TABORA: Wafanyakazi 11 wa TRL mbaroni kwa ufisadi wa dizeli ya kuendeshea treni

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
tabora%284%29.jpg


Watumishi kumi na moja wa shirika la Reli nchini (TRL) wa karakana ya Tabora wanashikiriwa na Jeshi la Polisi kupisha uchunguzi wa kina, katika kile kilichodaiwa kuwa,ni kuhusika katika kuhujumu shirika kwa kuuza mafuta ya Dizel ya kuendeshea Treni.

Akizungumza na ITV katika ofisi za shirika hilo mjini Tabora Kaimu Mhandisi wilaya Tabora Mhandisi,Edgar Bakuza amesema,baada ya kufanya ukaguzi wa kushtukiza walibaini kuwepo na wizi mkubwa wa mafuta,na kukamata lita ishirini na madumu zaidi yaliyokuwa yamefichwa kwa ajili ya kupatia tena.

Aidha amesema kuwa,wilaya ya Tabora yenye njia za reli za Mwanza, Kigoma na Mpanda imekuwa ikikabiliwa na changamoto ya wizi wa mafuta aina ya Dizel ka kusababisha utendaji kuwa duni huku treini za mizigo na abiria kulazimika kusimama njiani,na kukamatwa kwao kutakuwa fundisho.

Wakizungumzia changamoto inayoikabili karakana hiyo ya Tabora, baadhi ya wafanyakazi wamesema kuwa,eneo la karakana halina uzio hali ambayo imekuwa akiwapa wakati mgumu,kuwadhibiti waarifu,hoja iliyopingwa na mhandisi akidai hoja kubwa ni waadilifu na sio uzio.
 
Sasa kama hawajalipwa mishahara wataishije?
unajua mpaka shirika limefikia hatua hiyo ni nani wa kulaumiwa?
Wizi wa mizigo
Mafuta
halafu bado unatetea wizi, unategemea vipi watalipwa mshahara wakati pesa inayotakiwa kununulia mafuta haizalishi inavyotakiwa lazima tuwe wakweli ni sisi wenyewe tunawajibika na kuua mashirika yetu wenyewe halafu tunalaumu serikali kubinafsisha
 
Duh wizi mkubwa!!!!!!! Litre 20 za diesel sawa na sh 32,000!!!!!!!!! si wangesema wizi wa kawaida, sasa na haya majizi/ mafisadi wizi wao tuuitaje????
 
Wafanyakazi wamekata tamaa wanapoona mafisadi ya escrow yanachota hela kwa kutumbua visalfeti na viroba bila kukamatwa na kuchukuliwa hatua
 
Back
Top Bottom