Tafakuri ya leo

Tafakuri ya leo

Dogoli kinyamkela

JF-Expert Member
Joined
Nov 21, 2024
Posts
2,144
Reaction score
3,459
Kaini alimuua Abeli, kisha akafukuzwa na kwenda kuishi nchi ya mbali na kule akaanzisha uzao wake!!🤔

Je Kaini alimuoa nani kule nchi ya mbali? Alizaa na nani?🤷🏿

Ikiwa Dunia ilikuwa na Adam & Eva
(Watu wawili tu)

Nao wakazaa Kaini & Abeli
(Wakawa 4)

Abeli akafa wakabaki Mtu tatu!!

Kaini Alizaa na nani kule nchi ya mbali?

Kitabu kinasema baadae
Adam & Eva walimzaa Seth na baadae wakazaa watoto wengine (BAADAE)🤔

Hapo lakini Kaini tayari alishaanzisha uzao wake! Je Alianzisha na nani?🤔

Inawezekana Adam & Hawa hawakuwa watu wa kwanza duniani hapa, tayari dunia ilishakuwa na watu kabla yao?🤔

Au inawezekana Eva hakuwa mwanamke wa kwanza kwa Adamu, tayari Adamu alishakuwa na Ma’mtu mwingine kabla na wakazaa watoto?🤔

Au je mwanamke huyo ndo’ yule LILITH?🤔

Kivyovyote vile Kaini alilala na Sister Ake!!
1755465687430.jpg
 
Hizo ni hadithi tu.

"Mungu alisema Tuumbe mtu kwa mfano wetu".

Mungu alikuwa na nani? Au wako wa ngapi Miungu?

Walimuumba Adam kwa mfano wao, kisha waka muumba Hawa kutoka ubavu wa Adam.

Eva/Hawa ni mfano wa nani?

Shetani alitupwa duniani, lakini alifika bustani ya Eden kuwa rubuni Adam na Hawa, hiyo Eden iko Duniani?

Adam na hawa nao walivyo kula tunda la mti wa kati, Mungu aliwafukuza Kutoka bustani ya Eden, nani alibaki huko Eden na Eden iko wapi Mbinguni au Duniani?
 
Hizo ni hadithi tu.

"Mungu alisema Tuumbe mtu kwa mfano wetu".

Mungu alikuwa na nani? Au wako wa ngapi Miungu?

Walimuumba Adam kwa mfano wao, kisha waka muumba Hawa kutoka ubavu wa Adam.

Eva ni mfano wa nani?

Shetani alitupwa duniani, lakini alifika busyani ya Eden kuwa rubini Adam na Hawa, hiyo Eden iko Duniani?

Adam na hawa nao walivyo kula tunda la mti wa kati, Mungu aliwafukuza Kutoka bustani ya Eden, nani alibaki huko Eden na Eden iko wapi Mbinguni au Duniani?
Inafikilisha sana
 
Abeli akafa wakabaki Mtu tatu!!
Hapana kabla na baada walikua wanaendelea kuzaa watoto wengine na sio kwamba walikua hao tu, ila kisa chao ndio kiliwasimulia hao tu, unajua biblia ni imeandikwa kwa maneno fulani fikirishi sana

Biblia ya zamani ilikua inamtaja roho mtakatifu km holy ghost ila baadae walipokaa wakalemba maneno kwamba ni holy spirit

Sasa issue inakuja ni pale watu walipohoji kwamba mwili wa Yesu haukuwepo kaburini ila mwili huo huo unaweza kupenya kwenye kuta za nyumba bila kufungua mlango mbaya zaidi wakasema mwili huo ukapaa na ulionekana na wanafunzi wake ukipaa, kiukweli kilichokua kinasimuliwa hapo ni mzimu wa Yesu sio mwili halisi halisia wa Yesu, kilichokua kinazungumziwa ni Mzimu.

