Sweet, Sticky and Spicy Chicken

Pilipilihoho

JF-Expert Member
Jan 29, 2016
202
145
Mahitaji
  • Kuku nusu kilo
  • Asali vijiko 4
  • Sukari ya brown kijiko 1 na nusu
  • Soy sauce nusu kikombe ,hii ni sawa na vijiko 8 vya mezani
  • Tangawizi vijiko 2 vya chai
  • Kitunguu saumu vijiko 2 vya chai
  • Chilli sauce vijiko 3 vya mezani
  • Chumvi kiasi
  • Cayenne pepper kiasi
  • Mafuta ya olive vijiko 5 vya chakula
  • Currypowder kijiko 1 cha chai
  • Coriander powder kijiko 1 cha chai
  • Ndimu 1
Maelekezo
Changanya pamoja sukari, asali, soy sauce, tangawizi, kitunguu saumu na chilli sauce kwenye kibakuli kidogo.
Safisha kuku, mkaushe maji, mkate vipande vidogo vidogo muweke kwenye kikaangio, mnyunyizie chumvi, cayenne pepper na ndimu kiasi.
Weka mafuta jikoni kisha weka kuku na anza kumgeuza gueze kuku mpaka mafuta yapate moto, usiache kugeuza mpaka kuku awe wa brown.
Weka viungo vilivyobaki currypowder na coriander powder, koroga kwa dakika 5.
Mwisho mwagia sauce uliyoandaa, usifunike. Pika hadi sauce iwe nzito.
Epua nyama ya kuku na jirambe na familia.
 
Sijapika nina muda mrefu sasa,
Ngoja wikiendi nijaribu kupika hii kitu mwenyewe.
Nikishindwa kalagabao.
 
Mimi kuku kumtia Sukari, nahisi kama hatokuwa mtamu.maybe I'm wrong.nimeshazoea kuku sio wa sukari.maybe nikionja ni mtamu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom