Taifa limepoteza Uhuru

Taifa limepoteza Uhuru

Nanyaro Ephata

JF-Expert Member
Joined
Jan 22, 2011
Posts
1,237
Reaction score
1,828
Taifa lipo njia panda likiweweseka,na hatari kuu za maangamizi.Nchi imekosa dira na mwelekeo wa maendeleo,uchumi wan chi
umelala.Tunaimbishwa wimbo wa ujamaa huku tukichezeshwa ngoma ya Ubebari.Taifa linakabiliwa na umomonyokaji mkubwa wa maadili na utamaduni,nchi inabugia makapi na sumu ya kila aina kwa maangamizi yake yenyewe.Taifa bila utamaduni na maadili yake ni sawa na mti bila mizizi.

Heshima ya mtanzania ndani nan je ya nchi imetoweka,udini umeshika kasi,na hata kutishia kuigawa nchi katika vipande vipande
Watanzania tumepokwa haki na uhuru wetu wa kitaifa,kwa maana ya kujitawala na hatma yetu bila kuingiliwa na watu wasio
wazalendo,tumepoteza uhuru dhidi ya magonjwa,uhuru dhidi ya njaa,uhuru wa kiuchumi.Kupotea kwa uhuru huu ni matokeo ya uchumi na rasilimali za nchi kumilikiwa na kikundi cha watu wachache,huku serikali dhaifu ikisalimu amri kwa genge hili la wahujumu wachache.

Watanzania wamepoteza uhuru binafsi,haki ya kuishi maisha ya heshima,haki ya kupata habari,usawa kwa wote.Eee Mtanzania amka kuwa sehemu ya mabaliko utakayo.

"Kuna nyakati unaweza kuchoka kupinga dhulma na uonevu katika jamii,lakini kamwe isitokee nyakati ukaacha kupinga dhulma na uonevu katika jamii"
 
Dhulma mbaya kama hizi za ugaidi zatakiwa kupingwa na kulaaniwa kwa nguvu zote
 
Fanya kazi muda wa kulalamika umekwisha mkuu

Huyu Nanyaro ana maisha mazuri kuliko wewe jobless,kuwadi wa magamba..huo mfumo unaoutetea hao wachumia tumbo wakimaliza mtoto wako atakuja kukufanyia kitu mbaya kwa kuulea mfumo huo ndani ya umaskini uliokithiri.
 
Hekima ni uhuru tosha wa kukufanya kutokuharakia hicho unachokiita ukombozi.

Ukombozi wa kweli ni ule wa kutokuthamini na kuendekeza mamboleo.

Hapa hakuna haja ya kulaumiana kwani yote hayo uliyaorodhesha ni matokeo

ya mamboleo ambayo mimi na wewe ni mojawapo ya waathilika wakubwa.

Cha msingi ni kuwa wavumilivu na kupeana moyo kwani yote haya yalikwisha tokea kwa nchi nyingi duniani zilizopitia

mifumo mbalimbali ya kiutawala.
 
Hili ndiyo tatizo la watu kushinda kwenye vijiwe vya kahawa.

Malalamiko kibao kwa serikali wakati kila kukicha wako kwenye vijiwe vya kahawa. hizi ni excuse kuficha mapungufu yako.

Fanya kazi kwa bidii. Mbona wengine hatuyaoni hayo. Maisha mdundo.

Endelea na longo longo zako wenzako tunapiga hatua

PANGILIA VIZURI HILO BANDIKO LAKO ILI LISOMEKE VIZURI.
 
wenye macho, na wenye masikio hawana haja ya kuambiwa. this is the beginning of the end.
 
Nchi inaliwa na viwavi,
Serikali imekuwa ya kikundi fulani,
Tuko watu takribani M40+ lakini wenye haki ndani ya nchi hii hawafiki hata M1,matatizo ni mengi ndani ya jamii,wengine wanakula na kusaza wengine hawana uhakika wa kupata japo mlo mmoja,
wengine wanacheka kwa furaha wengine ni vilio na manung'uniko kila uchwao,dah ila tutafika japo kwa mbinde sana.
 
Hekima ni uhuru tosha wa kukufanya kutokuharakia hicho unachokiita ukombozi.

Ukombozi wa kweli ni ule wa kutokuthamini na kuendekeza mamboleo.

Hapa hakuna haja ya kulaumiana kwani yote hayo uliyaorodhesha ni matokeo

ya mamboleo ambayo mimi na wewe ni mojawapo ya waathilika wakubwa.

Cha msingi ni kuwa wavumilivu na kupeana moyo kwani yote haya yalikwisha tokea kwa nchi nyingi duniani zilizopitia

mifumo mbalimbali ya kiutawala.

Uvumilie wewe hadi mguu uote tende
 
Watanzania woga tu ndiyo unatumaliza. Tunayaona yote lakini hatudhubutu hata kufanya kitu. Kwa sasa tukae kitako tume zifanye kazi kwani wanakuuwa na kujichunguza wenyewe hata kuleta majibu wao wenyewe. Hiyo Tanzania ya 2013.
 
Hili ndiyo tatizo la watu kushinda kwenye vijiwe vya kahawa.

Malalamiko kibao kwa serikali wakati kila kukicha wako kwenye vijiwe vya kahawa. hizi ni excuse kuficha mapungufu yako.

Fanya kazi kwa bidii. Mbona wengine hatuyaoni hayo. Maisha mdundo.

Endelea na longo longo zako wenzako tunapiga hatua

PANGILIA VIZURI HILO BANDIKO LAKO ILI LISOMEKE VIZURI.

Unless unafaidika na utawala uliopo sitashangaa ulichokiandika.Hongera sana kwa kufaidika nao,naonea huruma uzao wako.
 
Back
Top Bottom