Haya ndo madhara ya kuwaweka waliokimbia maths katika nyazifa zinazohitaji uwezo mkubwa wa ku-reason ili kuja na sababu halisi na za msingi kwenye matukio yanayogusa watu wengi. Ivi ukitilia shaka jambo kinachofuata ni hukumu, kuna haja kweli nyie Sumatra kutuambia mnatilia shaka sifa za madereva wakati sifa za udereva ziko wazi?na kama ni walevi si mkawapime, au hizo gari zinaendeshwa na msukule so wanaoendesha hawajulikani wala hawaonekani? Acheni u....ga nyie Sumatra, hata hizo ajali mlizo-account zinavyoonyesha zinatokana na huo ubabaishaji wa Serikali kutojenga service road za waenda kwa miguu au waendesha baiskeli katika maeneo ya makazi ya watu ambapo barabara kuu zinapita.
mambo hayo yameanza watu wa kasikazini kupigwa vita . na haitaishia hapo mambo tutajuzana tu.
Nanukuu ''mamlaka inatilia shaka sifa za madereva wa kampuni ya mabasi dar express'' nimeshindwa kuwaelewa kabisa hawa summatra,hivi wanafikiri mmiliki wa dar express ni mjinga kiasi gani akampe gari yake dereva asiyekuwa na sifa? hicho kitu hakiwezekani kabisa kutokana na dhamani ya gari zake kama vile scania izira ambazo mpaka sasa hakuna mbongo mwingine aliyeweza kununu ikiwa mpya hata used walishindwa wakaishia kwny marcopolo used, na sasa ameingiza kitu Benzi,bongo nzima hakuna hii,leo uje useme anaajiri madereva wasiokuwa na sifa? gari zake sio yutong au malori ya kuchongea body pale quality grp,malva,banbross or maste kule kenya.sumatra watoe sababu za msingi waache ubabaishaji. Hao watu mmoja mmoja waliogongwa kwa kanuni za udereva tena hasa ule wa abiria ni bora kumgonga mkatiza barabara mmoja akafa kuliko kumkwepa ukaangusha gari ukaua hamsini. Sijui hawa sumatra viongozi wake wamesoma wapi.au kwa sababu mmiliki wa dar exprss ni mlokole na hatoi rushwa?