Tahadhari: Msajili wa vyama vya siasa (Jaji Mutungi) anakaribia kutapeliwa na Prof. Lipumba

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba sasa amekuwa tapeli wa kisiasa. Anatumia njia na mbinu za matapeli wa aina nyingine katika kufanikisha mambo yake. Njia kuu ni kutaka kuaminika na kuungwa mkono na ambao 'wapo naye' lakini wanajifanya 'hawapo naye'. Prof. Lipumba analenga kumtapeli Msajili wa Vyama vya Siasa hapa nchini, Jaji Francis Mutungi.

Prof. Lipumba anajua kuwa yeye na hata upande wake hauna mamlaka ya kumvua Ukatibu Mkuu Maalim Seif. Anajua fika kuwa kuna shauri liko Mahakama Kuu linalohusiana na mgogoro wa CUF. Anajua fika kuwa hata Uenyekiti wake wa CUF una utata kwakuwa naye 'alishafukuzwa' Uenyekiti na uanachama. Hata Magdalena Sakaya naye alishafukuzwa.

Prof. Lipumba anataka kumuaminisha Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuwa CUF imefanya maamuzi na mabadiliko ya uongozi. Anataka kumuaminisha jaji Mutungi kuwa sasa signatories wa ruzuku za CUF ni yeye na Magdalena Sakaya. Huu ni utapeli wa wazi ambao Msajili wa vyama vya siasa anapaswa kuwa nao macho.

Upande wa Prof. Lipumba ulikuwa ukikwama kupata ruzuku kutokana na idhinisho la Katibu Mkuu wa CUF, kama mmoja wa signatories/watia sahihi wa kutoa pesa, kukosekana. Prof. Lipumba anadhani na kuamini kuwa kumpa cheo cha Katibu Mkuu Sakaya ni kupata watia sahihi. Anajidanganya. Maalim anapaswa kujitoa rasmi na Sakaya kuingia. Prof. Lipumba atakwama.

Wote wanaomuunga mkono Prof. Lipumba katika utapeli wake huu, kupitia mgongo wa siasa, hawalitakii mema Taifa hili na demokrasia yake. Kama mpenda demokrasia ya kweli, amani, uhuru na umoja wa Taifa, nitawaanika wote walio nyuma ya Prof. Lipumba katika jambo hili la maigizo na utapeli wa kujifanya anaweza kufanya atakalo CUF.

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Muda wa kuwaanika ni sasa, au unataka kufanya postmortem. Unasubiri ndege aruke ndio ujifanye unaruka kumkamata? Wataje sasa tumalize mbadala.
 
Magufuli alipoapishwa tu,mtu wa kwanza kumtembelea Ikulu alikuwa Lipumba,wakateta,ndani ya wiki moja akafutiwa kesi yake mahakamani ambayo alifunguliwaga mwishoni mwa utawala wa Kikwete.

Lipumba akaenda Azam Tv na kuanza kumpamba TrumpRapa huku akimnanga mkwere. Kuanzia hapo visa na viroja vikatamalaki!!
 
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba sasa amekuwa tapeli wa kisiasa. Anatumia njia na mbinu za matapeli wa aina nyingine katika kufanikisha mambo yake. Njia kuu ni kutaka kuaminika na kuungwa mkono na ambao 'wapo naye' lakini wanajifanya 'hawapo naye'. Prof. Lipumba analenga kumtapeli Msajili wa Vyama vya Siasa hapa nchini, Jaji Francis Mutungi.

Prof. Lipumba anajua kuwa yeye na hata upande wake hauna mamlaka ya kumvua Ukatibu Mkuu Maalim Seif. Anajua fika kuwa kuna shauri liko Mahakama Kuu linalohusiana na mgogoro wa CUF. Anajua fika kuwa hata Uenyekiti wake wa CUF una utata kwakuwa naye 'alishafukuzwa' Uenyekiti na uanachama. Hata Magdalena Sakaya naye alishafukuzwa.

Prof. Lipumba anataka kumuaminisha Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuwa CUF imefanya maamuzi na mabadiliko ya uongozi. Anataka kumuaminisha jaji Mutungi kuwa sasa signatories wa ruzuku za CUF ni yeye na Magdalena Sakaya. Huu ni utapeli wa wazi ambao Msajili wa vyama vya siasa anapaswa kuwa nao macho.

Upande wa Prof. Lipumba ulikuwa ukikwama kupata ruzuku kutokana na idhinisho la Katibu Mkuu wa CUF, kama mmoja wa signatories/watia sahihi wa kutoa pesa, kukosekana. Prof. Lipumba anadhani na kuamini kuwa kumpa cheo cha Katibu Mkuu Sakaya ni kupata watia sahihi. Anajidanganya. Maalim anapaswa kujitoa rasmi na Sakaya kuingia. Prof. Lipumba atakwama.

