tahadhari:airtel wameanza wizi wao tena!

tahadhari:airtel wameanza wizi wao tena!

figganigga

Platinum Member
Joined
Oct 17, 2010
Posts
27,635
Reaction score
62,523
wale wanao tumia vifurushi vya airtel kaeni makini sana.
wanaibaje?- Hawa jamaa ukijiunga na kifurushi cha siku, wiki au mwezi huwa wana disconnect kabla muda uliolipia haujaisha hasa kama simu yako au kifaa unachokitumia kina hela ya ziada. Ile siku ya mwisho ndo wanakata salio. lakini kama hamna salio mnaenda nao sawa hadi dakika ya mwisho.
So ukinunua kifurushi hakikisha kifaa unacho kitumia hakina heka ya ziada vinginevyo utakuta imekombwa yote.
Mimi baada ya kutokea hilo tatizo nikawaendea hewani wakaniambia tatizo wanalishughulikia lakini hamna kitu. Nami ntakomaa nao hadi wanirudishie hela yangu walio niibia. wameshanikomba salio langu kama mara tatu. So sasa hivi nakua makini na kubakiza hela ninunuapo kifurushi.
Natumia nafasi hii kuwaomba airtel waache kunifanyia uhuni mimi mlala hoi. ni hayo tu. mia
 
Sasa kama simu ina hela baada ya kujiunga niipeleke wapi? Nikiitumia ili wasikate si nitakuwa nimefanya kitu hicho hicho?
 
Mimi imenitokea mara ya pili. Nilienda mlimani city kuwaeleza wakaniambia watarekebisha lakini hakuna kitu. Ukichukua kifurushi cha wiki wanakupiga chini siku ya tano au sita kwenye data, lakini airtime na sms hawakati mpaka mwisho. Kama una smartphone ambayo kila wakati inahitaji access ya internet, hela yako inaliwa zile siku ya mwisho.
 
Hii kitu imenitokea kama mara mbili hivi nikawa najiuliza tatizo ni nini na inatokea kwangu tuu...

Kumbe na nyie wenzangu inawakuta aiseee.....
 
Mkuu mbona mi nimeangalia hapa naona ziko vile vile????

utakua hautumii smartphone.
tatizo linaanza siku mbili za mwisho. mtu unakua unajua kwamba mzigo unaisha jumapili kama kuna hela watskatisha jumamosi. kama simu haina hela hawafanyi. mia
 
kweli kabisa maana jana niliunga cha siku Tsh 600 leo naamka asubuhi nakuta empty nawapigia wananipiga time tu. Asante kwa kunishtua.
 
Me washaniliza mara 2 salio baada kukata bando kabla ya muda wake kufika. Dah! kucheki sms & dakika zipo lkn net bando 0 bytes.
 
kweli kabisa maana jana niliunga cha siku Tsh 600 leo naamka asubuhi nakuta empty nawapigia wananipiga time tu. Asante kwa kunishtua.
Mimi juzi nilijiunga na 900 nikapata MB 400 nikatumia kwenye simu kama nusu saa, asubuhi jana naamka nikakuta 0MB.....Wahuni sana hawa
 
Halafu kitu kingine, wamepandisha gharama za vifurushi bila taarifa.
 
Back
Top Bottom