Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,813
- 11,991
*SAMAKIBA KUSHIRIKIANA NA DORIS MOLLEL FOUNDATION KUWEKEZA KWA WATOTO NJITI
Taasisi ya Doris Mollel Foundation kwa kushirikiana na Samakiba Foundation (@samakibafoundation )wamezindua kampeni ya mechi ya hisani iendayo kwa jina la Nifuate na Upendo wa Zambarau 2023. Mechi hii ya hisani bkwa mwaka huu itafanyika mnamo tarehe 17 Juni 2023 katika kiwanja cha Azam Complex kilichopo Mbagala Chamazi ambayo imelenga kutoa msaada wa vifaa tiba katika hospitali zilizopo Kibiti na Kigoma.
Katika kuelekea mechi hio ya hisani kutakuwa na matukio mbali mbali yakiambatana na Bonanza mbili zitakazotarajiwa kufanyika mnamo tarehe 10 na 11 Juni 2023 katika viwanja vya Kariakoo na Mbagala. Ikumbukwe kuwa, Samakiba Foundation ni taasisi iliyoanzishwa mwaka 2020 na Mbwana Samatta (@samagoal77 )na Alikiba (@officialalikiba), ikiwa na lengo la kusaidia wale wanaohitaji ndani ya jamii kupitia mechi yao ya hisani iendayo kwa jina la Nifuate.
#Nifuate2023 #UpendoWaZambarau
Taasisi ya Doris Mollel Foundation kwa kushirikiana na Samakiba Foundation (@samakibafoundation )wamezindua kampeni ya mechi ya hisani iendayo kwa jina la Nifuate na Upendo wa Zambarau 2023. Mechi hii ya hisani bkwa mwaka huu itafanyika mnamo tarehe 17 Juni 2023 katika kiwanja cha Azam Complex kilichopo Mbagala Chamazi ambayo imelenga kutoa msaada wa vifaa tiba katika hospitali zilizopo Kibiti na Kigoma.
Katika kuelekea mechi hio ya hisani kutakuwa na matukio mbali mbali yakiambatana na Bonanza mbili zitakazotarajiwa kufanyika mnamo tarehe 10 na 11 Juni 2023 katika viwanja vya Kariakoo na Mbagala. Ikumbukwe kuwa, Samakiba Foundation ni taasisi iliyoanzishwa mwaka 2020 na Mbwana Samatta (@samagoal77 )na Alikiba (@officialalikiba), ikiwa na lengo la kusaidia wale wanaohitaji ndani ya jamii kupitia mechi yao ya hisani iendayo kwa jina la Nifuate.
#Nifuate2023 #UpendoWaZambarau