Subramaniam aendelea na Kazi pamoja na kuwa na expired work Permit
Naona mchezo mchafu unafanywa kuhusu suala la uhalali wa aliyekuwa Meneja Mkuu wa Fedha wa kampuni ya IPTL, Dk. Magesvaran Subramaniam, raia wa Malaysia.
Ninanavyofahamu baada ya kumaliza mkataba wake wa ajira IPTL, na kukabidhi ofisi kwa uongozi, kibali chake cha kuishi nchini kilimalizika na hivyo kutakiwa kuondolewa nchini baada ya kulipwa haki zake zote alizostahili.
Uamuzi huo ulizingatia muda wa mkataba wa ajira yake ambao ni wa miaka miwili kuanzia Februar mosi 2009. Kibali chake cha kuishi nchini chenye Na. 079388 kilicholipiwa Dola 700 za Marekani kilimalizika muda Februari 19, 2011.
Inashangaza kuona hajaondoka na inavyoonekana, anahangaika kutafuta kubaki nchini kwa vyovyote. Ushahidi wa hilo ni kuendelea kila siku kufika IPTL na kufanya kazi.
Upo wasiwasi kwamba analindwa na kwa kuwa sasa inaendeshwa kwa utaratibu wa "ufilisi mahsusi" chini ya Wakala wa Usajili na Ufilisi (RITA) inayoongozwa na Phili Saliboko.
Zipo fununu jwamba kuna jitihada za kumpatia kibali kipya cha kufanya kazi nchini hatua ambayo ni kinyume na sheria ya Uhamiaji. Mgeni yeyote akimaliza muda wa kibali chake cha awali, anapaswa kuondoka nchini ndipo aanze utaratibu wa kupata kibali kingine. Hastahili. Nchi yetu ina wataalamu wengi wa masuala ya fedha.
Suala lake linahitaji kufuatiliwa na vyombo husika ikianzia na Idara ya Uhamiaji yenyewe, na Usalama wa Taifa. Ufuatiliaji uanze haraka chini ya usimamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ili kuzuia mbinu chafu.
Mfanyakazi Mzalendo
Independent Power Tanzania
Limite (IPTL)
Dar es Salaam
Source: MwanaHalisi April 20, 2011
Naona mchezo mchafu unafanywa kuhusu suala la uhalali wa aliyekuwa Meneja Mkuu wa Fedha wa kampuni ya IPTL, Dk. Magesvaran Subramaniam, raia wa Malaysia.
Ninanavyofahamu baada ya kumaliza mkataba wake wa ajira IPTL, na kukabidhi ofisi kwa uongozi, kibali chake cha kuishi nchini kilimalizika na hivyo kutakiwa kuondolewa nchini baada ya kulipwa haki zake zote alizostahili.
Uamuzi huo ulizingatia muda wa mkataba wa ajira yake ambao ni wa miaka miwili kuanzia Februar mosi 2009. Kibali chake cha kuishi nchini chenye Na. 079388 kilicholipiwa Dola 700 za Marekani kilimalizika muda Februari 19, 2011.
Inashangaza kuona hajaondoka na inavyoonekana, anahangaika kutafuta kubaki nchini kwa vyovyote. Ushahidi wa hilo ni kuendelea kila siku kufika IPTL na kufanya kazi.
Upo wasiwasi kwamba analindwa na kwa kuwa sasa inaendeshwa kwa utaratibu wa "ufilisi mahsusi" chini ya Wakala wa Usajili na Ufilisi (RITA) inayoongozwa na Phili Saliboko.
Zipo fununu jwamba kuna jitihada za kumpatia kibali kipya cha kufanya kazi nchini hatua ambayo ni kinyume na sheria ya Uhamiaji. Mgeni yeyote akimaliza muda wa kibali chake cha awali, anapaswa kuondoka nchini ndipo aanze utaratibu wa kupata kibali kingine. Hastahili. Nchi yetu ina wataalamu wengi wa masuala ya fedha.
Suala lake linahitaji kufuatiliwa na vyombo husika ikianzia na Idara ya Uhamiaji yenyewe, na Usalama wa Taifa. Ufuatiliaji uanze haraka chini ya usimamizi wa Wizara ya Mambo ya Ndani, ili kuzuia mbinu chafu.
Mfanyakazi Mzalendo
Independent Power Tanzania
Limite (IPTL)
Dar es Salaam
Source: MwanaHalisi April 20, 2011