Kwa hio leo hii ukiambiwa unaabudu Mzimu wa Yesu aliekwishakufa usikatae ndio maana tamaduni imeendelea mpaka leo kwa wale wenye imani fulani wanaabudu mizimu ya waliokufa kwa kuwaita watakatifu, utasikia wakiimba Mtakatifu fulani utuombee hapo wanaiambia mizimu
 
Eti Mungu alimtupa Shetani duniani na sisi wanadamu viumbe wake wapendwa nasi tuko duniani.

Kwanini shetani asingetupwa Mercury au Jupiter ili kumtenganisha na wanadamu?

Kwa mapenzi yake alituchanganya na shetani halafu siku ya mwisho aje atuhukumu, hiyo inakuingia akilini?

Usikute wanadamu ndiye shetani mwenyewe, au mwenzetu uwe uliwahi kumuona shetani dunia hii.
 
Habari za Vizazi katika Biblia zilizingatia zaid ma MAIN CHARACTER wa story.
Mfano, soma habari za uzazi wa Yesu Kristo utakuta ni wanaume wamezaana... je hapakua na wanawake?
 
Kaini alimuua Abeli, kisha akafukuzwa na kwenda kuishi nchi ya mbali na kule akaanzisha uzao wake!!🤔

Je Kaini alimuoa nani kule nchi ya mbali? Alizaa na nani?🤷🏿

Ikiwa Dunia ilikuwa na Adam & Eva
(Watu wawili tu)

Nao wakazaa Kaini & Abeli
(Wakawa 4)

Abeli akafa wakabaki Mtu tatu!!

Kaini Alizaa na nani kule nchi ya mbali?

Kitabu kinasema baadae
Adam & Eva walimzaa Seth na baadae wakazaa watoto wengine (BAADAE)🤔

Hapo lakini Kaini tayari alishaanzisha uzao wake! Je Alianzisha na nani?🤔

Inawezekana Adam & Hawa hawakuwa watu wa kwanza duniani hapa, tayari dunia ilishakuwa na watu kabla yao?🤔

Au inawezekana Eva hakuwa mwanamke wa kwanza kwa Adamu, tayari Adamu alishakuwa na Ma’mtu mwingine kabla na wakazaa watoto?🤔

Au je mwanamke huyo ndo’ yule LILITH?🤔

Kivyovyote vile Kaini alilala na Sister Ake!!View attachment 3444703
Kaini alizaa a Dadaake na ndio kisa cha ugomvi uliopeelekea kifo cha Abel kwakua walikua wakimgombania.
 
Hizo ni hadithi tu.

"Mungu alisema Tuumbe mtu kwa mfano wetu".

Mungu alikuwa na nani? Au wako wa ngapi Miungu?

Walimuumba Adam kwa mfano wao, kisha waka muumba Hawa kutoka ubavu wa Adam.

Eva ni mfano wa nani?

Shetani alitupwa duniani, lakini alifika bustani ya Eden kuwa rubuni Adam na Hawa, hiyo Eden iko Duniani?

Adam na hawa nao walivyo kula tunda la mti wa kati, Mungu aliwafukuza Kutoka bustani ya Eden, nani alibaki huko Eden na Eden iko wapi Mbinguni au Duniani?
Haya maswali ukiimuuliza yule Askofu atakwambia Adamu ndio Hawa na Hawa ndio Adamu wanachotofautiana ni via vya uzazi tu ila kitu ni kile kile yaan hawana tofauti yoyote anachoweza kufanya Adamu hata Hawa anaweza kukifanya hilo ndilo jibu lake la mkazo zaidi anasimamiaga hapo.

