serikali tatu ni mhimili na msingi wa rasimu.. Bunge halina mamlaka ya kuondoa isipokuwa wananchi.. Bunge linatakiwa tu kujadili hizo serikali tatu ziwe za namna gani basiiiiiii.... Na syo serikali mbili.. Ambyo ni maoni ya baadhi ya viongozi wa ccm
Mkulima hahitaji serikali tatu anachotaka ni serikali moja itakayompa uhuru wa kumiliki ardhi na kulima popote na kuuza popote
Mfanyabiashara anachotaka ni serikali moja yenye sheria za biashara na kodi za aina moja na taratibu za aina moja zinazomwezesha kufanya biashara popote bila bughudha ya aina yoyote
Mfanyakazi angependa kuwe na serikali moja ambapo yuko huru kufanya kazi popote na kwa viwango sawia vya mishahara na marupurupu
Mvuvi angependa serikali moja inayomwezesha kuvua popote na kujiuzia popote
Kiongozi wa dini angependa serikali moja yenye sheria moja ambayo inamwezesha yeye kutangaza dini yake na kuabudisha popote bila vikwazo
Mwanafunzi angependa awe huru kusoma popote na kupata mkopo wa kusoma popote
Lakini wanasiasa ndio wanataka serikali tatu ili wawe na nyimbo zao,majeshi yao,balozi zao,na vyeo vyao vya kisiasa na mafungu yao ya kugawana mapato yatokanayo na kukamua kodi wanyonge
Wakili wa kujitegemea angependa serikali moja ya kumwezesha kufanya kazi zake popote bila vikwazo ndani ya nchi moja.
Mfugaji wa kuhama hama angependa serikali moja inayoruhusu yeye kujichungia mifugo yake popote penye malisho mazuri ya mifugo yake
Hivi hiyo tume ya Warioba ina uhakika kuwa wananchi ndio wanataka serikali tatu?
Mimi baada ya kuwahoji wanachi wa kawaida wengi wameruka kuwa hilo la serikali tatu anayelijua vizuri ni huyo warioba na tume yake na hao wanasiasa wa UKAWA.
Wataka serikali tatu wanaotoa hadi mapovu ni wanasiasa ambao wanaishi kwa kutegemea siasa tu na wanaofaidika na ulaji kodi za wananchi ila wanajaribu kutumia wananchi kama ngao ya ubaradhuli wao.
Chadema na CUF wanajua kuwa si rahisi wao kushika nchi ikiwa moja kwa sababu CUF ina nguvu sana Zanzibar lakini bara haina nguvu hivyo nchi ikiwa moja wanajua hawatapata kura bara na CHADEMA wanaona kukiwa na serikali moja watakwama kwa kuwa wana nguvu sana Tanzania bara lakini Zanzibar hawana nguvu hivyo kukitokea uchaguzi kukiwa na serikali moja wanajua watakwama. Hivyo makundi haya mawili ya CUF na CHADEMA yanapigania serikali tatu kwa kuota ndoto za Alnacha kuwa zikipatikana basi CUF itashika Zanzibar CHADEMA tashika BARA na CCM itaambulia hako kaserikali ka muungano kasikokuwa na NGUVU wala raslimali bali kanategemea michango ya washirika.
Ukweli ndio huo wanasiasa ndio wanataka serikali tatu na warioba akaona muhimu kuwasikiliza hao na akayaita eti ndio maoni ya wananchi sio kweli.
Katika vitu vya aibu ambavyo tume imefanya ni kuchukua maoni ya wanasiasa kuhusu serikali tatu na kuyaita maoni ya wananchi .Ni aibu kwa tume. Najisikia vibaya tume kwa hili imekula posho ZA KODI ZA WANANCHI bure kabisa.