Kujua raisi wa TFF ajae ni rahisi, kwani kuna washindani wawili tu (kwa mujibu wa vyanzo mbali mbali) ambao ni Jamal Malinzi na Nyamlani. Kiuhalisia wako watatu lakini huyo mmoja (nimemsahau jina) anaonekana ni msindikizaji kwa sababu hajui FITNA ZA MPIRA. Ninasikitika sana kuona tunaelekea Enzi za FAT. kwa sababu hao wote hawana jipya, wanaendekeza fitna na kugawa wanachana. Walikuwa busy sana kisimika watu wao wakati wa uchaguzi wa mikoani, wamemwaga fedha nyingi sana (siwezi kuwa na ushahidi wa kimahakama) ili kuweka watu wao ambao baada ya kuchaguliwa kwenye urais wawe wanawatumikia na sio kutumikia TFF. nasikitika.