Tajiri wa matajiri
Senior Member
- Apr 17, 2024
- 166
- 664
TAFSIRI BINAFSI JUU YA KIFO CHA HAYATI JPM KATI YA MSITU MNENE WA TAFSIRI MBALIMBALI NCHINI.
Na Eng. Bishanga G.C. (Edc.facilitator & MP aspirant ) :Kyerwa, Kagera, Tanzania 🇹🇿
gbishanga90@gmail.com
0755372659/ 0625945455
Pole Tanzania, poleni Watanzania
Watanzania tumefiwa na Rais wa nchi, kiongozi wa ngazi ya juu kabisa kuachia nafsi yake ya uongozi kabla ya muda wake kuisha, tena na kutokana na Kifo. Buriani Hayati John Joseph Pombe Magufuri. Historia imeandikwa na Hakika mwendo umeumaliza na Iman yako binafsi umeilinda. Tangulia Shujaa, sisi tutakufuata lakini sasa ngoja tutafsiri yote uliotuachia na tujifunze kutokana na ukweli kwamba Kila jambo ni mpango wa MUNGU binadamu kujifunza.
Tafsiri Yangu juu ya Hayati Magufuli kwa watu Baki (wanyonge)
“Nafanya haya yote kwa ajili ya Watu wanyonge, watu masikini” ni Wimbo ulioimbwa na Hayati JPM Muda wote katika uongozi wake na hakika alionesha kwa vitendo dhamira ya kuwasaidia Wanyonge, masikini nao Waliamini hakika wamepata Kiongozi ambaye anatengeneza njia ya Neema na Matumaini kwa masikini, sasa tangu kutangazwa kwa Msiba huu mzito kila mtu mnyonge/masikini ukimsikiliza kuhusu kuguswa na masiba huo, wanaonekana kabisa KUKATA TAMAA NA MATUMAINI YAO YAMEKWISHA. Kwasababu walikuwa wanamuona JPM ndio MKOMBOZI pekee naye JPM alikuwa anawaona Masikini /wanyonge pekee kuwa ndio wanaostahili Kupata UKOMBOZI wa Kiuchumi. (Sasa Upande mmoja umeondoka na kuacha upande mmoja kuwa yatima )
My Take
Urais ni Taasisi inayopaswa Kujiendesha katika mipango ya kiutendaji na utekelezaji wa mipango hiyo kimfumo (collective responsibility) na sio kibinafsi (individuality), sasa kipi kimetokea wanyonge hawa masikini kukata tamaa ya matumaini waliokuwa nayo kwa JPM maanake ni kwamba Kilichokuwa kinawapa matumaini ya ukombozi sio Mfumo bali ni mtu aliyejiaminisha kaja kwa ajili yao, na baadaye anawaacha.
Nipende kushauri viongozi wakubwa wa kiserikali hasa wenye nafsi kubwa zaidi ya kimaamuzi mbalimbali hasa katika muhimili wa Kiserikali (Executive) waweze kutumia vyombo vya kiutendaji katika maamuzi Yaani kama Bunge (Parliament) na Mahakama (judicial) ambapo huko ndiko kutaonekana kabisa mifumo ya Pamoja inayopangika kikatiba kabisa kimaandishi na kutekelezeka Yaani (collective responsibility) kuliko kuwa na mtu mmoja ambaye amebeba maono (vision) yote kichwani pekeake (individuality)na mfano akija kuanguka shida hii inatokea.
Tafsiri yangu juu ya JPM na Waliobaki kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM) dhidi ya Vyama vya upande wa pili (Vyama vipanzani).
Niseme wazi mimi ni kada mtihifu kabisa wa chama cha mapunduzi , kama Mwanachama nimeumia sana juu ya msiba huu mzito uliotufika kama Taifa lakini kama chama kupoteza Mwenyekiti wa chama chetu aliyetuunganisha takribani kwa miaka 6 ya uongozi wake. Chama kimekuwa madarakani tangu nchi hii kupata uhuru, na kipindi chote hicho chama kimeweza kuleta maendeleo ya hakika kwa vipindi tofauti tofauti vya miaka kumi, kumi kwa awamu nne tofauti kuongozwa na marais tofauti mpaka hii awamu ya tano ya JPM tumefikia Uchumi wa kati, ni Safari ndefu kupigwa tangu tupate Tuanze siasa ya vyama vya upinzani (1992) na uchaguzi wa kwanza wa vyama vya upinzani (1995) naamini mawazo mbadala ya kutoka upande wa pili (vyama pinzani) ndio yaliwezesha kutuimarisha zaidi kama chama kuwa IMARA ZAIDI, hata katika upangazi wa sera na Itikadi umekuwa kuimarika na kuwa bora zaidi katika ILANI zetu za uchaguzi na kuwashinda upande wa pili (vyama pinzani).
