The redemeer
JF-Expert Member
- Jan 28, 2025
- 4,780
- 8,155
Moja ya tabia ya watu waliofanikiwa ni watu wasiopenda kabisa kupewa vitu vya bure.Free lunch,free sijui nini nk
Ukitaka kuwakosa watu waliofanikiwa kwenye jambo lako wambie tu kuwa ni buree kamwe hutawaona kabisaa.
Na ukitaka kujua kuwa na wewe umekua na unaingia kwenye list ya watu waliofanikiwa utaanza kuchukia kulipiwa au kupewa vitu vya bure ambavyo hujavifanyia kazi.
Hata ikitokea mmetoka out na watu hata kama kuna mtu unaona ana uwezo wa kulipa Bill utakataa na kutaka kulipa walau kushare gharama iliyo tumika hata kama ni kulipia tu vinywaji.
Na hata ikitokea umealikwa sherehe na unajua kuwa kila kitu kipo na kimelipiwa walau unabeba zawadi kuwapa wale waliokualika walau ushiriki kwa namna moja ama nyingine.
Kumbuka hawa watu waliofanikiwa hawataki kabisa kupewa bure kitu,maana wanaamini kuwa cha kupewa bure hakina thamani.
Watu waliofanikiwa huamini kutoa kuliko kupokea.
Kwao, kutoa ndiyo njia ya kuongeza, si kupokea.
Na zaidi, wanathamini kile walichokitolea jasho, si walichopewa bure.
Wewe je? Uko kundi lipi?
Umeanza kuchukia "vya bure bure"? Basi karibu kwenye familia ya watu waliofanikiwa.
Unaweza kubadili mtazamo wako na Unaweza kuwa mmoja wa watu waliofanikiwa .
Mfalme Daudi alikataa kupewa vya bure
Esau alikataa kupewa vya bure na ndugu yake Yakobo. Ibrahimu alikataa kupewa ardhi bure kwaajili ya kumzikia mke wake Sara bali aliinunua (Mwanzo 23:17-18)
Ibrahimu Aliikataa zawadi ya bure kutoka kwa mfalme wa Sodoma (Mwanzo 14:23)
Daudi alikataa kumpa Mungu sadaka ya bure.
Wakati Daudi aliponunua kiwanja cha Arauna ili kumtolea Mungu sadaka (baada ya pigo kwa Israeli), Arauna alitaka kumpa kiwanja na sadaka bure. Lakini Daudi alikataa.
Lakini mfalme akamwambia Arauna, La! lakini nitakinunua kwako kwa thamani yake; maana sitamtolea Bwana, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa nisizozilipia gharama.”( 2 Samweli 24:24)
Ikawe amani,kibali na utoshelevu kwako
Bure ina gharama kubwa kwako kiroho.Toa ili upokee,kubali kulipia gharama ili ukue.
Ukitaka kuwakosa watu waliofanikiwa kwenye jambo lako wambie tu kuwa ni buree kamwe hutawaona kabisaa.
Na ukitaka kujua kuwa na wewe umekua na unaingia kwenye list ya watu waliofanikiwa utaanza kuchukia kulipiwa au kupewa vitu vya bure ambavyo hujavifanyia kazi.
Hata ikitokea mmetoka out na watu hata kama kuna mtu unaona ana uwezo wa kulipa Bill utakataa na kutaka kulipa walau kushare gharama iliyo tumika hata kama ni kulipia tu vinywaji.
Na hata ikitokea umealikwa sherehe na unajua kuwa kila kitu kipo na kimelipiwa walau unabeba zawadi kuwapa wale waliokualika walau ushiriki kwa namna moja ama nyingine.
Kumbuka hawa watu waliofanikiwa hawataki kabisa kupewa bure kitu,maana wanaamini kuwa cha kupewa bure hakina thamani.
Watu waliofanikiwa huamini kutoa kuliko kupokea.
Kwao, kutoa ndiyo njia ya kuongeza, si kupokea.
Na zaidi, wanathamini kile walichokitolea jasho, si walichopewa bure.
Wewe je? Uko kundi lipi?
Umeanza kuchukia "vya bure bure"? Basi karibu kwenye familia ya watu waliofanikiwa.
Unaweza kubadili mtazamo wako na Unaweza kuwa mmoja wa watu waliofanikiwa .
Mfalme Daudi alikataa kupewa vya bure
Esau alikataa kupewa vya bure na ndugu yake Yakobo. Ibrahimu alikataa kupewa ardhi bure kwaajili ya kumzikia mke wake Sara bali aliinunua (Mwanzo 23:17-18)
Ibrahimu Aliikataa zawadi ya bure kutoka kwa mfalme wa Sodoma (Mwanzo 14:23)
Daudi alikataa kumpa Mungu sadaka ya bure.
Wakati Daudi aliponunua kiwanja cha Arauna ili kumtolea Mungu sadaka (baada ya pigo kwa Israeli), Arauna alitaka kumpa kiwanja na sadaka bure. Lakini Daudi alikataa.
Lakini mfalme akamwambia Arauna, La! lakini nitakinunua kwako kwa thamani yake; maana sitamtolea Bwana, Mungu wangu, sadaka za kuteketezwa nisizozilipia gharama.”( 2 Samweli 24:24)
Ikawe amani,kibali na utoshelevu kwako
Bure ina gharama kubwa kwako kiroho.Toa ili upokee,kubali kulipia gharama ili ukue.