SUMATRA mna tatizo gani na usafiri Dar?

hesabu900

Member
Apr 18, 2017
78
62
Habarini,

Kipindi cha ugonjwa wa corona kutokana na shule kufungwa na daladala kukatazwa kujaza abiria yaani iwe level seat. Serikali ilitoa ruhusa kwa ma bus binafsi hasa yale yaliyokuwa yanasafirisha wanafunzi nayo yafanye kazi za daladala na ikaelekeza waombe vibali SUMATRA, unaomba kibali na kama una vigezo basi unalipia unapata kibali cha miezi minne minne.

Ajabu sasa hivi vibali havijaisha wafanyakazi wa SUMATRA wanasimama barabarani na kuanza kukamata magari na kuomba rushwa au kutishia kuipelea gari yard.

Swali langu hivi kama hivi vibali vimesitishwa kwanini wasitangaze magazetini au radioni tukaelewa kama tulivyotangaziwa wakati tunapewa hivi vibali. Kumbuka hivi vibali tumevilipia. Au si waseme kama kibali kikiisha iwe basi hakuna ku-renew tena. Kuliko kukamata kimya kimya na kusumbua magari.

Mfanyabiashara anafanya biashara na analipa kodi hivi unapomsumbua unakuwa na lengo gani. Atalipa vipi kodi. Au kufanya biashara ni dhambi? Hawa ndio wanaofanya wananchi wawe na chuki na serikali yao.

Usafiri wa Dar miaka yote ni wa tabu yaani abiria ni wengi kuliko idadi ya magari.

Sioni sababu ya kukamata au kusumbua gari ambayo ina vibali vyote halali vya serikali.

Tafadhali tunaomba Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam. Pamoja na Takukuru wafuatilie hili. Na ikiwezekana hawa watu wachukuliwe hatua. Tupo tayari kuwataja.

Asante.
 
LATRA ni shida tena kubwa sana. Haieleweki wanafanya nini.

Sijui iliundwa ili wapeane ukurugenzi?
 
Yaani wakishaona mfumo unafanya kazi vizuri na wananchi wamefurahia kwa kuondokewa kero zao za usafiri, roho zinawauma wanaharibu mfumo mzuri na kufosi limfumo lao la usafiri litakalo waongezea wananchi kero kubwa ya usafiri ili kuwaharibia amani yao ya maisha na kuwaongezea shida na msongo wa mawazo ya usafiri na kuwaongezea wananchi ugumu wa kushi kwa amani katika nchi yao.
 
Kwanza nakushauri upende kusikiliza taarifa za habari na ukiweza soma habari zote kwenye magazeti.
SUMATRA ilikufa zamani sana, sana, sasa ipo LATRA.
 
Yaani wakishaona mfumo unafanya kazi vizuri na wananchi wamefurahia kwa kuondokewa kero zao za usafiri, roho zinawauma wanaharibu mfumo mzuri na kufosi limfumo lao la usafiri litakalo waongezea wananchi kero kubwa ya usafiri ili kuwaharibia amani yao ya maisha na kuwaongezea shida na msongo wa mawazo ya usafiri na kuwaongezea wananchi ugumu wa kushi kwa amani katika nchi yao.
Yaani ni ngumu kuwaelewa. Hivi kuna tatizo gani kwa gari kubeba abiria ( kwa vibali vya muda ) tena wanavilipia. Mfano shule au vyuo vimefungwa. Kuna tatizo gani kuomba kibali cha muda tena kinalipiwa. Au hawaoni hawaoni shida ya usafiri dar. Hawaoni ambavyo watu wanabanana kwenye mwendo kasi.
 
latra ina vijana vidogoo vina majibu ya kunya sana na nidhamu ni 0. Wale jamaa wenye weledi wa usimamizi hawako tena sijui walienda wapi akina shayo waliokuwa wanafanya ukaguzi hadi usiku. kahatano vipi mkuu upo au nawe umesepa?
 
Back
Top Bottom