TAHLISO yaigomea CCM kwa UKAWA

TAHLISO yaigomea CCM kwa UKAWA

chitalula

JF-Expert Member
Joined
Nov 3, 2010
Posts
1,302
Reaction score
415
JUMUIYA ya Taasisi ya Elimu ya Juu Tanzania (Tahliso), imegomea mkakati wa kutumiwa na Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kutoa matamko ya kuvishambulia vyama vya upinzani vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA).

Tanzania Daima Jumatano limedokezwa kuwa baada ya mpango huo kukwama, makada wa CCM wamefadhili mgogoro ndani ya jumuiya hiyo ili kumng’o Mwenyekiti wa sasa, Musa Mdede akidaiwa kuendesha uongozi kisiasa.

Hii si mara kwanza Tahliso kugoma kutumiwa na CCM. Mwaka jana, wakati rasimu ya kwanza ya katiba ikijadiliwa kwenye ngazi ya mabaraza, mmoja wa makada wa CCM anayetajwa kutaka kugombea urais 2015, alijaribu kujipenyeza bila mafanikio.

Kada huyo aliingilia mkutano wa baraza la katiba la Tahliso lililokutana mkoni Mbeya, akitaka kuwarubuni viongozi watoe tamko la kupendekeza kuunga mkono umri wa mgombea urais upunguzwe kutoka miaka 40 ya sasa hadi 35.

Hata hivyo, baadhi ya viongozi wa Tahliso walishtukia uchafu huo na kumzuia kada huyo aliyekuwa amealikwa kinyemera kufunga kikao chao asiingie ukumbini.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, kuhusu mkakati huo unaoendeshwa na kundi lingine, Mdede aliwataja viongozi wa CCM wanataka kuwavuruga kwa maslahi ya kundi lao la urais wa 2015.

Amtaja Katibu wa Chipukizi na Uhamasishaji wa Umoja wa Vijana (UVCCM) Taifa, Paul Makonda na Katibu wa CCM mkoa wa Vyuo Vikuu, Chrstopher Ngubiagai.


Mdede alisema baada ya uongozi wake kuingia madarakani Desemba mwaka jana, amekuwa akipokea simu mbali mbali kutoka kwa viongozi waandamizi wa CCM wakimtaka kutoa kauli katika baadhi ya mambo jambo ambalo alilipinga.

“Viongozi waandamizi wa CCM wamekuwa wakinipigia simu kila mara nitoe matamko ya kisiasa. Mimi jibu langu kwao lilikuwa ni moja tu kuwa taasisi yetu si sabuni ya kuwasafishia watu wanaoutaka urais,”

“Niliwaambia kuwa Tahliso si kisemeo cha chama chochote cha siasa bali ni taasisi iliyopo kwa ajili ya maslahi ya wanafunzi wa elimu ya juu,”alisema.

Mdede alifafanua kuwa hata taarifa zilizotolewa hivi karibuni kuwa uongozi wao umeondolewa madarakani si sahihi kwa sababu mkutano uliofanyika Chuo cha Kodi jijini hapa haukumalizika kutokana na fujo zilizojitokeza.

Aliongeza kuwa baada ya kuahirishwa kwa mkutano huo kikundi cha watu kilijikusanya sehemu na kutoa tamko kama wanachuo.

Alisisitiza kuwa CCM imekuwa na utamaduni wa kuitumia Tahliso kukamilisha azma mbali mbali za kisiasa na kwamba baada ya uongozi wake kuingia madarakani jambo hilo alilipiga marufuku hali iliyomtengenezea uaduni na wenzake.

“Katika kuhakikisha tunaondolewa madarakani, vikao kadhaa vilifanyika vikiongozwa na Ngubiagai. Kikao cha kwanza kilifanyika Januari 28 mwaka huu katika hoteli ya (anaitaja) iliyopo Magomeni na kingine kufanyika (anataja),”alisema.

