Taifa letu limejaa watu wanafki na wenye husda

MIXOLOGIST

JF-Expert Member
Mar 1, 2016
12,695
31,475
Habari za asubuhi wana JF

Kwa masikitiko kabisa naomba niwasilishe hii hoja chungu. Taifa letu limejaa watu wanafki na wenye husda. Ni jambo la kawaida kabisa kuona watu wakimshangilia kiongozi au mtu mwenye pesa ambaye anafanya mambo ambayo siyo sahihi. Sehemu kubwa ya watu wetu ni watu waoga wenye tabia za kujipendekeza. Jamii yetu imejaa watu ambao furaha yao inakamilika pale ambapo mtu mwingine anaharibikiwa. Ikiwa mtu amefukuzwa kazi, au amefilisika, au amepatwa na matatizo basi jamii yetu inapata furaha.

Haya mambo ni ya hovyo kabisa kwenye jamii yoyote ile na kamwe taifa haliwezi kuendelea likiwa limesheheni watu wenye husda na unafki. Kwa mamtiki hiyo, itatuchukua miaka mingi sana kupata maendeleo tukiwa tunaendekeza wanafki na watu wenye husda. Watu wa aina hii wanarudisha maendeleo yetu nyuma. Kuna baadhi ya nchi kwenye bara la ulaya haswa karne zilizopita waliamua kuwaua wanafki, wachamwi (watu wenye husda) na washirikina wote. Hivyo basi, ni lazima tuwatambue wanafki na watu wenye husda kama ni maadau wa taifa letu na ndiyo watu wanaoturudisha nyuma kimaendeleo. NAOMBA KUWASILISHA, mapovu yanaruhusiwa.
 
husda maana yake ni nini mkuu.
hizo ni tabia za watu weusi wenye asili ya afrika popote walipo duniani.
Husda ni roho ya chuki imwingiayo mtu anapopata taarifa kuwa mwenzake amepata au amefanikiwa, roho hii inamfanya asiwe na furaha na atatafuta namna ili mwenzake aharibikiwe. Hii ni ile roho ya mtu kutopenda watu wengine wawe na mafanikio, kutaka watu waishi maisha ya shida, wawe wanataabika.
 
Husda ni roho ya chuki imwingiayo mtu anapopata taarifa kuwa mwenzake amepata au amefanikiwa, roho hii inamfanya asiwe na furaha nakutafuta namna ili mwenzake aharibikiwe. ile roho ya mtu kutopenda watu wengine wawe na mafanikio, kutaka watu waishi maisha ya shida, wawe wanataabika.
nashukuru sana mkuu nimeelewa sana.
hii husda naishuhudia sana kwenye jamii yetu.
mfano kuna mama mmoja kafanikiwa kitu ambacho ndugu na jamaa hawakutegemea, leo wote wamemnunia, hawampigii simu, wamekoswa raha kabisa ...
 
Watanzania tumebarikiwa chuki, roho mbaya, wivu, visasi, unafiki.
Haya ni matatizo ambayo lazima mkakati wa kitaifa uundewe ili kuyaondoa, ni mambo ya kishamba na kizamani sana, mataifa yalioyoendelea vitu hivi havipo kwa kiwango cha hapa kwetu
 
nashukuru sana mkuu nimeelewa sana.
hii husda naishuhudia sana kwenye jamii yetu.
mfano kuna mama mmoja kafanikiwa kitu ambacho ndugu na jamaa hawakutegemea, leo wote wamemnunia, hawampigii simu, wamekoswa raha kabisa ...
Taifa hili lina mambo ya kustaajabisha kabisa, wapo watu wanafurahi watanzania wenzao waishi kama mashetani
 
Ni kweli kabisa.

Hatuwezi kuwa na Taifa la watu waadilifu kwa kubaguana.

Rushwa ni rushwa tu hata kama imefanywa na rafiki yako.
Utaogopwa na kuheshimiwa endapo hutamuonea aibu ndugu yako,rafiki yako, mwanachama wa chama chako,mtu wa dini yako na mtu wa kabila lako pale anapokiuka maadili na kwenda kinyume cha taratibu au pale anapotuhumiwa kutenda kosa.

Mfano Kama sheria inasema kuwa Msimamizi wa uchaguzi atamtangaza kuwa mshindi wa uchaguzi mgombea aliyeshinda kwa kura nyingi halafu yeye kwa kupewa rushwa ya madaraka au fedha akabadili matokeo na kumtangaza aliyeshindwa, basi hii ni moja ya dhulma na kujenga jamii iliyojaa dhulma kuanzia ngaza juu mpaka chini.

Kiongozi anayechaguliwa kwa wizi wa kura au kwa mabavu na kukiuka taratibu za wazi na za haki za kupiga na kuhesabu kura ni wazi kuwa huyo ni mtu aliyejawa na roho ya dhulma na ubaguzi.

