Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 25,168
- 48,446
Kwa mfano mtu alighushi cheti akawa Askari Polisi, akamkamata mtu, huyo mtu akafunguliwa Mashitaka Mahakamani, Mahakamani akahukumiwa na Hakimu aliyeghushi cheti chake pia, akapelekwa Gerezani ambako nako kwa wakati fulani alilindwa na Askari Magereza aliyeghushi cheti. Je mtu huyu anaweza kushitaki kwa kukamatwa isivyo halali, kuhukumiwa na mtu asiye na sifa na kushikiliwa kifungoni na Askari Magereza aliyeghushi cheti?
Mzazi anampeleka mtoto wake shule ya Msingi, sekondari na mpaka chuo kikuu. Huko kote kwa wakati fulani alifundishwa na waalimu walioghushi vyeti. Huyu mtu usomi wake ni halali au ni haramu. Kitendo cha kufundishwa na waalimu walioghushi vyeti kinachukuliwa kama ni kosa?
Mama mjamzito kafika Hospitali, kapokelewa na Muuguzi aliyepata kazi hiyo kwa kughushi cheti, akaandikiwa dawa na Daktari aliyeghushi cheti na hatimaye akasaidiwa kujifungua na Mkunga ambaye naye alighushi cheti chake hata akaupata huo ukunga. Mama huyo ana haki ya kufungua mashitaka dhidi ya serikali kwa kuhatarisha maisha yake kwa kuajiri watu walioghushi vyeti?
Mzazi anampeleka mtoto wake shule ya Msingi, sekondari na mpaka chuo kikuu. Huko kote kwa wakati fulani alifundishwa na waalimu walioghushi vyeti. Huyu mtu usomi wake ni halali au ni haramu. Kitendo cha kufundishwa na waalimu walioghushi vyeti kinachukuliwa kama ni kosa?
Mama mjamzito kafika Hospitali, kapokelewa na Muuguzi aliyepata kazi hiyo kwa kughushi cheti, akaandikiwa dawa na Daktari aliyeghushi cheti na hatimaye akasaidiwa kujifungua na Mkunga ambaye naye alighushi cheti chake hata akaupata huo ukunga. Mama huyo ana haki ya kufungua mashitaka dhidi ya serikali kwa kuhatarisha maisha yake kwa kuajiri watu walioghushi vyeti?