Aliongeza kuwa ushawishi alioambiwa aufanye kwa vijana wanaotarajia kuhitimu hivi karibuni ni kwamba wajiunge na CCM kwa ajili ya kupatiwa ajira.

Chanzo: Tanzania daima

MAONI YANGU:
Walau sasa TAHLISO imepata watu wenye msimamo, hii itawajengea heshima sana kwa wananchi, ni jambo la aibu sana wasomi wetu kutumiwa na wanasiasa uchwara, tukumbuke pia tahliso iliyumba sn kwa kutumiwa na ccm mpaka baadhi ya vyuo vilijitoa na kuanzisha umoja mwingine.

Tunawapongeza sana muendelee na msimamo huohuo
 
Isiwe nguvu ya soda, tunajua vitisho na vikwazo wataendelea kuvipata lakini kumbukeni sometimes IT IS GOOD TO BE BAD kwa maslahi ya HAKI NA KWELI.

Hatuwezi kuwa na jamii ya wasomi wanafundwa kuwa watu wa NDIYO MZEE, hili halikubaliki kwa namna yoyote, lazima kupractise uhuru wa mawazo yenu severely.
 
kumbe si kila msomi anadanganyika, tatizo nchi yetu imejaa wasomi wenye njaa njaa sana kiasi wako tayari kuuza utu wao
 
Huu ndio ujinga mwingine wewe nyie nao kina nani ? Mbona hamnaga la maana tulilowahi kuliona hawa Tahliso wamekosaa kazi huyo aliepinduliwa si aligombea Ubunge sasa mnaposema hamjihusishi na siasa ndo luga gani au ukiwa Ccm ndio Siasa ukiwa Chadema siyo siasa Nyambafu zenu
 
tahilso hongereni mwaka 2007-8 udsm na sua walijitoa ktk umoja huo baada ya kugundulika njama za magamba kupenyeza matakwa yao
 
Huu ndio ujinga mwingine wewe nyie nao kina nani ? Mbona hamnaga la maana tulilowahi kuliona hawa Tahliso wamekosaa kazi huyo aliepinduliwa si aligombea Ubunge sasa mnaposema hamjihusishi na siasa ndo luga gani au ukiwa Ccm ndio Siasa ukiwa Chadema siyo siasa Nyambafu zenu

unaweza kuwa mwanasiasa lakini ukawa hutumiki kisiasa tofauti na intarahamwe...
 
Serikali ya intarahamwe ilitusumbua sana wakati tunaianzisha TAHLISO hadi kupata usajili ilituchukua zaidi ya mwaka mmoja tunazungushwa tu kati ya wizara ya mambo ya ndani na wizara ya sayansi, teknolojia na elimu ya juu.

Sasa ni ajabu kwamba hao hao intarahamwe ndio wamekuwa wakijaribu kuweka makada wao kwenye uongozi wa TAHLISO. Wanaposhindwa kuweka makada wao huamua aidha kuwatumia viongozi waliopo na wakishindwa kuwatumia hutengeneza chokochoko na mapinduzi ili kuondoa hali ya umoja na mshikamano baina ya viongozi kama wanavyofanya sasa.
 
Nadhani hali iliyojionesha dhahiri pale tabora mwishoni mwa wiki iliopita tulipaswa kujifunza kuwa kuna wakati utawalaghai sana watu lkn iko siku itafika ukomo. Makamba na rage walitegemea mteremko baada ya kuona mambo imegeuka akaanza kuongea kama vile mtu aliepoteza fahamu na kuzinduka, huwezi amini. Alisema badala ya kushabikia ser 2 au 3 ooh bora wajikite kwenye masomo na kutoa ushauri juu katiba mpya huku akijisahau kuwa ushauri walikwisha utoa ambao ni maoni yaliyoko kwenye rasimu. Makamba anajikita sana kwenye hizi taasis lkn huku akitumia akili fupi kuliko unavoeza kumwona kwa sura ya nje
 
Back
Top Bottom