Hapo kwa Shetani atakwambia kwamba Shetani alikua Malaika aliependwa na Mungu sana, ni km mtoto wa Mwisho anavyopendwa na kile walichopewa Adamu na Hawa yeye alitegemea atapewa yeye yaan yeye alitaka yeye ndio awe wa Mwisho km kifunga mimba yaan kusiwe na watoto wengine wa Mungu, ndio Watoto wa Mungu, lakini Mungu alipowatoto Watoto weengine wawili Shetani akasema Baba hizi mali nilijua ukifa narithi mimi sasa umeongeza hawa Washeenzi wengine na mali yenyewe ndogo kiasi hiki basi hawa ngoja niwafanyie figisu wafukuzwe nirithi mimi kila kitu, baada ya hapo kukazuka vita kali sana mbinguni na Shetani akashindwa Vita ndio wakatupwa wote duniani.

Kuhusu Edeni ipo wapi MBINGUNI au DUNIANI, atakujibu kwamba Edeni ni hapo hapo ulipo hakuna MBINGUNI wala DUNIANI, ni kwa mujibu wa Askofu sio mimi
 
Haya maswali ukiimuuliza yule Askofu atakwambia Adamu ndio Hawa na Hawa ndio Adamu wanachotofautiana ni via vya uzazi tu ila kitu ni kile kile yaan hawana tofauti yoyote anachoweza kufanya Adamu hata Hawa anaweza kukifanya hilo ndilo jibu lake la mkazo zaidi anasimamiaga hapo.

Hapo kwa Shetani atakwambia kwamba Shetani alikua Malaika aliependwa na Mungu sana, ni km mtoto wa Mwisho anavyopendwa na kile walichopewa Adamu na Hawa yeye alitegemea atapewa yeye yaan yeye alitaka yeye ndio awe wa Mwisho km kifunga mimba yaan kusiwe na watoto wengine wa Mungu, ndio Watoto wa Mungu, lakini Mungu alipowatoto Watoto weengine wawili Shetani akasema Baba hizi mali nilijua ukifa narithi mimi sasa umeongeza hawa Washeenzi wengine na mali yenyewe ndogo kiasi hiki basi hawa ngoja niwafanyie figisu wafukuzwe nirithi mimi kila kitu, baada ya hapo kukazuka vita kali sana mbinguni na Shetani akashindwa Vita ndio wakatupwa wote duniani.

Kuhusu Edeni ipo wapi MBINGUNI au DUNIANI, atakujibu kwamba Edeni ni hapo hapo ulipo hakuna MBINGUNI wala DUNIANI, ni kwa mujibu wa Askofu sio mimi
Sasa kama shetani alilianzisha timbwili Ilikuwaje Adam na Hawa nao watupwe duniani? Au kwa Mungu hakuna mahakama na sheria kuangali nani mkorofi/mkosefu ni ikatenda Haki?

Tunaambiwa Adam aliishi Eden na Hawa ila waliambiwa wale kila kitu isipokuwa matunda ya mti wa kati kati.

Shetani alikuja akamwambia Hawa usiwe fala kula uone, akala akaona kisga akamfuata Adam na kumshawishi naye ale aone, naye hskufanya ajizi akala wote wakaona mengi na hata kujua kwamba wako uchi.

Kwanini hakuwapa nafasi ya kuwasikiliza ili aelewe walichokifanya haikuwa ridhaa yao bali walidanganywa?!

Ila sisi tunaambiwa Mungu ana huruma, tukitubu tu anatusamehe, lakini hakuwasamehe Adam na Hawa.

Au kuna maelezo ya kesi na hukumu hayakupatikana wakati wa uandishi wa biblia.
 
Kaini alimuua Abeli, kisha akafukuzwa na kwenda kuishi nchi ya mbali na kule akaanzisha uzao wake!!🤔

Je Kaini alimuoa nani kule nchi ya mbali? Alizaa na nani?🤷🏿

Ikiwa Dunia ilikuwa na Adam & Eva
(Watu wawili tu)

Nao wakazaa Kaini & Abeli
(Wakawa 4)

Abeli akafa wakabaki Mtu tatu!!

Kaini Alizaa na nani kule nchi ya mbali?

