Kweli alikuwa hana uwezo?Najua nitapigwa mishale ya kutosha ila kwangu mimi kanumba alikua overrated
Akitaka demu atamwingiza kwenye tasnia.Mtu kama Patcho Mwamba hakuwa na hobby kabisa ya kuigiza ila ushawishiaa Kanumba jamaa akaanza kuigiza na karibia kila filamu ya Kanumba lazima amuite Patcho wacheze naye.
Kifupi Kanumba alikuwa mtu wa kufosi wengine aliowaleta kama Patcho at least wapo vizuri ila wengine walisababisha tasnia nzima ya filamu kuonekana hovyo.
Nonsense...Huyo analeta ujuaji mwingi na hana anachokijua.
Nakutolea mfano girlfriend filamu iliyochezwa na T.I.D ,AY,Monalisa,Ndende,Jay Mo,Jafarai, Nina nk , waliunganisha nguvu watu wanne ,Maneno Tamba, Sultan Tamba, mume wa Monalisa ambaye ni mkenya anaitwa George Tyson ambaye kwa sasa ni marehemu baada ya kupata ajali, na kuna mwingine jina limenitoka.
Yote hayo yakifanyika chini ya Tamba Arts group.
Upambanaji...Yes.Kweli alikuwa hana uwezo?
Kweli alikuwa sio mpambanaji?
Haha!...
Huo ndio ukweli mchungu ,Kanumba alikuwa overated .Najua nitapigwa mishale ya kutosha ila kwangu mimi kanumba alikua overrated
Ndio ilikuwa michezo yake hiyo🤣🤣🤣🤣🤣🤣Aki
Akitaka demu atamwingiza kwenye tasnia.
kama filamu ipi?Kwangu ni bora zilivyokosa muendelezo maana si kwa majini yale yaliyokuwa yanavuka barabara kwakuangalia kushoto na kulia mtu akiwaza lazima aangalie juu ya dali
Yakweli yale?Kosa lake ni kukiuka makubaliano na shetani angekuwa hai Hadi leo
CV zinatutisha hizi 😁Nonsense...
Nimekuwa Katibu Mkuu wa Tanzania Film Federation na Board Director wa Tanzania Film Board. Mimi pia ni mwasisi wa Bongo Movie na nimefanya kazi na wasanii wengi ambao walikuja kuwa maarufu.
Narudia tena kusema HUJUI CHOCHOTE kuhusu film industry. Kwenye filamu ya Girlfriend, Tamba Arts Group hawahusiki wala Maneno Tamba hahusiki.
Sultan Tamba na Kesa Mwambeleko walipewa credit kwa kuwa walikuja na idea lakini kazi nzima ilifanywa na George Otieno Tyson...
Hii hata mimi niliiogopa aisee🤣🤣🤣.Chite chite Chite Ukae 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 🤣 yule bibi mshenzi alikua ananitisha , kweli uhalisia ulikuwepo watu wanakutaka nyumbani
Ahahaha jamaa alikua anadai laki 5,, daah yule Rasta aliwapiga mishale hahaha..Sultani Tamba movies zake ziliegemea vitisho zaidi ila Mussa Banzi alikuwa anapiga kotekote mapenzi na vitisho.
Kuna movie ya Sultan Tamba inaitwa Wasiwasi, wanaume wawili wanagonga mlango usiku wa manane, mlango ulipofanguliwa wanauliza wapi kuna msiba.
Aliefungua mlango anashangaa na kusema hana taarifa za msiba, wakamuambia msiba upo tena ni wa mtu wako muhimu fanya utafiti utajua. Wanaondoka!
Yule jamaa hakuendelea kulala, akatoka kulelekea kwa mchumba wake anaetaka kumuoa karibuni, kufika tu anasikia kama mtu anaugulia maumivu kupitia dirishani. Kuchungulia anakuta mchumba wake amepigwa kisu cha tumbo.
Akaenda haraka kwenye mlango mkubwa ambao ulikuwa wazi akaingia ndani amuokoe ila ikashindikana.
Mama yake na yule binti nae akaamka maana alisikia sauti na kukurukakara, kuingia kwa binti yake anakuta keshakufa na mchumba wake ndio kashikilia kisu.
Ikaonekana yeye ndio kaua jumba bovu likamuangikia.
Na kuna nyingine inaitwa Miwani meusi!
Haha! Nilitaka kumwonesha mleta uzi kuwa nakifahamu ninachokisema...CV zinatutisha hizi
Ni kweli movies za part 1&2 zilikuja kuharibu maana watayarishaji walilazimishwa kurefusha matukio ili filamu zao ziwe ndefu. Utakuta mtu kwenye movie anatembea barabarani dakika 5, establishing shot ya mji dakika saba! Issue ya Gabriel Mtitu (Game 1st Quality) ni kweli hatajwi ila ndiye aliyemwibua Kanumba na wasanii wengine wengi tu... Movies zote za mwanzo za Kanumba (ukiacha zile alizotengeneza kwa Steps) zilikuwa za Mtitu...Issue ya movies kuwa na Part 1 na Part 2 nadhani msambazaji alikuwa anawalazimisha na wenyewe walililalamikia sana.
Kingine kinachinisikitisha ni kuwa mtitu wa game first quality huwa hatajwi ilhali yeye ndio alitengeneza movie za mwanzo za Kanumba na Ray kama Johari, sikitiko langu, A point of No return, oprah na nyingine nyingi
Huyu jamaa movies zake zilikuwa kali ila zilizohit ni zile zenye mahadhi ya kinaija
Kingine, Mussa Banzi na sultani, movies zao zilikuwa na uhalisia sana sanaa na story kali ila kwenye uigizaji kuna walakini. Kuna kama game of love, watu wanaigiza kama wanaigiza maneno waliyokariri badala ya kuuvaa uhusika