Sumbawanga kweli ni hatari!!

Sumbawanga kweli ni hatari!!

chilamanyika

JF-Expert Member
Joined
Nov 20, 2016
Posts
405
Reaction score
272
Ni mbwa mmoja mwenyewe tabia za kushangaza,
Mnyama huyu anapatukana mji wa Laela wilaya ya sumbawanga vijijini mbwa huyu kwa muda mrefu amekua na tabia ya kuhudhulia misiba yote inayo tokea mjini hapo,
Kitu ambacho kinawashangaza wakaazi wa eneo hilo ni kwanba mbwa huyu hua anajuaje misiba inayo tokea kila kona ya mji? Na kibaya zaidi hajulikani mmiliki wake ni nani?
Majuzi mnyama huyu aliwashangaza watu wenyeji na wageni waliokua wakiuaga mwili wa mzee mmoja maalufu sana baada ya kuona mbwa huyu amepanga foreni kwenda kuaga kama walivyo fanya binadamu, wakisimulia kwa undani baazi ya watu msibani hapo walisema mbwa huyo huambatana na waombolezaji hadi kanisani/msikitini na baadaye hutoweka msibani Siku ya matanga
IMG_20181029_140630.jpg
IMG_20181029_140642.jpg
IMG_20180409_132503.jpg
 
Suala la kifo ni siri kubwa lakini kuna baadhi ya viumbe wakiwemo baadhi ya binadamu na wanyama hujua kabla ya kutokea. Ilinishangaza maeneo ya Moshi vijijini kuna vichaa ambao huenda vijiji vya mbali kufuata misiba kwa kuota. Hawaambiwi na mtu yeyote ila kila msiba katika kila kijiji hata kama kwenye kijiji anachotoka hakuna anayejua yeye ataenda.
 
sioni cha ajabu hapo, labda kama huwajui mbwa. wewe unadhani mbwa huwa wanajua vipi kua kuna jike liko kwenye joto upande wa pili wa mji?? mbwa ni miongoni mwa wanyama wenye uwezo mzuri wa kujifunza na kutunza kumbukumbu. kwenye misiba kuna vitu ambavyo ni common kama vile upatikanaji rahisi wa chakula (mbwa ni bingwa wa kufuata harufu), vilio vya waombolezaji (mbwa anauwezo mzuri wa kusikia na kutambua maana ya sauti) N.K
kwa taarifa yako huko moscow kuna mbwa wa mitaani ambao wanauwezo hadi wa kupanda treni na kwenda mitaa yenye chakula kisha wanapanda tena treni kurudi kwenye territory zao, mbwa hao pia wanauwezo mkubwa wa kosoma nyuso za watu kiasi kwamba hua wanaweza kutofautisha mtu mkarimu atakae wapa chakula na mtu asiyejali!!!
 
sioni cha ajabu hapo, labda kama huwajui mbwa. wewe unadhani mbwa huwa wanajua vipi kua kuna jike liko kwenye joto upande wa pili wa mji?? mbwa ni miongoni mwa wanyama wenye uwezo mzuri wa kujifunza na kutunza kumbukumbu. kwenye misiba kuna vitu ambavyo ni common kama vile upatikanaji rahisi wa chakula (mbwa ni bingwa wa kufuata harufu), vilio vya waombolezaji (mbwa anauwezo mzuri wa kusikia na kutambua maana ya sauti) N.K
kwa taarifa yako huko moscow kuna mbwa wa mitaani ambao wanauwezo hadi wa kupanda treni na kwenda mitaa yenye chakula kisha wanapanda tena treni kurudi kwenye territory zao, mbwa hao pia wanauwezo mkubwa wa kosoma nyuso za watu kiasi kwamba hua wanaweza kutofautisha mtu mkarimu atakae wapa chakula na mtu asiyejali!!!
Hii imeshamaliza!
 
Brother acha kuzuga watu hapa jamvini huyu mbwa ni wako wewe mwenyewe maana inasemekana wewe ndo mchawi mkubwa wa hicho Kijiji.u sharoga watu kibao hapo.acha unafiki broo
 
Brother acha kuzuga watu hapa jamvini huyu mbwa ni wako wewe mwenyewe maana inasemekana wewe ndo mchawi mkubwa wa hicho Kijiji.u sharoga watu kibao hapo.acha unafiki broo
Ningekua najua hiyo sayansi hiyo mbwa angehudhulia mazishi yako kesho
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom