Stress za Long Distance Relationship

Stress za Long Distance Relationship

Mbagala stendi

JF-Expert Member
Joined
Nov 8, 2020
Posts
343
Reaction score
407
Niaje niaje ladies & gentlemans ...
Ni mitano tena lazima tutoboe au sio mazee.

kila mwanadamu aliyekamilika akishafikia umri fulani wa kujitambua na kujihandle anahitaji Rafiki au Mtu wa karibu wa kuanzisha nae mahusiano ya kimapenzi.

kijana aidha ladies au gentles nakushauri chagua mtu aliye sahihi kwako na sio kuchagua eti kwa sababu ya status ya mtu fulani my friend utalia na kusaga meno kwenye giza totolo achana na hawa viumbe wanaojihita pisi kali kwa sababu hawa wenye status ni lazima utatumia nguvu nyingi hilikuendesha. Mahusiano so itakubidi kuwe na investment za muda ,pesa na akili pia.

Mimi ni mmoja wa wahanga wa PIS KALI, napenda kishea nanyi experience niliyoipata enzi nipo shule fulani hivi high school kuna kibinti kizuri sana kilitokea kunpenda sana. Alikuwa kama karogwa maana alikuwa ananipenda kwa dhati bila kipimo alihaidi kubadili dini awe mkristo mafans na mafellows wa shule wakampatia jina Charity lilimpendeza sana.

Baada ya kumalza shule kila mtu akaelekea kwake mimi nikarudi dar nae akaenda moro so tungaanza lasmi kuwa long distance relationship yani hapa ndipo panaponifanya nianzishe thread hii

Jamani hakuna long distance relationship ukiona mwenza wako ameenda far away from you hachana nae hakuna mapenzi tena hapo ukiona kuna ubize bize kula kona mapema kabla hata ya kuja kuanzisha thread hapa muda ni wathamani sana my friend.pis kali ilinitesa sana kila kukicha ni stress tu. Unaweza mpigia hasipokee simu na akipokea anasema yupo bize, ukimtext hajibu na hakijibu anajibu kifupi hawa viumbe wanaweza kufanya wakakugeuza kichwa chini miguu juu

lakini nilivumilia ndani ya miezi mitatu maji yaliponifika shingoni ni kaamua kufanya maamuzi magumu nikakubali kumwacha aendezake japo nilikuwa bado nampenda lakini nilikuwa sina jinsi alinitesa sana kifikra maumivu yasiyo hitaji dawa ujui nini hasa kinachokuuma lakini mwili unakuwa dhaifu.

mapenzi bana hacha tu kijana kama bado ujafikia umri wa kuoa achana na mapenzi tafuta pesa kama ni mwanachuo ebu soma huandae future yako muda haurudi nyuma usipoteze hata seconde moja katika maisha yako be true and follow your heart usiingie kwenye mahusiano bila kujua kuna effect mbili za mahusiano aidha break up or marriage.

asanteni na karibuni kwa experience.
 
Alafu huo ulikua utoto unakusumbua ww, badala ya kusoma unawaza mapenzi
Sio utoto kiongozi bali kuwa na mtu wa karibu ni jambo la kheri hasa kishuleshule kuna changamoto mbili tatu za kimasomo ndio inapelekea different gendee to be closer
 
Pole kwa experience yako, lakini siyo kweli.
Mimi nipo ktk long distance for 1 year now na kila kitu kinaenda sawa, so usikariri mkuu.
Kama ni mtu ambaye ni matured kabisa na umri umeenda na anajielewa, long distance relationships zinakuwa sawa. Lakini kwa hivi vijitu ndio vimemaliza tu high school, long distance relationship ni ngumu sababu ni wachanga kwenye mambo ya relationships na wanadanganyika kirahisi. Hivyo aliye karibu ndio analabua nyoka, wa mbali ni stress tupu kama jamaa sababu yeye ni wa pili au wa tatu hapo kwa huyo mdada.
 
Kama ni mtu ambaye ni matured kabisa na umri umeenda na anajielewa, long distance relationships zinakuwa sawa. Lakini kwa hivi vijitu ndio vimemaliza tu high school, long distance relationship ni ngumu sababu ni wachanga kwenye mambo ya relationships na wanadanganyika kirahisi. Hivyo aliye karibu ndio analabua nyoka, wa mbali ni stress tupu kama jamaa sababu yeye ni wa pili au wa tatu hapo kwa huyo mdada.
Nakubaliana nawe ujue long distance is nothing for the true love lakini kwa wakati hule ilikuwa vigumu kuendelea na long distance kwa sababu mmoja wetu alishaanza kuwekwa plan B au Plan C
 
Back
Top Bottom