Suala la Escrow: Asante wabunge wetu, Mungu awabariki!

Suala la Escrow: Asante wabunge wetu, Mungu awabariki!

masopakyindi

Platinum Member
Joined
Jul 5, 2011
Posts
18,625
Reaction score
14,591
Kwa kweli hata kabla ya kuhitimishwa kwa mjadala wa Escrow account, nimependezwa sana msimamo wa umoja katika kulitazama suala la wizi wa fedha za umma zilizomo katika Escrow account.

Nimewaona wabunge, mawaziri, wenyeviti wa kamati mbali mbali, wote wamempinga wazi wazi waziri Muhongo na wahujumu wengine.
Hili ni funzo kubwa kwa wale wana CCM waliokuwa na maoni potofu, na hivyo basi kushabikia wezi na si CCM.
Cha kujivunia ni kwamba wabunge wote na wa vyama vyote walionyesha msimamo unaofanana-kuitetea nchi na Taifa.
Kwa hili Mungu awalinde.
 
Hata huku kwangu TANESCO weshachukua umeme!
 
Huku pia tanescoccm wamekata umeme tusitazame bunge,ila namshukuru Dr Mengi kwani ITV na RADIO ONE watarudia
 
Muhongo kwa kweli leo amedhalilishwa kwa statement zake za uongo.
Kingwangwala kamuita Waziri Muhongo ni muongo hajapata kuona.
Na mbunge Mpina vile vile amerudia kuwa statements za Muhongo ni za uongo.
 
Katika suala lililonisikitisha ni taarifa kuwa yule kijana mwanasheria aliyegundua utapeli wa Seth , yule Singa singa kuwa ni tapeli , amefunguliwa mashitaka ya kupandikizwa ya mauaji.

Kweli hao watu ndio walimuua yule waziri wa fedha , Mgimwa.
 
Back
Top Bottom