wenye mtazamo unaofanana katika kuenzi misingi ya demokrasia, uhuru na utawala wa sheria, kwa mujibu wa tovuti ya Focus Taiwan.
Israel ina uhusiano mzuri wa kirafiki na Taiwan pamoja na ushirikiano wa kibiashara, ingawa uhusiano wao wa kidiplomasia si rasmi sana kutokana na Israel kuwa na uhusiano wa moja kwa moja na Jamhuri ya Watu wa China.
Kwa mujibu wa Focus Taiwan, Taiwan na Somaliland zimekuwa zikijenga uhusiano wa pande mbili kwa miaka kadhaa, na mwaka 2020 zilifungua ofisi za uwakilishi katika miji mikuu ya kila upande.
-------------
Taiwan has seemingly become the first country to welcome Israel’s recognition of Somaliland.
Israel on Friday became the first country in the world to recognize the breakaway Somalian region as an independent state, drawing widespread condemnation from countries backing Mogadishu.
In a statement, the foreign ministry in Taipei says Israel, Somaliland and Taiwan are “like-minded democratic partners sharing the values of democracy, freedom, and rule of law,” according to the Focus Taiwan news site
Source: Times Of Israel