SUMATRA Haiendani na kasi ya magufuri ivyo ni bora ivunje

Nyamuhokwa

Member
Feb 20, 2014
17
3
Raisi wa awamu ya tano ndugu John Pombe Magufuri, ameanza uongozi kwa kasi kubwa ambayo imefurahisha wananchi walio wengi. Ameanza kwa kubana ukwepaji kodi bandarini na sehemu nyingine chache. Lakini pamoja na jitihada zake, kuna baadhi ya taasisi zinamwangusha. Mfano mmoja wapo ni SUMATRA. Hawa ni kama hawajui majukumu yao. SUMATRA kazi yao ni kusimamia usafiri wa majini na nchi kavu. Kuhakikisha vyombo vya usafiri viko safi na salama. Na abiria wanapatiwa tiketi. Lakini cha ajabu suala la tiketi kwenye dala dala limesaulika kabisa. Makondakta kwa sasa hawatoi tiketi. Kitendo cha kutotoa tiketi kinachofanya na makondakta hao kinaikosesha serikari mapato makubwa. Chukulia mzunguko wa daladala nchi nzima je ni kiasi gani cha pesa kinapotea kwa siku, wiki, mwezi. Je SUMATRA Wanasubiri mpaka Raisi awakumbushe wajibu wao.
 
Back
Top Bottom