Mbona mihemko haiwaiishi? Uchaguzi ulishaisha...au ndio jinsi kutekeleza kauli mbiu ya HapaKazi tu. Nilifikiri kama kweli mna mapenzi mema na hii nchi mnngeacha kubwabwaja maneno mithili ya taarabu ktk jukwaa hili, na na kuanza kutekeleza kauli mbiu ya HapaKazi tu kwa kuchapa kazi, kuhimiza mshikamano, umoja wa kitaifa ktk kuleta maendeleo. Nilitegemea wanalumumba wangekuwa kwenye vijiwe vya wanamabadiliko kuhubiri amani, kuhimiza kufanya kazi na kuachana na ulofa kama wasemavyo, pia kuwa wa kwanza kupigana kuondoa ukabila, ukanda na udini. CHA AJABU MNAPALILIA MIZIZI YA UKANDA NA UKABILA, Hili limekuwa wazi hata kwa baadhi ya viongozi waliochaguliwa.