Taarifa iliyotolewa na TBC kuwa madaktari wa bugando wamesitisha mgomo kwa kile walichokiita kuchoka kuburuzwa si za kweli, ni propaganda ya watu fulani kwa lengo la kujisafisha na kuupotosha umma wa watanzania.
Madaktari hawafanyi propaganda wana madai ya msingi ambayo wanayasimamia, na mgomo bugando upo.
Kilichotokea ni kwamba, kuna wajinga fulani walibandika kijitangazo usiku wa manane kuwa eti hawataki kuburuzwa na wakajiita G25, nadhani walikuwa wanakumbushia ile ya wabunge waliojiita G55 enzi nzileee. sasa wakati kinajadiliwa hicho kijiujumbe asubuhi kumbe waandishi wameitwa na kupewa kuwa ndo news ya kuripoti hiyo.
Hakuna hata mtu mmoja aliyejitokeza kuhusika na kijitangazo hicho. Ni upuuzi wa hali ya juu.
Viongozi waongo ndo wataiangusha hii serikali maana wataipotosha nayo itapotoka na kuchukua maamuzi mabovu na mwisho mpotoko huo unaweza kuzaa mengine
Chanzo cha habari ni mimi mweneywe, nipo bugando
Madaktari hawafanyi propaganda wana madai ya msingi ambayo wanayasimamia, na mgomo bugando upo.
Kilichotokea ni kwamba, kuna wajinga fulani walibandika kijitangazo usiku wa manane kuwa eti hawataki kuburuzwa na wakajiita G25, nadhani walikuwa wanakumbushia ile ya wabunge waliojiita G55 enzi nzileee. sasa wakati kinajadiliwa hicho kijiujumbe asubuhi kumbe waandishi wameitwa na kupewa kuwa ndo news ya kuripoti hiyo.
Hakuna hata mtu mmoja aliyejitokeza kuhusika na kijitangazo hicho. Ni upuuzi wa hali ya juu.
Viongozi waongo ndo wataiangusha hii serikali maana wataipotosha nayo itapotoka na kuchukua maamuzi mabovu na mwisho mpotoko huo unaweza kuzaa mengine
Chanzo cha habari ni mimi mweneywe, nipo bugando