Leo imezuka taharuki NSSF makao makuu pale wazee wastaafu walipokusanyika kudai pension yao ya mwezi January ambapo fedha yao kwa utaratibu mpya zinaenda kwenye benki zao walipofungua akaunti zao.Akaunti zilifunguliwa wakati wa uhakiki hivi karibuni.
Wazee wale kila mmoja alikuwa akiongea lake wengine wakiwa nje ya ofisi ghorofa ya 10 wakitaka waruhusiwe kuingia ndani huku wakiambiwa wasubiri.
Walikuwa pale kuanzia majira ya saa 4 hadi saa saba alipojitokeza mfanyakazi mwananamama akiwaambia wote wakusanyike pamoja ghorofa ya 4 awape maelezo kwa pamoja.
Kule waliambiwa ni taratibu tu za kibenki lakini fedha yao itaenda kwamba wao Nssf walishapeleka NBC na CRDB .Utaratibu wa kuhamishia benki zingine ni wa kibenki.
Sasa kwa hili lina ukakasi kwa sababu Nssf walitakiwa watoe taarifa mapema kwa ujumla kwani vyombo vya habari vipo vingi tu. Sasa wastaafu waliopo mikoani nao waje Dar kupata ufafanuzi ?
Jirekebisheni Nssf.Kwa maneno niliyoyasikua leo kwa wazee wale, hakika mnawajengea chuki na serikali yao bila sababu.
Wazee wale kila mmoja alikuwa akiongea lake wengine wakiwa nje ya ofisi ghorofa ya 10 wakitaka waruhusiwe kuingia ndani huku wakiambiwa wasubiri.
Walikuwa pale kuanzia majira ya saa 4 hadi saa saba alipojitokeza mfanyakazi mwananamama akiwaambia wote wakusanyike pamoja ghorofa ya 4 awape maelezo kwa pamoja.
Kule waliambiwa ni taratibu tu za kibenki lakini fedha yao itaenda kwamba wao Nssf walishapeleka NBC na CRDB .Utaratibu wa kuhamishia benki zingine ni wa kibenki.
Sasa kwa hili lina ukakasi kwa sababu Nssf walitakiwa watoe taarifa mapema kwa ujumla kwani vyombo vya habari vipo vingi tu. Sasa wastaafu waliopo mikoani nao waje Dar kupata ufafanuzi ?
Jirekebisheni Nssf.Kwa maneno niliyoyasikua leo kwa wazee wale, hakika mnawajengea chuki na serikali yao bila sababu.

