Sultan Suleiman khan na viongozi wetu Africa

Sultan Suleiman khan na viongozi wetu Africa

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
17,180
Reaction score
16,866
Naangalia tamthilia sultan Azam tv. Nimevutiwa na uhusika wa sultan Suleiman khan, hureem, mawaziri na washauri wake wanaomzunguuka.

himaya ya Otthoman inaenda kuanguka Kwa hila za Hurem lakini hata mawaziri na washauri wao wanaogopa kumshauri dhidi ya hila za Hurem ingawa wasaidizi wake wote wanaufahamu umbaya wa Hurem. Mfalme sultan amejikinga dhidi ya ushauri wowote dhidi ya Hurem. Washauri wake wanaogopa kuchinjwa na mtawala wa dunia mtukufu sultan Suleiman khan. kasha wapoteza mawaziri wake wakuu, mama yake, dada yake na shemeji zake Kwa hila za Hurem lakini hataki kuambiwa chochote kibaya kuhusu Hurem.

Viongozi wa kiafrika wengi wao wanafanana na Suleiman, hawataki kuambiwi kuhusu ubaya wao.
 
Naangalia tamthilia sultan Azam tv. Nimevutiwa na uhusika wa sultan Suleiman khan, hureem, mawaziri na washauri wake wanaomzunguuka.

himaya ya Otthoman inaenda kuanguka Kwa hila za Hurem lakini hata mawaziri na washauri wao wanaogopa kumshauri dhidi ya hila za Hurem ingawa wasaidizi wake wote wanaufahamu umbaya wa Hurem. Mfalme sultan amejikinga dhidi ya ushauri wowote dhidi ya Hurem. Washauri wake wanaogopa kuchinjwa na mtawala wa dunia mtukufu sultan Suleiman khan. kasha wapoteza mawaziri wake wakuu, mama yake, dada yake na shemeji zake Kwa hila za Hurem lakini hataki kuambiwa chochote kibaya kuhusu Hurem.

Viongozi wa kiafrika wengi wao wanafanana na Suleiman, hawataki kuambiwi kuhusu ubaya wao.
Wengi wanaidharau ile tamthilia kwakuwa hawaifuatilii na wengine ndio wale wenye redio tu makwao[emoji23]

Ila ukija nyuma ya pazia ile tamthilia imeeleza mengi hasa hatari ya mwanamke katika mahusiano kama usipokuwa nae makini. Pia Sultan suleiman ni mwanaume goi goi ambae hacgunguzi habari anazoletewe ya kazi kuitikia ndio tu

Wanawake zake ndio chanzo cha anguko la ile himaya, maana wataanza kuuwana wenyewe kwa wenyewe, dam itamwagika sana na huko. Mbeleni ndio hatari watauwana ndugu kwa ndugu. Sultan atamuua mwanae mustapha kwa mikono yake, shahazad selim atakuja kumuuwa mdogo wake beyazid pamoja na watoto

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sultan amejitengenezea mazingira ya kuogopwa kushauriwa. Wasaidizi wake wote hakuna anayethubutu kumshauri hata kama kuna hatari za wazi kabisa za himaya yake kuporomoka. Mapenzi gani hayo!!
 
Back
Top Bottom