threat unazoongelea hapa ni mhusika mwenyewe dhidi ya mahasimu wake rejea kuwa mawazo alikuwa ccm hivyo anawajua weakness zao anapopanda jukwaani anamwaga sumu ya kutosha hivi upande mmoja kukosa raha hivyo ukiangalia kwa juu juu utaona weakness za upande mmoja ndio zilizaa threat hii ambayo haipo kwa sasa hivo kuleta strength upande mwingine
kama ndo wanasheria tulionao mnaandika hivi, I'm sure tuna safari ndefu ya kufika nchi ya ahadi!!!
Lowasa ni Rais mtake msitake, hata Magufuli anajua hilo
Lowasa ni Rais mtake msitake, hata Magufuli anajua hilo
Amani ya Bwana iwe nanyi wadau,
Kwanza kabisa napenda kuanza kutoa pole kwa wale wote walioguswa na kifo na ndugu Alphonce Mawazo. Kifo chochote sio jambo la kawaida kwa hiyo hata iweje lazima pole itolewe hasa kwa wale walioguswa kwa dhati na kifo hiki.
Nikiwa natafakari kifo hiki kumekuwa na maneno mbalimbali yamekuwa yakiendelea humu mitandaaoni kwa watu kurushiana maneno hasa wakihusishana na kifo hiki. Watu hawa kwa kifupi ni wafuasi wa CHADEMA wakisema kuwa CCM wanahusika na kifo hiko, wengine wanadai kuwa ni polisi na huyu si mwingine bali ni mgombea ubunge wa jimbo la Arusha mjini ambaye ameenda mbali zaidi hadi kuwataja polisi kuwa wanahusika na kifo hicho.
Nikiwa mwanasheria na mdau wa mambo ya kisheria hapa napenda nishirikiane na wenzangu jambo hili, nalo ni kama nilivyoandika kwenye kichwa cha thread husika kuwa CCM WAMUUE MAWAZO KWA SABABU ZIPI HASA?
Hili swali linaweza kuonekana la ajabu kwa watu ambao sio critical thinkers ila kwa critical thinkers ni swali la msingi na la muhimu sana kwa sababu hata upande kwa upelelezi unapoanza kuchunguza tukio ili kumuhusisha mtuhumiwa na mauaji kwanza wanaanzaga kuangalia MOTIVE YAANI KWA LUGHA NYINGINE INTENTION.
Kwa wale msioelewa maana ya motive ni nia au dhamira ya mtenda kosa. Sasa kwenye hili tukio ili kuwahusisha CCM napenda kuuliza kuwa Je kuna sababu zipi hasa kwa CCM kumuua ndugu Mawazo ili tu kuweza kutengeneza au kupata motive yao?
Sijaandika ili kuwatetea CCM ila as long as taarifa za kipelelezi hazijatoka napenda tujiulize kwa pamoja kuna sababu gani za msingi kwa CCM kama chama kupanga au kutekeleza mauaji ya ndugu Mawazo?
Nimefikiria sana hata sijaweza pata hata moja kwa sababu hata kwa Geita mawazo hakuwa threat kwa chama kwa kusema kuwa hali ya upinzani kwenye uchaguzi huu kwa Geita imeonyesha kuwa haikuwa nzuri yaani hata ushawishi wao haujaonekana kwa sababu robo tatu ya mkoa tena kama sio wote kwenye uchaguzi uliomalizika imeenda CCM sasa kulikuwa na threat gani kwa CCM hadi waseme wamuue ndugu mawazo? kwa sababu ili iweze kuihusisha CCM na mauaji ya ndugu Mawazo lazima narudia ni lazima ili motive ipatikane tuweze kujiridhisha kiwango cha threat ambacho ndugu mawazo alikiweka kwa CCM. Kama hakijapatikana basi hapo hatuwezi kuihusisha CCM na mauaji ya ndugu Mawazo.
Jambo la pili ni kuhusiana na Polisi kwa sababu ndugu LEMA amejaribu kuwahusisha polisi, swali lilelile napenda kuli impose hapa Je, ndugu Mawazo alikuwa na threat gani kwa polisi hadi polisi wahusike na mauaji yake? Hadi sasa swali hili halijaweza kujibiwa popote pale.
Napenda kumaliza kwa kusema ingawa haturuhusiwi kuongelea upande negative wa marehemu ila hapa lazima tuseme kitu. Marehemu alikuwa anajulikana vizuri sana kuwa ni mtu mtata sana hasa kitabia na hulka na hata kuna thread humu ndani alizokuwa akimsema vibaya kwa vitisho ndugu Zitto Kabwe zinaonekana humu ndani. Naomba tusiondoe nadharia hii kwenye kifo cha marehemu kuwa inawezekana marehemu alikuwa kwenye ugomvi na wauaji wake na kwenye huo ugomvi ndo yakatokea yaliyotokea. Na pia inawezekana yeye ndo alikuwa mgomvi kwa sababau hadi sasa hivi hatujaweza kuelezwa kuwa marehemu alikuwa na nani na kitu gani kilitokea hadi kusababisha mauti yake.
MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATANZANIA.
watu wa geita wapi! wale ni vijana wenu mliokaa mkawalisha maneno wa lopoke hovyo hovyo kwa faida za kisiasa, kila jambo likitokea kosa lenu kubwa ni kufanya mtaji wakisiasa angalia tukio la bomu la arusha mkajifanya mnaushaidi mwisho wa siku hadi leo hakuna kilichofanyika