Jamani hii aibu itatuondoke lini. Nuimekuwa nikiangalia movie za kibongo ile channel ya movie za kiswahili kupitia DSTV, Jamani ni aibu yaani unaogopa kabisa subtitles ya kuaibisha kabisa na imerushw, a kitu cha ajabu kabisa lakini unshangaa hivi hawa jamaa wanapotengeneza hizi subtitles huwa kweli wanajua wanachokifanya. Halafu wale DSTV wanazirusha tu bila hata kuzifanyia kazi. Mtu unakuta anasema nilikuona kwenye sub title wameandika I so you yaani makosa Ni mengi na huwa najiuliza lakini kwa nini wasitafute wataaalamu wawasaidie kutafsiri. Tunaanikwa uchi kabisa kimataifa. Lazima bidhaa kupelekwa sokoni zipitie viwango na dhani hata TBS wanatakiwa kufika huku jamani