Tukitaka tuwe na ujasiri na taifa la watu waadilifu ni lazima tuanze na mambo rahisi kabisa kama namna ya kupata viongozi kwa njia halali na kura halali.

Kama unashindwa kumwambia mwanachama mwenzako kuwa pole sana ndugu yangu uchaguzi huu umeshindwa kwa bahati mbaya lakini usikate tamaa jaribu tena awamu ijayo.
Na aliyekushinda naye ni mtanzania kama wewe hivyo hatuna sababu ya kumnyang'anya mtanzania huyo ili tumpe mwingine na kuacha chuki na uhasama miongoni mwa jamii.
Huu ndio ustarabu na uadilifu.

Kwa sasa sijaona mtu wa namna hiyo hivyo ni lazima tuweke katiba mpya itakayowalazimisha waliopewa majukumu kuwa waadilifu.
Tuliitegemea sana serikali ya awamu ya tano kuwa itakua serikali ya watu waadilufu wasiojali vyama ,ukabila ,dini n.k lakini bado kuna kubeba chama kuliko kujenga utaifa.

Siasa zimezidi tena kwa kufanywa kwa mikono ya serikali.
TBC inashindwa kutuonyesha live Shughuli za Bunge lakini kutwa nzima inatuonyesha shughuli za uchaguzi wa chama cha mapinduzi.

Hatuonyeshwa jinsi sheria kandamizi na zile zinazoyagusa maisha yetu zinavyojadiliwa lakini tunaonyeshwa mambo ya siasa ya chama kimoja tu ambazo hazina umuhimu zaidi ya kampeni zisizoisha . Wakati huo huo tunaambiwa siasa mpaka 2020.

Nchi moja iliyopata uhuru miaka 57 iliyopita lakini ina watu wanaobaguana kuliko hata makaburu walivyokuwa wanawabagua waafrika kule S.A.
 
Ni kweli kabisa.

Hatuwezi kuwa na Taifa la watu waadilifu kwa kubaguana.

Rushwa ni rushwa tu hata kama imefanywa na rafiki yako.
Utaogopwa na kuheshimiwa endapo hutamuonea aibu ndugu yako,rafiki yako, mwanachama wa chama chako,mtu wa dini yako na mtu wa kabila lako pale anapokiuka maadili na kwenda kinyume cha taratibu au pale anapotuhumiwa kutenda kosa.

Mfano Kama sheria inasema kuwa Msimamizi wa uchaguzi atamtangaza kuwa mshindi wa uchaguzi mgombea aliyeshinda kwa kura nyingi halafu yeye kwa kupewa rushwa ya madaraka au fedha akabadili matokeo na kumtangaza aliyeshindwa, basi hii ni moja ya dhulma na kujenga jamii iliyojaa dhulma kuanzia ngaza juu mpaka chini.

Kiongozi anayechaguliwa kwa wizi wa kura au kwa mabavu na kukiuka taratibu za wazi na za haki za kupiga na kuhesabu kura ni wazi kuwa huyo ni mtu aliyejawa na roho ya dhulma na ubaguzi.

Tukitaka tuwe na ujasiri na taifa la watu waadilifu ni lazima tuanze na mambo rahisi kabisa kama namna ya kupata viongozi kwa njia halali na kura halali.

Kama unashindwa kumwambia mwanachama mwenzako kuwa pole sana ndugu yangu uchaguzi huu umeshinda.
Na aliyekushinda naye ni mtanzania kama wewe hivyo hatuna sababu ya kumnyang'anya mtanzania huyo ili umpe mwingine na kuacha chuki na uhasama.
Huu ndio ustarabu na uadilifu.
Kwa sasa sijaona mtu wa namna hiyo hivyo ni lazima tuweke katiba mpya itakayowalazimisha waliopewa majukumu kuwa waadilifu.
Tuliitegemea sana serikali ya awamu ya tano kuwa itakua serikali ya watu waadilufu wasiojali vyama ,ukabila ,dini n.k lakini bado kuna kubeba chama kuliko kujenga utaifa.

Siasa zimezidi tena kwa kufanywa kwa mikono ya serikali.
TBC inashindwa kutuonyesha live Shughuli za Bunge lakini kutwa nzima inatuonyesha shughuli za uchaguzi wa chama cha mapinduzi.

Hatuonyeshwa jinsi sheria kandamizi na zile zinazoyagusa maisha yetu zinavyojadiliwa lakini tunaonyeshwa mambo ya siasa ya chama kimoja tu ambazo hazina umuhimu zaidi ya kampeni zisizoisha . Wakati huo huo tunaambiwa siasa mpaka 2020.

