SIMBA mtoto
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 204
- 100
TAARIFA KWA UMMA
KUKOSEKANA HUDUMAYA MAJI KWA SIKU MBILI JIJINI DAR
Dawasco inawatangazia wakazi wote wa jiji la Dar es salaam na Mji wa Bagamoyo kuwa mtambo
wa kuzalisha Maji wa Ruvu Chini utazimwa kwa wastani wa saa 48 kwa siku za Ijumaa na Jumamosi
ya tarehe 23 na 24 Januari 2015, kuanzia saa kumi na mbili asubuhi, ili kuruhusu mkandarasi
(Sino-hydro Corporation ltd) kuunganisha bomba la zamani na bomba jipya
(Cross-connection) ndani ya Mtambo wa Ruvu Chini , Bagamoyo.
Kuzimwa kwa mtambo wa Ruvu Chini kutasababisha maeneo yafuatayo kukosa Maji; Mji wa Bagamoyo, Mapinga, Bunju, Boko, Tegeta, Kunduchi, Salasala, Jangwani, Mbezi beach na Kawe.
Maeneo mengine ni Mlalakuwa, Mwenge, Mikocheni, Msasani, Sinza,Manzese, Mabibo, Kijitonyama,
Kinondoni, Oysterbay, Magomeni, Upanga, Kariakoo, City Centre, Ilala, Ubungo Maziwa, Kigogo, Mburahati,
Hospitali ya rufaa Muhimbili (MNH), Buguruni, Changombe na Keko.
Wananchi mnashauriwa kuhifadhi maji ya kutosha na kuyatumia kwa matumizi ya lazima.
Au wasiliana na kituo cha huduma kwa wateja namba 022-2194800
Dawasco inaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
Imetolewa na ofisi ya uhusiano,Dawasco
-
Makao Makuu
.
KUKOSEKANA HUDUMAYA MAJI KWA SIKU MBILI JIJINI DAR
Dawasco inawatangazia wakazi wote wa jiji la Dar es salaam na Mji wa Bagamoyo kuwa mtambo
wa kuzalisha Maji wa Ruvu Chini utazimwa kwa wastani wa saa 48 kwa siku za Ijumaa na Jumamosi
ya tarehe 23 na 24 Januari 2015, kuanzia saa kumi na mbili asubuhi, ili kuruhusu mkandarasi
(Sino-hydro Corporation ltd) kuunganisha bomba la zamani na bomba jipya
(Cross-connection) ndani ya Mtambo wa Ruvu Chini , Bagamoyo.
Kuzimwa kwa mtambo wa Ruvu Chini kutasababisha maeneo yafuatayo kukosa Maji; Mji wa Bagamoyo, Mapinga, Bunju, Boko, Tegeta, Kunduchi, Salasala, Jangwani, Mbezi beach na Kawe.
Maeneo mengine ni Mlalakuwa, Mwenge, Mikocheni, Msasani, Sinza,Manzese, Mabibo, Kijitonyama,
Kinondoni, Oysterbay, Magomeni, Upanga, Kariakoo, City Centre, Ilala, Ubungo Maziwa, Kigogo, Mburahati,
Hospitali ya rufaa Muhimbili (MNH), Buguruni, Changombe na Keko.
Wananchi mnashauriwa kuhifadhi maji ya kutosha na kuyatumia kwa matumizi ya lazima.
Au wasiliana na kituo cha huduma kwa wateja namba 022-2194800
Dawasco inaomba radhi kwa usumbufu wowote utakaojitokeza.
Imetolewa na ofisi ya uhusiano,Dawasco
-
Makao Makuu
.