Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,162
- 162,590
Nimeangali taarifa ya habari ya baadhi ya vituo vya Television kama Channel 10 naona wameshindwa kabisa kutoa sehemu muhimu ya clip ya Lissu akimtaja muhusika wa Richmond badala yake wameikata ile sehemu muhimu inayomtaja mtuhumiwa kama Lissu alivyomtaja na badala yake wakatuonyesha sehemu isiyo muhimu ambayo Lissu aliikusudia ili kukata mzizi wa fitina.
Je,haya ndio maadili?
Kama ni maadili,maadili yanasemaje kuhusu jambo hili?
Je,mnawatendea haki watazamaji wenu?
Je,angekuwa ametuhumiwa mtu mwingine mngefanya mlivyofanya?
Hivi maadili yanayoongoza vyombo vya habari kama magazeti ni tofauti na maadili ya vyombo vya habari kama Television?
Kama hoja ni muda,sehemu ipi ya clip hiyo ilipaswa kurushwa na ipi ilipaswa kutorushwa kwa kigezo cha kulinda muda?
Kama sheria na kanuni ni zile zile,mbona magazeti yanakuwa huru kuripoti baadhi ya matukio kwa uwazi kabisa kuliko Television?
Ndugu yangu mwana-JamiiForums hapo ulipo naomba nawe useme kuhusu tv ulioangalia wameirushaje hiyo clip ya Lissu kwenye taarifa zao za habari ili tuweke mambo sawa.
Nimesoma magazeti mawili online muda huu naona nayo yamekwepa kabisa kumtaja muhusika kama hii clip iliyopo hapa JamiiForums inavyotuhabarisha.
Wameshindwa hata kumnukuu Lissu!
Hivi ingekuwa katika nchi za wenzetu kama vile Marekani habari hii ingeripotiwa kwa style hii?
Je,haya ndio maadili?
Kama ni maadili,maadili yanasemaje kuhusu jambo hili?
Je,mnawatendea haki watazamaji wenu?
Je,angekuwa ametuhumiwa mtu mwingine mngefanya mlivyofanya?
Hivi maadili yanayoongoza vyombo vya habari kama magazeti ni tofauti na maadili ya vyombo vya habari kama Television?
Kama hoja ni muda,sehemu ipi ya clip hiyo ilipaswa kurushwa na ipi ilipaswa kutorushwa kwa kigezo cha kulinda muda?
Kama sheria na kanuni ni zile zile,mbona magazeti yanakuwa huru kuripoti baadhi ya matukio kwa uwazi kabisa kuliko Television?
Ndugu yangu mwana-JamiiForums hapo ulipo naomba nawe useme kuhusu tv ulioangalia wameirushaje hiyo clip ya Lissu kwenye taarifa zao za habari ili tuweke mambo sawa.
Nimesoma magazeti mawili online muda huu naona nayo yamekwepa kabisa kumtaja muhusika kama hii clip iliyopo hapa JamiiForums inavyotuhabarisha.
Wameshindwa hata kumnukuu Lissu!
Hivi ingekuwa katika nchi za wenzetu kama vile Marekani habari hii ingeripotiwa kwa style hii?