TataMadiba
JF-Expert Member
- Feb 7, 2014
- 9,868
- 5,753
UTAFITI wa Taasisi ya Tanzania Development Initiative Programme(TADIP) uliomtaja Edward Lowassa kuongoza dhidi ya Dk John Magufuli katika kinyang'anyiro cha urais umegubikwa na utata ikibainika taasisi hiyo ni mali ya CHADEMA. Katika utafiti huo uliotangazwa na taasisi hiyo septemba 25, 2015, jijini Dar es Salaam , Lowassa alipewa alama za ushindi kwa asilimia 54.5 na Dk. Magufuli asilimia 40.
Baada ya matokeo ya utafiti wao huo, uchunguzi uliofanywa na gazeti la Raia Tanzania umebaini kwamba taasisi hiyo ya TADIP ni mali ya CHADEMA iliyoanzishwa mwaka 2006, ikifanya kazi maalumu ya kwa maelekezo ya chama hicho ambacho kwa sasa ndicho chama kikuu cha upinzani.
Uchunguzi zaidi umebaini kwamba taasisi hiyo ndani ya CHADEMA , Mkurugenzi wake wa kwanza ni aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, ZUBERI ZITTO.
Mbali na uchunguzi wa Raia Tanzania, maelezo mengine yaliolifikia gazeti hilo yanadai kwamba, TADIP ilichukua hatua ya dharura kutangaza utafiti huo ili kukabili ule wa taasisi mbili za TWAWEZA na SYNOVATE, ambazo zilionesha Lowassa kusidi kuelemewa na kupoteza umaarufu.
Kati ya mei na Juni , mwaka huu, TADIP ikifanya kazi za chama (CHADEMA) iliendesha utafiti kujua kati ya aliyekuwa mgombea wake mtarajiwa , Dk. Wilbrod Slaa na wagombea wengine waliokuwa wakitajwa , akiwemo Edward Lowassa akiwa ndani ya CCM, nani zaidi. Barua ya Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TADIP ya julai 26, 2015, George Shumbusho, iliyoandikwa kwenda kwa Katibu Mkuu wa Chadema, ilibainisha kuwa utafiti huo uliofanywa katika mikoa minne ya Tanzania bara ulimpa nafasi kubwa Dk. Slaa dhidi ya wanasiasa wa CCM, akiwemo Lowassa.
Pichani(kushoto) ni George Shumbusho akitangaza matokeo ya Utafiti wa TADIP , Septemba 25 wiki iliyopita. Kulia ni Shumbusho akionesha kushabikia Chadema, picha hiyo imekuwa ikisambazwa mitandaoni na uongozi wa TADIP umeikanusha.
Source: Raia Tanzania.
Baada ya matokeo ya utafiti wao huo, uchunguzi uliofanywa na gazeti la Raia Tanzania umebaini kwamba taasisi hiyo ya TADIP ni mali ya CHADEMA iliyoanzishwa mwaka 2006, ikifanya kazi maalumu ya kwa maelekezo ya chama hicho ambacho kwa sasa ndicho chama kikuu cha upinzani.
Uchunguzi zaidi umebaini kwamba taasisi hiyo ndani ya CHADEMA , Mkurugenzi wake wa kwanza ni aliyekuwa Mbunge wa Kigoma Kaskazini na Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, ZUBERI ZITTO.
Mbali na uchunguzi wa Raia Tanzania, maelezo mengine yaliolifikia gazeti hilo yanadai kwamba, TADIP ilichukua hatua ya dharura kutangaza utafiti huo ili kukabili ule wa taasisi mbili za TWAWEZA na SYNOVATE, ambazo zilionesha Lowassa kusidi kuelemewa na kupoteza umaarufu.
Kati ya mei na Juni , mwaka huu, TADIP ikifanya kazi za chama (CHADEMA) iliendesha utafiti kujua kati ya aliyekuwa mgombea wake mtarajiwa , Dk. Wilbrod Slaa na wagombea wengine waliokuwa wakitajwa , akiwemo Edward Lowassa akiwa ndani ya CCM, nani zaidi. Barua ya Kaimu Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa TADIP ya julai 26, 2015, George Shumbusho, iliyoandikwa kwenda kwa Katibu Mkuu wa Chadema, ilibainisha kuwa utafiti huo uliofanywa katika mikoa minne ya Tanzania bara ulimpa nafasi kubwa Dk. Slaa dhidi ya wanasiasa wa CCM, akiwemo Lowassa.
Pichani(kushoto) ni George Shumbusho akitangaza matokeo ya Utafiti wa TADIP , Septemba 25 wiki iliyopita. Kulia ni Shumbusho akionesha kushabikia Chadema, picha hiyo imekuwa ikisambazwa mitandaoni na uongozi wa TADIP umeikanusha.
Source: Raia Tanzania.