Nchi moja iliyopata uhuru miaka 57 iliyopita lakini ina watu wanaobaguana kuliko hata makaburu walivyokuwa wanawabagua waafrika kule S.A.
Haya ni mambo ambayo kama taifa lazima tuyatafakari upya, ni aibu sana katika karne hii mambo kama haya kutokea katika nchi yetu
 
Haya ni mambo ambayo kama taifa lazima tuyatafakari upya, ni aibu sana katika karne hii mambo kama haya kutokea katika nchi yetu



Kila awamu imekua na madhaifu makubwa sana kutokana na kutumia nguvu kubwa kulinda maslahi ya chama kuliko kujenga Taifa moja.

Kuna wakati hua nasema tuna bahati mbaya kwani siasa ndiyo iliyotufikisha hapa.

Kwa mfano awamu ya nne ilikua na nafasi ya kuliacha taifa hili mahali pazuri sana kutokana na jinsi awamu hiyo ilivyojitahidi kujenga misingi ya uwazi ,demokrasia na utawala bora kwa kiwango fulani.Hasa pale ilipoanzisha muafaka wa Zanzibar na kujenga umoja kule Zanzibar. Na pia Ilipoanzisha mchakato wa Katiba.
Hata hivyo lilipoingia suala la itikadi za chama cha mapinduzi kila kitu kiliharibika. Walichotizama viongozi wa chama na serikali ni suala la uwezekano wa kushindwa endapo katiba ya warioba ingepita.
Walifikia mahali pa kuwakashfu hata makada wao waliokuwa wamefanya kazi kubwa ya kukusanya maoni nchi nzima.
Pia suala la kuundwa kwa Bunge maalumu liliwekwa kiitikadi zaidi.

Nje ya wabunge wengi wa CCM lakini pia walijazwa makada wengi wa CCM kwa lengo la kuhakikisha kuwa katiba ya warioba inabadilishwa na kuleta katiba inayoendana na msimamo wa chama cha mapinduzi.

Matokeo yake mpaka leo suala la katiba mpya limebaki kitendawili.
Waliofikiri wanawakosoa wapinzani ndio walioanza kuumizwa na kukosekana kwa katiba ile ya Warioba.
Katiba iliyokuwa imejaa uzalendo wa Kweli na kulinda haki ya kila mtu.

Hata hivyo tulikosa yote kwa sababu ya kulinda madaraka ya watu wanayoyapata kirahisi kupitia chama cha mapinduzi.

Hayo pia yanaendelea kujitikeza. Suala la kulinda chama kwa nguvu zote lipo hata awamu hii ya Tano.
Hofu kubwa kwa watawala ni kulinda neno CCM. Wakotayari kuangamiza kila kitu alimradi hilo neno CCM libaki . Watu wanasahau kuwa chama hicho ni chama kama vilivyo vyama vingine. Cha msingi ni utaifa wetu na umoja wetu na utu wetu.

Unapombagua mtanzania mwenzako kwa sababu ya chama tu hata kufikia mahali pa kumkata kichwa ujue basi nchi itajaa wanafiki wengi.
Unambagua mtu kwa sababu ya chama chake au dini yake au kabila lake ili aende wapi ?
Na kama haumtaki inamaanisha utachagua njia ya kumfukuzilia mbali alimradi unataka kusikia sauti moja tu hata kama ni ya kinafiki.
 
Kuna watu wa dini moja hapa Tanzania sanaongoza kwa tabia izi za kipumbavu. Adi wenyewe wanajisema sisi atupendani, unafiki tu na kunyoosheana vidole.
 
Habari za asubuhi wana JF

Kwa masikitiko kabisa naomba niwasilishe hii hoja chungu. Taifa letu limejaa watu wanafki na wenye husda. Ni jambo la kawaida kabisa kuona watu wakimshangilia kiongozi au mtu mwenye pesa ambaye anafanya mambo ambayo siyo sahihi. Sehemu kubwa ya watu wetu ni watu waoga wenye tabia za kujipendekeza. Jamii yetu imejaa watu ambao furaha yao inakamilika pale ambapo mtu mwingine anaharibikiwa. Ikiwa mtu amefukuzwa kazi, au amefilisika, au amepatwa na matatizo basi jamii yetu inapata furaha.

Haya mambo ni ya hovyo kabisa kwenye jamii yoyote ile na kamwe taifa haliwezi kuendelea likiwa limesheheni watu wenye husda na unafki. Kwa mamtiki hiyo, itatuchukua miaka mingi sana kupata maendeleo tukiwa tunaendekeza wanafki na watu wenye husda. Watu wa aina hii wanarudisha maendeleo yetu nyuma. Kuna baadhi ya nchi kwenye bara la ulaya haswa karne zilizopita waliamua kuwaua wanafki, wachamwi (watu wenye husda) na washirikina wote. Hivyo basi, ni lazima tuwatambue wanafki na watu wenye husda kama ni maadau wa taifa letu na ndiyo watu wanaoturudisha nyuma kimaendeleo. NAOMBA KUWASILISHA, mapovu yanaruhusiwa.
rudia kidogo!
 
Back
Top Bottom