Taarifa ya serikali mlipuko wa Arusha

mathabane

JF-Expert Member
Jan 27, 2013
2,406
1,891
Nmefanikiwa kusikiliza taarifa ya serikari juu ya tukio la mlipuko wa bomu kwenye mkutano wa chadema iliyosomwa na Lukuvi. Bado inanipa shida juu ya taaluma, ujuzi na umakini pia weledi wa maofisa wa serikari ku-deal na ku-handle masuala na changamoto kubwa za kitaifa. In short, taarifa imeelekeza lawama kwa cdm badala ya kukemea uzembe wa wanausalama.
 
wanaongea upuuzi tu hakuna hata critical thinking waliofanya. kuongozwa na maccm ni kuipeleka nchi kwenye janga.
 
Nchi ina utajiri wa kila nama kasoro viongozi tu. Hili genge la wahuni limetuharibia jina la nchi yetu kupita kiasi. Tanzania will never be the same. Shame on you Lukuvi and the rest of the so called government leaders. We truly don't have any for now!
 
siku zote mwizi hajisemi kua ni.humsingizia mwenzie kua labda atakua fulan huu ni mchezo mchafu wa ccm kutaka kuusambaratisha upinzani mlianza kwa TLP.CUFna sasa kwa cdm kwa sasa.ccm mmefika mwisho watanzania wamejua ubaya wenu
 
Inasikitisha lakini tuseme nini wakati wenyewe sio wakweli katika nafsi zao. Wanalindana, walisema wanajivua magamba hadi leo kimya, kwa hali hiyo wanajihusisha na mbinu chafu. Bahati mbaya wamechelewa watz wameamka na wanajua haki zao na wanajua nani mkweli nani mbabaishaji. Ya arusha ndio kwanza yanawachafua zaidi. Alamsiki tuonane 2015 kama sio mapema zaidi.
 
Back
Top Bottom