My Take
Siasa sio Uadui bali ni chanzo cha kuibua mawazo na fikira kinzani ambazo zikichakatwa vyema zile fikira au wazo zuri lita shida wazo jingine, hivyo chama kimoja ni pinzani au mbadala wa chama kingine kwasababu vyote huleta na kutoa mawazo na fikira tofauti kwa nwenzake (hivyo dhana ya kutaka kuviondoa vyama pinzani, Si fikira sahihi kwasababu ni vyama vinavyotufanya tuimarike zaidi na kuwa chama Tawala kikuu dhidi ya vyama vingine).
Tupendane na kuwafanya Wapinzani ni miongoni mwa wachangia maendeleo nchini, Tukifanya hivyo tutawafanya hata wao kuwa wazalendo wa kuisemea vizuri nchi yetu na sio baadae kuwa “Treat Negative “ na kupandikiza chuki kwao kisha wanaamua hasira zao kuzipeka huko mataifa ya mbali na kuisemea vibaya nchi yetu nasisi tunaanza kuwaita “MABEBERU”. Nchi ni yetu yote kwahiyo sisi tulibaki tupeane nafasi vyema tuijenge nchi yetu kwa Pamoja kati ya mawazo mbadala kwakuwa “MAWAZO HAYAPIGWI RUNGU, MAWAZO BORA ZADI YANAZIDI YALE MWENGINE”
Mwisho zaidi hatuna budi kuanza upya kurekebisha pale kuliko na upungufu na kuijenga nchi yetu na kuendeleza yale mazuri ambayo Hayati JPM aliyaanzisha na hasa yale mambo mazuri aliyokuwa akiyaamini na kuyatekeleza bila ya kushirikisha Mihimili mengine kama Bunge na mahakama basi yaende huko yakatachakatwe na yaletwe katika maandishi ili yaingie kwenye utekelezaji na sio kuondoka nayo na kupoteza mambo mazuri ambayo mpendwa wetu Hayati JPM aliyaanzisha.
Na Eng. Bishanga G.C. (Edc.facilitator & MP aspirant ) :Kyerwa, Kagera, Tanzania 🇹🇿
gbishanga90@gmail.com
0755372659/ 0625945455
Pole Tanzania, poleni Watanzania
Watanzania tumefiwa na Rais wa nchi, kiongozi wa ngazi ya juu kabisa kuachia nafsi yake ya uongozi kabla ya muda wake kuisha, tena na kutokana na Kifo. Buriani Hayati John Joseph Pombe Magufuri. Historia imeandikwa na Hakika mwendo umeumaliza na Iman yako binafsi umeilinda. Tangulia Shujaa, sisi tutakufuata lakini sasa ngoja tutafsiri yote uliotuachia na tujifunze kutokana na ukweli kwamba Kila jambo ni mpango wa MUNGU binadamu kujifunza.
Tafsiri Yangu juu ya Hayati Magufuli kwa watu Baki (wanyonge)
“Nafanya haya yote kwa ajili ya Watu wanyonge, watu masikini” ni Wimbo ulioimbwa na Hayati JPM Muda wote katika uongozi wake na hakika alionesha kwa vitendo dhamira ya kuwasaidia Wanyonge, masikini nao Waliamini hakika wamepata Kiongozi ambaye anatengeneza njia ya Neema na Matumaini kwa masikini, sasa tangu kutangazwa kwa Msiba huu mzito kila mtu mnyonge/masikini ukimsikiliza kuhusu kuguswa na masiba huo, wanaonekana kabisa KUKATA TAMAA NA MATUMAINI YAO YAMEKWISHA. Kwasababu walikuwa wanamuona JPM ndio MKOMBOZI pekee naye JPM alikuwa anawaona Masikini /wanyonge pekee kuwa ndio wanaostahili Kupata UKOMBOZI wa Kiuchumi. (Sasa Upande mmoja umeondoka na kuacha upande mmoja kuwa yatima )
My Take
Urais ni Taasisi inayopaswa Kujiendesha katika mipango ya kiutendaji na utekelezaji wa mipango hiyo kimfumo (collective responsibility) na sio kibinafsi (individuality), sasa kipi kimetokea wanyonge hawa masikini kukata tamaa ya matumaini waliokuwa nayo kwa JPM maanake ni kwamba Kilichokuwa kinawapa matumaini ya ukombozi sio Mfumo bali ni mtu aliyejiaminisha kaja kwa ajili yao, na baadaye anawaacha.