Kitabu kinasema baadae
Adam & Eva walimzaa Seth na baadae wakazaa watoto wengine (BAADAE)🤔

Hapo lakini Kaini tayari alishaanzisha uzao wake! Je Alianzisha na nani?🤔

Inawezekana Adam & Hawa hawakuwa watu wa kwanza duniani hapa, tayari dunia ilishakuwa na watu kabla yao?🤔

Au inawezekana Eva hakuwa mwanamke wa kwanza kwa Adamu, tayari Adamu alishakuwa na Ma’mtu mwingine kabla na wakazaa watoto?🤔

Au je mwanamke huyo ndo’ yule LILITH?🤔

Kivyovyote vile Kaini alilala na Sister Ake!!View attachment 3444703
1. Kain Alimuoa Nani na Alizaa na Nani?
Biblia (Mwanzo 4:17) inasema kwamba Kain alimudu mke wake, naye akazaa Henoki, na kwamba Kain alijenga mji. Hata hivyo, Biblia haimtaji kwa jina mke wa Kain wala asili yake. Kulingana na maandiko, Adamu na Hawa ndio walikuwa watu wa kwanza (Mwanzo 1:27, 2:7, 2:22), na wao walizaa watoto wengi, ikiwa ni pamoja na Kain, Abeli, Sethi, na "wengineo wanaume na wanawake" (Mwanzo 5:4).
Tafsiri ya kawaida ya Kikristo na ya Kiyahudi ni kwamba Kain alimuoa dada yake au mjukuu wa Adamu na Hawa. Hii inatokana na ukweli kwamba, kulingana na maandiko, hakuna binadamu wengine waliotajwa kabla ya Adamu na Hawa. Katika siku za mwanzo, ndoa kati ya ndugu au jamaa wa karibu ziliruhusiwa kwa sababu idadi ya watu ilikuwa ndogo, na sheria za baadaye za kumudu jamaa wa karibu (kama zilivyoainishwa katika Mambo ya Walawi 18) hazikuwepo wakati huo. Kwa hiyo, Kain anaweza kuwa alimuoa dada yake au mjukuu wa Adamu na Hawa, na naye akazaa watoto.
2. Je, Dunia Ilikuwa na Watu Wengine Kabla ya Adamu na Hawa?
Kulingana na maandiko ya Mwanzo, Adamu na Hawa waliumbwa kama binadamu wa kwanza (Mwanzo 1:26-27, 2:7). Biblia haionyeshi uwepo wa watu wengine kabla yao. Hata hivyo, kuna nadharia za kitheolojia na tafsiri za kihistoria ambazo zinadhani kwamba labda kulikuwa na watu wengine ambao hawakutajwa moja kwa moja katika maandiko. Nadharia hizi hazipati msingi wa moja kwa moja katika Biblia bali zinatokana na maswali kama lako, hasa kutokana na swali la "Kain alimuoa nani?".
Tafsiri ya Kibiblia: Maandiko ya Mwanzo yanasisitiza kwamba Adamu na Hawa ndio asili ya binadamu wote, na watoto wao (pamoja na wajukuu) walieneza idadi ya watu duniani. Hivyo, hakuna dalili ya moja kwa moja kwamba kulikuwa na watu wengine kabla ya Adamu na Hawa.
Tafsiri za Nje ya Biblia: Baadhi ya wasomi wanasema kwamba labda maandiko ya Mwanzo ni ya mfano (allegorical) au yanawasilisha hadithi ya kikundi cha watu badala ya watu binafsi wawili tu. Hata hivyo, hii ni tafsiri ya kisasa na haipati msingi wa moja kwa moja katika maandiko.
3. Je, Adamu Alikuwa na Mke Mwingine Kabla ya Hawa, kama Lilith?
Hadithi ya Lilith haipatikani katika Biblia ya Kikristo au ya Kiyahudi (Tanakh) kama ilivyoandikwa. Lilith anatajwa katika hadithi za kale za Kiyahudi, hasa katika maandiko ya kabla ya karne za kati kama vile Alphabets of Ben Sira (karne ya 8-10 BK) na katika hekaya za Kikabala (kama Zohar). Kulingana na hadithi hizi, Lilith alikuwa mke wa kwanza wa Adamu, aliumbwa sawa na yeye (sio kutoka kwa mbavu yake kama Hawa), lakini alikataa kujisalimisha kwake na akaondoka Edeni. Baada ya hapo, Hawa aliumbwa kama mke wa pili.
Hata hivyo:
Lilith si Sehemu ya Biblia: Hadithi ya Lilith ni ya kihekaya (mythological) na haipatikani katika maandiko ya Mwanzo wala katika Biblia yote. Katika Biblia, Hawa ndiye mke wa kwanza na wa pekee wa Adamu anayetajwa (Mwanzo 2:22-24).
Asili ya Lilith: Jina la Lilith linatoka katika hadithi za kale za Mesopotamia, ambapo alikuwa roho au shetani wa kike. Katika Isaya 34:14, neno "Lilith" linatajwa katika toleo la Kiebrania (linalotafsiriwa kama "screech owl" au "viumbe vya usiku" katika toleo la King James), lakini hii haimaanishi kuwa ni mtu halisi bali roho au kiumbe cha hadithi.
Msimamo wa Kikristo: Wengi wa Wakristo wanakataa wazo la Lilith kama sehemu ya maandiko ya Biblia, na wanaona kuwa Hawa ndiye mke pekee wa Adamu.
4. Hitimisho
Kulingana na maandiko ya Biblia:
Kain alimuoa dada yake au mjukuu wa Adamu na Hawa, kwani hakuna watu wengine waliotajwa katika maandiko wakati huo.
Adamu na Hawa ndio binadamu wa kwanza kulingana na Mwanzo, na hakuna dalili ya moja kwa moja ya watu wengine kabla yao.
Hadithi ya Lilith si sehemu ya Biblia bali ni ya kihekaya, na haizingatiwi kama sehemu ya historia ya Kikristo au ya Kiyahudi ya Orthodox.
 
