Sumatra mko 'biased'

Sumatra mko 'biased'

TWIZAMALLYA

JF-Expert Member
Joined
Oct 1, 2011
Posts
397
Reaction score
81
Ongezeko la nauli lililotangazwa hivi karibuni na SUMATRA inaonyesha ni jinsi gani hawa watu walivyonunuliwa na wafanyabiashara.Kwa jinsi hali ilivyo kwa sasa mimi binafsi sikutegemea kama hawa watu watakuja na move hiyo.

vipato vya raia wengi viko duni sana,tumeshuhudia waalimu wakidai nyongeza ya mishahara yao lakini bahati mbaya walibezwa tu nao wakaja na staili ya mgomo baridi ambayo madhara yake kila mtu mwenye macho ameyaona,ni matokeo ya Kawambwa.

Funny thing hawa watu walio kwenye hali mbaya wanaongezewa matatizo tena. Kwa kusema kweli mimi sijawahi kuona kitu chochote cha maana ambacho SUMATRA wamefanya kuwalinda watumioaji wa vyombo vya usafiri.Moja ya kero kubwa sana ambayo wao wana'ignore' ni daladala kukatisha Route zake.

Mfano ukiwa posta mpya unaenda mbezi ya Kimara huwezi kupata daladala ya kwenda huko,sanasana utapata gari ya Ubungo kuzungukia feri,ukifika Ubungo utapata gari ya Kimara,na ukifika kimara unapata gari ya kwa Msuguri,ukifika kwa msuguri unapata gari Mbezi.Haya yanafanyika na Sumatra wako maofisini wamekaa tu.

Kwa vile nchi hii imejaa ufisadi kila kona maamuzi kama ya sumatra yataendelea kutolewa.Kwa kupandisha kwenu hizo Nauli angalieni mfano huo juu muone mtu wa kima cha chini atawezaje kumudu hizo gharama mlizombebesha
.
 
hivi hao sumatra vipato vyao vikoje?? tuambiane au nyie wenzetu mnapanda daladala bure?? au wote hapo ofisini mnamiliki V8? kama jibu ni hapana basi tuangalieni na wenzenu.
 
Haya ni maandalizi kwa mwekezaji atakaetoa huduma za usafiri hapa dar. daladala za dar zinaonjeshwa hiyo nauli mpya tu. lengo ni kwa huyo mwekezaji. sasa hivi leseni ya daladala za kariakoo au posta ikiisha hakuna ku renew na ndio sababu daladala zimepungua kwenye route hizo
 
Back
Top Bottom