Nipende kushauri viongozi wakubwa wa kiserikali hasa wenye nafsi kubwa zaidi ya kimaamuzi mbalimbali hasa katika muhimili wa Kiserikali (Executive) waweze kutumia vyombo vya kiutendaji katika maamuzi Yaani kama Bunge (Parliament) na Mahakama (judicial) ambapo huko ndiko kutaonekana kabisa mifumo ya Pamoja inayopangika kikatiba kabisa kimaandishi na kutekelezeka Yaani (collective responsibility) kuliko kuwa na mtu mmoja ambaye amebeba maono (vision) yote kichwani pekeake (individuality)na mfano akija kuanguka shida hii inatokea.
Tafsiri yangu juu ya JPM na Waliobaki kwenye Chama Cha Mapinduzi (CCM) dhidi ya Vyama vya upande wa pili (Vyama vipanzani).
Niseme wazi mimi ni kada mtihifu kabisa wa chama cha mapunduzi , kama Mwanachama nimeumia sana juu ya msiba huu mzito uliotufika kama Taifa lakini kama chama kupoteza Mwenyekiti wa chama chetu aliyetuunganisha takribani kwa miaka 6 ya uongozi wake. Chama kimekuwa madarakani tangu nchi hii kupata uhuru, na kipindi chote hicho chama kimeweza kuleta maendeleo ya hakika kwa vipindi tofauti tofauti vya miaka kumi, kumi kwa awamu nne tofauti kuongozwa na marais tofauti mpaka hii awamu ya tano ya JPM tumefikia Uchumi wa kati, ni Safari ndefu kupigwa tangu tupate Tuanze siasa ya vyama vya upinzani (1992) na uchaguzi wa kwanza wa vyama vya upinzani (1995) naamini mawazo mbadala ya kutoka upande wa pili (vyama pinzani) ndio yaliwezesha kutuimarisha zaidi kama chama kuwa IMARA ZAIDI, hata katika upangazi wa sera na Itikadi umekuwa kuimarika na kuwa bora zaidi katika ILANI zetu za uchaguzi na kuwashinda upande wa pili (vyama pinzani).
My Take
Siasa sio Uadui bali ni chanzo cha kuibua mawazo na fikira kinzani ambazo zikichakatwa vyema zile fikira au wazo zuri lita shida wazo jingine, hivyo chama kimoja ni pinzani au mbadala wa chama kingine kwasababu vyote huleta na kutoa mawazo na fikira tofauti kwa nwenzake (hivyo dhana ya kutaka kuviondoa vyama pinzani, Si fikira sahihi kwasababu ni vyama vinavyotufanya tuimarike zaidi na kuwa chama Tawala kikuu dhidi ya vyama vingine).
Tupendane na kuwafanya Wapinzani ni miongoni mwa wachangia maendeleo nchini, Tukifanya hivyo tutawafanya hata wao kuwa wazalendo wa kuisemea vizuri nchi yetu na sio baadae kuwa “Treat Negative “ na kupandikiza chuki kwao kisha wanaamua hasira zao kuzipeka huko mataifa ya mbali na kuisemea vibaya nchi yetu nasisi tunaanza kuwaita “MABEBERU”. Nchi ni yetu yote kwahiyo sisi tulibaki tupeane nafasi vyema tuijenge nchi yetu kwa Pamoja kati ya mawazo mbadala kwakuwa “MAWAZO HAYAPIGWI RUNGU, MAWAZO BORA ZADI YANAZIDI YALE MWENGINE”
Mwisho zaidi hatuna budi kuanza upya kurekebisha pale kuliko na upungufu na kuijenga nchi yetu na kuendeleza yale mazuri ambayo Hayati JPM aliyaanzisha na hasa yale mambo mazuri aliyokuwa akiyaamini na kuyatekeleza bila ya kushirikisha Mihimili mengine kama Bunge na mahakama basi yaende huko yakatachakatwe na yaletwe katika maandishi ili yaingie kwenye utekelezaji na sio kuondoka nayo na kupoteza mambo mazuri ambayo mpendwa wetu Hayati JPM aliyaanzisha.