Sasa kama shetani alilianzisha timbwili Ilikuwaje Adam na Hawa nao watupwe duniani? Au kwa Mungu hakuna mahakama na sheria kuangali nani mkorofi/mkosefu ni ikatenda Haki?

Tunaambiwa Adam aliishi Eden na Hawa ila waliambiwa wale kila kitu isipokuwa matunda ya mti wa kati kati.

Shetani alikuja akamwambia Hawa usiwe fala kula uone, akala akaona kisga akamfuata Adam na kumshawishi naye ale aone, naye hskufanya ajizi akala wote wakaona mengi na hata kujua kwamba wako uchi.

Kwanini hakuwapa nafasi ya kuwasikiliza ili aelewe walichokifanya haikuwa ridhaa yao bali walidanganywa?!

Ila sisi tunaambiwa Mungu ana huruma, tukitubu tu anatusamehe, lakini hakuwasamehe Adam na Hawa.

Au kuna maelezo ya kesi na hukumu hayakupatikana wakati wa uandishi wa biblia.
Kwa kweli maswali yako haya Askofu hapendi kuulizwa maana yanafikirisha sana ila pia hujazungumzia ile kauli ya alichounganisha Mungu pinadamu asitenganishe hio sentensi Askofu anaitumia sana kwenye kuelezea mada ya Ndoa kwamba mfungishaji wa ndoa wa kwanza alikua ni Mungu mwenyewe

Lakini pia Askofu ataenda na kukwambia Yesu alisema Mungu ni Upendo yaan unapendana na mwenzio ndio yupo katikati yenu kuudumisha Upendo, ataenda mbali zaidi kwamba pamoja na kwamba hakuwasamehe ila hakuwaacha alichofanya aliwaondoa kule kuliko na Malaika

Askofu ataenda mbali na kukwambia kabla ya mwili kwanza iliumbwa Roho, kwa hio ujue tofauti ya Mwili na Roho, Mungu anaishi Rohoni sio Mwilini, hayo ni maelezo ya Askofu sio mimi
 
Eti Mungu alimtupa Shetani duniani na sisi wanadamu viumbe wake wapenda nasi tuko duniani.

