stewart frenk
Member
- Jun 9, 2013
- 48
- 15
Nimekuwa nasoma threads mbalimbali juu ya upotoshaji mkubwa unaofanywa na watu wanaotuona sisi mazuzu tafsiri ya maudhui ya uwepo wa RED BRIGADE.Kwanza kwa mtu makini hatakiwi kutafasiri jambo ambalo lipo kwenye katiba ya taasisi nje ya tafsiri ya na mantiki ya humo kwa hiyo kutafsiri RED BRIGADE kwa kufanya infarance ya ITALY ni kiwango cha hali ya juu cha upotoshaji na kutudhani sie ni mambumbu HOJA tunatafasiri RED BRIGADE kwa kuona mantiki ya kuundwa uwepo na kazi zake(ulinzi wa mali na viongozi).Katiba ya Tanzania inakataza mtu au taasisi yeyote kuwa na Jeshi(ibara 147) Je tuseme Jeshi la wokovu pale kurasini ni uvunjifu wa katiba?Hapana Sioni dhambi yeyote kwa chadema kuwa na kikundi maalumu kwa ajili ya ulinzi wa mali na viongozi wake ambapo kuna Taasisi nyingi za watu binafsi zinafanya shughuli hii(ulinzi). Na wanatumia hadi silaha za moto Group4,ultimate security etc zote ni ulinzi na usalama wa mali Je vyombo vya dola vimeshindwa kazi hapana huo ndio ulinzi shirikishi.Nilidhani hawa jamaa (CHADEMA) wangepongezwa kuimarisha ulinzi wa mali na viongozi maana wanatekeleza dhana ya Ulinzi shirikishi na Polisi jamii ambayo itapunguza kiwango cha jinai kuliko upotoshaji unaofanywa
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums