Symbion Power: Intelligence watupu

Tutapata umeme wa saloon na wa bulb za majumbani tu, umeme mkubwa wa kuweza kutumika viwandani itakuwa ni ndoto.

Hiyo ndio kazi ya CIA kuzifanya nchi zenye maskini wa kutengenezwa kubaki katika hali ya umaskini milele.

Wanajua wazi kabisa umeme ndio kiini cha mapinduzi ya viwanda na ili waafrica tuendelee kuuza bidhaa ghafi kwenda kwao lazima wahakikishe hatuna viwanda na dawa yake ni kucontrol sector ya umeme ili tupate umeme kwa kiwango wanachotaka wao no matter kama una uranium, makaa ya mawe au mito mingi.

Hiki ndicho kitu kinafanyika Iraq kwani pamoja na utajili wa mafuta bado nchi ina mgao wa umeme. Kuna thread ilishawahi anzishwa hapa kuwa Rostam ni agent wa CIA lakini watu waliipuuza tu, ni bora tuanze kuunganisha dot sasa, pamoja na majaribio ya kuuwawa Dr. Mwakyembe na issue za Richmond.

Mpaka kesho kutwa mtu mweupe hayuko tayari kuna bara la Africa linakuwa kiuchumi kwani ndio utakuwa mwisho wa constructed "white suprimacy". Napata wasiwasi na Balozi wetu aliyeko DC kama si agent basi atakuwa hajui analolifanya.
 
Tunachotaka ni balbu kuwaka, wawe intellijensia au sijui nani, lakini balbu zikiwaka si zimewaka?......

Tatizo lipo kwenye elimu, waache wenye jicho la tatu waisaidie Nchi yetu,wewe hujui chochote tulia. SIYO KILA UKIONACHO NI DHAHABU! hawa wawekezaji wengine wana mambo yao.vilaza wengi hawawezi kujua.
 

Baadae ili backfire maana walikuwa wamemchomea huyo mama kama agent serikali ikaingia matatani kwa kuhatarisha usalama wake.
 
Let them do the job, kule kwa wenzetu watu wenye background za Military wanaheshimika sana na wanafahamika sana kwa kupiga kazi. Huku kwetu lakini ni tofauti kidogo sijui kama wakina Mboma wanaweza kupewa hizi sifa.
 
Tutaisoma namba. Hivi ile tuzo ya dowans kwa ajili ya mapacha watatu kikwete,lowasa na rostamu wameshalipwa?
 

I agree with u fully, pia documentaries za Zeitgeist kaongelea sna huu mwenendo wa Marekani kuteka dunia na ukigoma wanakumaliza...

Sasa hvi naenda maeneo ya SAMORA kukisaka hcho kitab...... thx
 
Kwa nini wastaafu wetu hawaingii kwenye fani kama hizi na wao?

huko wanaingia wenye fani zao. Sio kama hawa wa kwetu failures au vibaka walioshindikana mtaani ndo wanapelekwa jeshini. Aut of it hana utaalamu mwingine wowote wa kumsaidia kuishi.
 

Yep,ndo huyo huyo mkuu,how have you been?
 
NJOZI
Ni kweli Marekani na Asasi yake ya Kijasusi wana nguvu za kiuchumi, kijasusi na hata kiteknolojia na kwamba pamoja na kusudio la kuhakikisha kuwa Marekani inakuwa nchi yenye maendeleo kwa watu wake, bado agenda ya njozi ya kutaka nchi yao iendelee kuwa ‘kiongozi na askari wa dunia' inawasumbua baadhi ya Wamarekani. Hata inapokuja kwenye kumtafuta nani awe Rais wao, huwa wanapenda kuwauliza wagombea hilo swali la hiyo njozi ingawa kwa namna tofauti tofauti.

HALI HALISI
Pamoja na nguvu na njozi zao, ni imani yangu kuwa nchi nyingine kama za kwetu pamoja na kuonekana ‘wadogo' kwa mataifa hayo ‘makubwa', si kweli kuwa hatuna kabisa sauti juu ya mambo kama haya ya UBADHILIFU wa wazi, maana watu wamekuwa na ulewa mkubwa na haki za binadamu zinatetewa kila mahala hata ndani yanchi ‘zilizoendelea' ambako kuna wananchi wengi sana (nguvu ya umma) ambao hawataki kuona Mataifa yao yajulikane kwa uovu na kuchukiwa na mengine kutokana na uonevu au wizi. Sote tunakumbuka hata suala la RADA likivyoanza kupigiwa kelele Uingereza, kabla ya sisi wenyewe hatujafikia kiasi hicho!

Hata wao si wajinga; wakikumbana na msimamo mkali unatoka kwa mtu mmoja (hata awe Rais au Waziri) au kikundi cha wachache tu basi wanapata nguvu ya kuwashawishi wengine wengi wanaobaki na hakika mwisho wa siku misimamo kama hiyo lazima ishindwe (at least in that material time); lakini wanapogundua kuwa Rais au Waziri anamsimamo mkali na mihimili yote ya dola inamuunga mkono plus wananchi (walio wengi), amini kuwa hakuna cha shirika la kijasusi wala nini hata wao hurudisha siraha nyuma wakiomba dua kusubiria upepo ubadilike!


HATUA:
Kwa vile suala la uzalishaji wa umeme wa nyongeza wa haya majenereta ya Syimbion na mikataba ya huko nyuma toka Richmond haina tija na inatia hasara TANESCO & Taifa letu kwa ujumla waziwazi, nashauri Katibu na Waziri mwenye dhamana kuwapa kazi watathmini wazawa wenye ujuzi na maadili toka hata UDSM & IFM to undertake a in-depth technical & financial appraisal kisha Waziri awasilishe kauli yake kwenye Baraza la Mawaziri na kisha Bungeni juu ya matokeo ya hiyo tathmnini na mapendekezo ya maamuzi magumu ya kuiokoa TANESCO kutokana na makucha ya haya makampuni, mikataba mibovu pia kesi ile kesi isioisha inayosimamiwa na Mh. Mkono & Advocates; halafu wananchi tuone ni nani anayepinga ambaye yuko upande wa hayo makampuni! Kwa kufanya hivi itabidi waamuwe kutupa a fair deal au waondoke, tununue majereta yetu wenyewe! Muda wa kututisha- a sovereign state na kulia lia sasa umekwisha. Kuwekewa vikwazo vya kiuchumi si lazima itangazwe UN, inawezwa kutangazwa kupitia mikataba mibovu, na kampuni kutuwekea mikwara tena ndani ya mipaka ya nchi yetu kwa kutunyima umeme na au kutuuzia kwa bei mbaya na kwa kutafuta support toka kwa wachumia-tumbo wachache wanaofikiri kuwa wanaweza kuwashawishi Wabunge wote kukubaliana na upuuzi huu!

Chukueni hatua sasa!
 
mbona hao wacia wapo kila pahala ! wewe unasemea simbion?
mpaka huko ikulu wana sources zao
 
Nyie si mnatuma mabalozi waimba taarabu tuu.Hamjui hata ni nchi gani amnapeleka nani kama mnavyowapa wizara mawaziri hovyo mkidai ni wazoefu.

hata uchina wana machinga wenye nishani za kutukuta kaktika mitaa yetu.Huoni wanavyowaadhibu wabongo wakitaka iba palipo maficho yao yaliyopo katik maghala?Na miwshowe hakuna wanachofanywa baada ya mkwara wa nchi zao?

Watu wanajua wafanyahco na hakuna optiona wanayoicha wala kubishana itumia.Ukisikia wakisema all options are on the table ujue wanamaanisha hivyo.Sasa walete nania wakati tayarai dunia imerdui katk mazingira kama ya mkutano wa berlini wa kugawa dunia..China mpaka kaamua samehe deni la tazara tazara na kuitengeza tena upya, US mmepiga kelele wasiweke base kwa dhaifu, Canada wanampigisha misele dhaifu na kusaini mikataba ya kuilinda canada, Ujerumani wanafadhili kila kitu kuanzia afya maji, baabara, siasa za vyama vyote ili wakikosa kimoja wapate kingine, Iran tayari anacheza na Zenj na bara kw akuwaletea mdaktari, waingereza wakwatete uongo rada, Walio na laoliondo wapo busy watumia walalamikaji, wakenya nao wameshajijua nao wanajituma tuweka ktk mstari.
 

pata hichi kitabu:

 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…