Kwanini shetani asingetupwa Mercury au Jupiter ili kumtenganisha na wanadamu?

Kwa mapenzi yake alituchanganya na shetani halafu siku ya mwisho aje atuhukumu, hiyo inakuingia akilini?

Usikute wanadamu ndiye shetani mwenyewe, au mwrnzetu uwe uliwahi kumuona shetani dunia hii.
Labda ndio ule msemo unasema , shetani wa mtu ni mtu
 
Kaini alimuua Abeli, kisha akafukuzwa na kwenda kuishi nchi ya mbali na kule akaanzisha uzao wake!!🤔

Je Kaini alimuoa nani kule nchi ya mbali? Alizaa na nani?🤷🏿

Ikiwa Dunia ilikuwa na Adam & Eva
(Watu wawili tu)

Nao wakazaa Kaini & Abeli
(Wakawa 4)

Abeli akafa wakabaki Mtu tatu!!

Kaini Alizaa na nani kule nchi ya mbali?

Kitabu kinasema baadae
Adam & Eva walimzaa Seth na baadae wakazaa watoto wengine (BAADAE)🤔

Hapo lakini Kaini tayari alishaanzisha uzao wake! Je Alianzisha na nani?🤔

Inawezekana Adam & Hawa hawakuwa watu wa kwanza duniani hapa, tayari dunia ilishakuwa na watu kabla yao?🤔

Au inawezekana Eva hakuwa mwanamke wa kwanza kwa Adamu, tayari Adamu alishakuwa na Ma’mtu mwingine kabla na wakazaa watoto?🤔

Au je mwanamke huyo ndo’ yule LILITH?🤔

Kivyovyote vile Kaini alilala na Sister Ake!!View attachment 3444703

Ni hivi

Baada ya Kaini kumuua ndugu yake Abeli (Mwanzo 4:8), Mungu alimlaani na kumwondoa katika uso wa nchi hiyo.

Kaini akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, upande wa mashariki mwa Edeni (Mwanzo 4:16).

Huko akaoa na kuzaa watoto.

Swali kubwa: Kaini alimuoa nani, wakati kulikuwa na watu wachache duniani?

1. Mtazamo wa Biblia

Biblia haisemi moja kwa moja ni nani aliyekuwa mke wa Kaini.

Lakini Mwanzo 5:4 unasema: “Adamu akaishi miaka 800 baada ya kumzaa Seti, akazaa wana na binti.”

Hii inamaanisha Adamu na Hawa walizaa watoto wengi zaidi (wana na binti) kuliko wale wachache waliotajwa majina.

Kwa hiyo mke wa Kaini aliweza kuwa dada yake au mjamaa wake wa karibu.

2. Kwa nini ilikuwa sawa wakati huo?

Mwanzo wa mwanadamu, kulikuwa hakuna sheria zilizokataza ndugu kuoana.

Sheria dhidi ya ndoa za kindugu zilitolewa baadaye katika Torati (Mambo ya Walawi 18).

Pia, wakati huo kizazi kilikuwa karibu sana na ukamilifu wa maumbile ya asili, hivyo matatizo ya vinasaba (genetic defects) hayakuwa makubwa kama yalivyo sasa.

Kwa ufupi:
Kaini alipofukuzwa, alienda nchi ya Nodi na akaoa mmoja wa ndugu zake wa kike (dada au mjukuu wa Adamu na Hawa). Biblia inasema Adamu na Hawa walizaa watoto wengi, ila haikuwataja wote kwa majina.
 
Tatizo mnaisoma biblia kama novel, kwa mtazamo huu mtafeli pakubwa
 
Hapana kabla na baada walikua wanaendelea kuzaa watoto wengine na sio kwamba walikua hao tu, ila kisa chao ndio kiliwasimulia hao tu, unajua biblia ni imeandikwa kwa maneno fulani fikirishi sana

Biblia ya zamani ilikua inamtaja roho mtakatifu km holy ghost ila baadae walipokaa wakalemba maneno kwamba ni holy spirit

Sasa issue inakuja ni pale watu walipohoji kwamba mwili wa Yesu haukuwepo kaburini ila mwili huo huo unaweza kupenya kwenye kuta za nyumba bila kufungua mlango mbaya zaidi wakasema mwili huo ukapaa na ulionekana na wanafunzi wake ukipaa, kiukweli kilichokua kinasimuliwa hapo ni mzimu wa Yesu sio mwili halisi halisia wa Yesu, kilichokua kinazungumziwa ni Mzimu.

Kwa hio leo hii ukiambiwa unaabudu Mzimu wa Yesu aliekwishakufa usikatae ndio maana tamaduni imeendelea mpaka leo kwa wale wenye imani fulani wanaabudu mizimu ya waliokufa kwa kuwaita watakatifu, utasikia wakiimba Mtakatifu fulani utuombee hapo wanaiambia mizimu
Una akili sana 🤣🤣
 
Ni hivi

Baada ya Kaini kumuua ndugu yake Abeli (Mwanzo 4:8), Mungu alimlaani na kumwondoa katika uso wa nchi hiyo.

Kaini akaenda kuishi katika nchi ya Nodi, upande wa mashariki mwa Edeni (Mwanzo 4:16).

Huko akaoa na kuzaa watoto.

Swali kubwa: Kaini alimuoa nani, wakati kulikuwa na watu wachache duniani?

1. Mtazamo wa Biblia

Biblia haisemi moja kwa moja ni nani aliyekuwa mke wa Kaini.

Lakini Mwanzo 5:4 unasema: “Adamu akaishi miaka 800 baada ya kumzaa Seti, akazaa wana na binti.”

Hii inamaanisha Adamu na Hawa walizaa watoto wengi zaidi (wana na binti) kuliko wale wachache waliotajwa majina.

Kwa hiyo mke wa Kaini aliweza kuwa dada yake au mjamaa wake wa karibu.

2. Kwa nini ilikuwa sawa wakati huo?

Mwanzo wa mwanadamu, kulikuwa hakuna sheria zilizokataza ndugu kuoana.

Sheria dhidi ya ndoa za kindugu zilitolewa baadaye katika Torati (Mambo ya Walawi 18).

Pia, wakati huo kizazi kilikuwa karibu sana na ukamilifu wa maumbile ya asili, hivyo matatizo ya vinasaba (genetic defects) hayakuwa makubwa kama yalivyo sasa.

Kwa ufupi:
Kaini alipofukuzwa, alienda nchi ya Nodi na akaoa mmoja wa ndugu zake wa kike (dada au mjukuu wa Adamu na Hawa). Biblia inasema Adamu na Hawa walizaa watoto wengi, ila haikuwataja wote kwa majina.
Ikiwa tunaenda kwa msitari wa Biblia pekee → Kaini alimuoa dada yake (au mjukuu wa Adamu na Eva).

Ikiwa tunaenda kwa mapokeo ya midrash na simulizi → huenda kulikuwa na mwanamke mwingine kama Lilith.

Ikiwa tunaangalia sayansi na falsafa → huenda Adam na Eva hawakuwa “wanadamu wa kwanza” duniani, bali watu wa kwanza kwenye mstari wa kiroho (Biblical lineage).


Kwa ufupi:

Kibiblia: Mke wa Kaini alikuwa dada yake.

Kimaapokeo (Talmud/Lilith): Huenda alimuoa mwanamke mwingine aliyekuwepo kabla ya Eva.

Kifalsafa/kisasa: Huenda walikuwepo binadamu wengine nje ya familia ya Adamu na Eva.
 