Wote wanaomuunga mkono Prof. Lipumba katika utapeli wake huu, kupitia mgongo wa siasa, hawalitakii mema Taifa hili na demokrasia yake. Kama mpenda demokrasia ya kweli, amani, uhuru na umoja wa Taifa, nitawaanika wote walio nyuma ya Prof. Lipumba katika jambo hili la maigizo na utapeli wa kujifanya anaweza kufanya atakalo CUF.

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
Hahah tupa tupa bwana et bastola ya nini tena jamani!?
 
Prof. Ibrahim Haruna Lipumba sasa amekuwa tapeli wa kisiasa. Anatumia njia na mbinu za matapeli wa aina nyingine katika kufanikisha mambo yake. Njia kuu ni kutaka kuaminika na kuungwa mkono na ambao 'wapo naye' lakini wanajifanya 'hawapo naye'. Prof. Lipumba analenga kumtapeli Msajili wa Vyama vya Siasa hapa nchini, Jaji Francis Mutungi.

Prof. Lipumba anajua kuwa yeye na hata upande wake hauna mamlaka ya kumvua Ukatibu Mkuu Maalim Seif. Anajua fika kuwa kuna shauri liko Mahakama Kuu linalohusiana na mgogoro wa CUF. Anajua fika kuwa hata Uenyekiti wake wa CUF una utata kwakuwa naye 'alishafukuzwa' Uenyekiti na uanachama. Hata Magdalena Sakaya naye alishafukuzwa.

Prof. Lipumba anataka kumuaminisha Msajili wa Vyama vya Siasa nchini kuwa CUF imefanya maamuzi na mabadiliko ya uongozi. Anataka kumuaminisha jaji Mutungi kuwa sasa signatories wa ruzuku za CUF ni yeye na Magdalena Sakaya. Huu ni utapeli wa wazi ambao Msajili wa vyama vya siasa anapaswa kuwa nao macho.

Upande wa Prof. Lipumba ulikuwa ukikwama kupata ruzuku kutokana na idhinisho la Katibu Mkuu wa CUF, kama mmoja wa signatories/watia sahihi wa kutoa pesa, kukosekana. Prof. Lipumba anadhani na kuamini kuwa kumpa cheo cha Katibu Mkuu Sakaya ni kupata watia sahihi. Anajidanganya. Maalim anapaswa kujitoa rasmi na Sakaya kuingia. Prof. Lipumba atakwama.

Wote wanaomuunga mkono Prof. Lipumba katika utapeli wake huu, kupitia mgongo wa siasa, hawalitakii mema Taifa hili na demokrasia yake. Kama mpenda demokrasia ya kweli, amani, uhuru na umoja wa Taifa, nitawaanika wote walio nyuma ya Prof. Lipumba katika jambo hili la maigizo na utapeli wa kujifanya anaweza kufanya atakalo CUF.

Bastola ya nini tena jamani!?

Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam

Na wewe Uncle utakuwa mmoja wao,kwa sababu kwanini usiwataje leo tukawajua??Wakiendelea kuharibu likitokea la kutokea na wewe uko nyuma yao,unafaidika nao.

Siri huwa hailali,ni kama Wekundu wa msimbazi usipolala kwa jirani
 
Magufuli alipoapishwa tu,mtu wa kwanza kumtembelea Ikulu alikuwa Lipumba,wakateta,ndani ya wiki moja akafutiwa kesi yake mahakamani ambayo alifunguliwaga mwishoni mwa utawala wa Kikwete.

Lipumba akaenda Azam Tv na kuanza kumpamba TrumpRapa huku akimnanga mkwere. Kuanzia hapo visa na viroja vikatamalaki!!

You have the point
 
Kuna watu wamesoma sana ila elimu waliyo ipata haijawasaidia kitu kabisa...Prof mzima na yeye leo amekubali kutumika kisa njaa.....Yaani Bongo hakuna tofauti wa aliepata FAFAFAFA na Professor wote wanongozwa na tumbo....
 
Na wewe Uncle utakuwa mmoja wao,kwa sababu kwanini usiwataje leo tukawajua??Wakiendelea kuharibu likitokea la kutokea na wewe uko nyuma yao,unafaidika nao.

Siri huwa hailali,ni kama Wekundu wa msimbazi usipolala kwa jirani
Mwanangu Tetty, acha nikusanye data za kutosha.

Mzee Tupatupa
 
Mtu aliyejiuzuru anatengua kauli yake na anajirudisha kwenye chama kinguvu na mamlaka zinampa nguvu...Maajabu haya yanatokea tanzania tu
 
Back
Top Bottom