Lukansola
JF-Expert Member
- Sep 5, 2010
- 5,435
- 1,597
Hamjambo?
Leo nimekikumbuka hiki kiboksi ambacho nilizoea kukiona sehemu mbalimbali ambazo zinatoa huduma, kama kwenye mabenki ofisi za serikali nk. Kwa ajili ya wateja kutoa maoni yao, kiboksi hiki huwa kimetengezwa kwa mbao, kimepigwa vanish halafu kina mlango/mfuniko uliofungwa kwa kufuli au vingine huwa na vitasa kama vile vya milango ya kabati.
Ingawa siku hizi sivioni sana viboksi hivi, bado kumbukumbu zangu zinaniambia kwamba sikuwahi kuona siku wala mahala popote kisanduku hiki kikifunguliwa. Zaidi ni kwamba vyote nilivyoviona vilikuwa vimejaa vumbi mpaka kwenye matundu ya funguo. Je ni mimi tu mwenye mawazo haya? Au kuna mmoja wetu amewahi kufungua kisanduku hicho huko afanyako kazi?
Leo nimekikumbuka hiki kiboksi ambacho nilizoea kukiona sehemu mbalimbali ambazo zinatoa huduma, kama kwenye mabenki ofisi za serikali nk. Kwa ajili ya wateja kutoa maoni yao, kiboksi hiki huwa kimetengezwa kwa mbao, kimepigwa vanish halafu kina mlango/mfuniko uliofungwa kwa kufuli au vingine huwa na vitasa kama vile vya milango ya kabati.
Ingawa siku hizi sivioni sana viboksi hivi, bado kumbukumbu zangu zinaniambia kwamba sikuwahi kuona siku wala mahala popote kisanduku hiki kikifunguliwa. Zaidi ni kwamba vyote nilivyoviona vilikuwa vimejaa vumbi mpaka kwenye matundu ya funguo. Je ni mimi tu mwenye mawazo haya? Au kuna mmoja wetu amewahi kufungua kisanduku hicho huko afanyako kazi?