Eti Mungu alimtupa Shetani duniani na sisi wanadamu viumbe wake wapenda nasi tuko duniani.

Kwanini shetani asingetupwa Mercury au Jupiter ili kumtenganisha na wanadamu?

Kwa mapenzi yake alituchanganya na shetani halafu siku ya mwisho aje atuhukumu, hiyo inakuingia akilini?

Usikute wanadamu ndiye shetani mwenyewe, au mwrnzetu uwe uliwahi kumuona shetani dunia hii.
Biblia

Ukimfuatilia Mungu wa Agano la Kale kisha ukaja ukamfuatilia Mungu wa Agano Jipya, utaelewa jambo kwa mujibu wa Askofu

Askofu hua hamzungumziagi sana Shetani ni mara chache mno kumsikia Askofu akimzungumzia Shetani maana hapo kwa Shetani ukimbananisha Askofu unamtoa knockout,

Yes of course kwa maelezo ya Askofu, wewe una kishetani chako kimoja pembeni pamoja na kimalaika chako kimoja pembeni hicho kishetani kazi yake ni kukushauri ufanye matendo ya jino kwa jino wamekuzingua wapeleekee gharika, wamekuzingua waue uzaliwa wao wa kwanza, halafu kuna kimalaika upande wa pili kinakwambia mpende jirani yako km unavyojipenda akikupiga shavu la kulia mgeuzie la kushoto akuongezee lingine, akichukua koti lako mpe na shati pia

Sasa hicho kishetani na hicho kimalaika ndivyo vinavyokuwakilisha wewe, sasa hivi mashetani wameumbiwa majehana na kuzimu za duniani ukiua unapelekwa mahakamani baadae ya kesi unapelekwa kuzimu au jehanamu ukamuone shetani anavyoishi ishi hapa duniani, hio ndio kuzimu

Askofu anaenda mbali anasema hakuna tofauti ya mbinguni na duniani, hapo hapo ulipo ndio mbinguni hapohapo ulipo ndio duniani, wewe ni Mungu Mdogo kwenye umbo la mwili ila huna unachoweza kumzidi Mungu Mkuu

Askofu akaishia hapo
 
Biblia

Ukimfuatilia Mungu wa Agano la Kale kisha ukaja ukamfuatilia Mungu wa Agano Jipya, utaelewa jambo kwa mujibu wa Askofu

Askofu hua hamzungumziagi sana Shetani ni mara chache mno kumsikia Askofu akimzungumzia Shetani maana hapo kwa Shetani ukimbananisha Askofu unamtoa knockout,

Yes of course kwa maelezo ya Askofu, wewe una kishetani chako kimoja pembeni pamoja na kimalaika chako kimoja pembeni hicho kishetani kazi yake ni kukushauri ufanye matendo ya jino kwa jino wamekuzingua wapeleekee gharika, wamekuzingua waue uzaliwa wao wa kwanza, halafu kuna kimalaika upande wa pili kinakwambia mpende jirani yako km unavyojipenda akikupiga shavu la kulia mgeuzie la kushoto akuongezee lingine, akichukua koti lako mpe na shati pia

Sasa hicho kishetani na hicho kimalaika ndivyo vinavyokuwakilisha wewe, sasa hivi mashetani wameumbiwa majehana na kuzimu za duniani ukiua unapelekwa mahakamani baadae ya kesi unapelekwa kuzimu au jehanamu ukamuone shetani anavyoishi ishi hapa duniani, hio ndio kuzimu

Askofu anaenda mbali anasema hakuna tofauti ya mbinguni na duniani, hapo hapo ulipo ndio mbinguni hapohapo ulipo ndio duniani, wewe ni Mungu Mdogo kwenye umbo la mwili ila huna unachoweza kumzidi Mungu Mkuu

Askofu akaishia hapo
Huu upotoshaji tunataka clarity.
 
Back
Top Bottom